< Warumi 2 >
1 Kwa hiyo hauna udhuru, wewe uhukumuye, kwa maana katika yale uhukumuyo mwingine wajitia hatiani mwenyewe. Kwa maana wewe uhukumuye unafanya mambo yale yale.
Therefore you have nothing to say in your own defence, whoever you are who set yourself up as a judge. In judging others you condemn yourself, for you who set yourself up as a judge do the very same things.
2 Lakini twajua kwamba hukumu ya Mungu ni ya kweli juu yao wafanyao mambo kama hayo.
And we know that God’s judgment falls unerringly upon those who do them.
3 Lakini wewe tafakari hili, wewe ambaye unahukumu wale wanaotenda mambo hayo ingawa nawe unafanya mambo yayo hayo. Je utaepuka hukumu ya Mungu?
You who judge those that do such things and yet are yourself guilty of them — do you suppose that you of all men will escape God’s judgment?
4 Au unafikiri kidogo sana juu ya wingi wa wema wake, kuchelewa kwa adhabu yake, na uvumilivu wake? Je, hujui kwamba wema wake unapaswa kukuelekeza katika toba?
Or do you think lightly of his abundant kindness, patience, and forbearance, not realising that his kindness is meant to lead you to repentance?
5 Bali kwa kadiri ya ugumu wako na kwa moyo wako usio na toba wajiwekea mwenyewe akiba ya ghadhabu kwa siku ile ya ghadhabu, yaani, siku ile ya ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu.
Hard-hearted and impenitent as you are, you are storing up for yourself Wrath on the ‘Day of Wrath,’ when God’s justice as a judge will be revealed;
6 Yeye atamlipa kila mtu kipimo sawa na matendo yake:
for ‘he will give to every man what his actions deserve.’
7 kwa wale ambao kwa uthabiti wa matendo mema wametafuta sifa, heshima na kutokuharibika, atawapa uzima wa milele. (aiōnios )
To those who, by perseverance in doing good, aim at glory, honour, and all that is imperishable, he will give Immortal Life; (aiōnios )
8 Lakini kwa wale ambao ni wabinafsi, wasioitii kweli bali hutii dhuluma, ghadhabu na hasira kali itakuja.
while as to those who are factious, and disobedient to Truth but obedient to Evil, wrath and anger, distress and despair,
9 Mungu ataleta dhiki na shida juu ya kila nafsi ya binadamu aliyefanya uovu, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia.
will fall upon every human being who persists in wrong-doing — upon the Jew first, but also upon the Greek.
10 Lakini sifa, heshima na amani itakuja kwa kila mtu atendaye mema, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia.
But there will be glory, honour, and peace for every one who does right — for the Jew first, but also for the Greek,
11 Kwa maana hakuna upendeleo kwa Mungu.
since God shows no partiality.
12 Kwa maana kama vile wengi waliokosa pasipo sheria watapotea pasipo sheria, na kama vile wengi waliokosa kulingana na sheria watahukumiwa kwa sheria.
All who, when they sin, are without Law will also perish without Law; while all who, when they sin, are under Law, will be judged as being under Law.
13 Maana si wasikiaji wa sheria walio wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale waitendao sheria watakaohesabiwa haki.
It is not those who hear the words of a Law that are righteous before God, but it is those who obey it that will be pronounced righteous.
14 Kwa maana watu wa Mataifa, ambao hawana sheria, wanafanya kwa asili mambo ya sheria, wao, wamekuwa sheria kwa nafsi zao, ingawa wao hawana sheria.
When Gentiles, who have no Law, do instinctively what the Law requires, they, though they have no Law, are a Law to themselves;
15 Kwa hili wanaonesha kwamba matendo yanayohitajika kwa mujibu wa sheria yameandikwa ndani ya mioyo yao. Dhamiri zao pia zinawashuhudia wao, na mawazo yao wenyewe ama huwashitaki au huwalinda wao wenyewe
for they show the demands of the Law written upon their hearts; their consciences corroborating it, while in their thoughts they argue either in self-accusation or, it may be, in self-defence —
16 na pia kwa Mungu. Haya yatatokea katika siku ambayo Mungu atazihukumu siri za watu wote, sawasawa na injili yangu, kwa njia ya Yesu Kristo.
on the day when God passes judgment on men’s inmost lives, as the Good News that I tell declares that he will do through Christ Jesus.
17 Tuseme kwamba unajiita mwenyewe Myahudi, aliyekaa katika sheria, shangilia kwa kujisifu katika Mungu,
But, perhaps, you bear the name of ‘Jew,’ and are relying upon Law, and boast of belonging to God, and understand his will,
18 yajue mapenzi yake, na kupima mambo ambayo yanatofautiana nayo, baada ya kuagizwa na sheria.
and, having been carefully instructed from the Law, have learned to appreciate the finer moral distinctions.
19 Na tuseme kwamba una ujasiri kwamba wewe mwenyewe ni kiongozi wa kipofu, mwanga kwa wale walio gizani,
Perhaps you are confident that you are a guide to the blind, a light to those who are in the dark, an instructor of the unintelligent,
20 msahihishaji wa wajinga, mwalimu wa watoto, na kwamba unayo katika sheria jinsi ya elimu na kweli.
and a teacher of the childish, because in the Law you possess the outline of all Knowledge and Truth.
21 Wewe basi, uhubiriye mwingine, je, hujifundishi mwenyewe? Wewe uhubiriye kutokuiba, je wewe huiba?
Why, then, you teacher of others, do not you teach yourself? Do you preach against stealing, and yet steal?
22 Wewe usemae usizini, je unazini? Wewe uchukiaye sanamu, je unaiba hekaluni?
Do you forbid adultery, and yet commit adultery? Do you loathe idols, and yet plunder temples?
23 Wewe ujisifuye katika sheria, je haumfedheheshi Mungu katika kuvunja sheria?
Boasting, as you do, of your Law, do you dishonour God by breaking the Law?
24 Kwa maana “jina la Mungu linafedheheshwa kati ya watu wa mataifa kwa sababu yenu,” kama ilivyoandikwa.
For, as Scripture says — ‘The name of God is reviled among the Gentiles because of you’!
25 Kwa maana Kutahiriwa kweli kwafaa kama ukitii sheria, lakini kama wewe ni mkiukaji wa sheria, kutahiriwa kwako kunakuwa kutokutahiriwa.
Circumcision has its value, if you are obeying the Law. But, if you are a breaker of the Law, your circumcision is no better than uncircumcision.
26 Basi, ikiwa, mtu asiyetahiriwa anaendelea kushika matakwa ya sheria, je kutokutahiriwa kwake hakutachukuliwa kana kwamba ametahiriwa?
If, then, an uncircumcised man pays regard to the requirements of the Law, will not he, although not circumcised, be regarded by God as if he were?
27 Na yeye asiyetahiriwa kwa asili hatakuhukumu kama akitimiza sheria? Hii ni kwa sababu una maandiko yaliyoandikwa na tohara pia lakini bado u mkiukaji wa sheria!
Indeed, the man who, owing to his birth, remains uncircumcised, and yet scrupulously obeys the Law, will condemn you, who, for all your written Law and your circumcision, are yet a breaker of the Law.
28 Kwa maana yeye si Myahudi aliye kwa hali ya nje; wala kutahiriwa si kule ambako ni kwa nje tu katika mwili.
For a man who is only a Jew outwardly is not a real Jew; nor is outward bodily circumcision real circumcision. The real Jew is the man who is a Jew in soul;
29 Lakini yeye ni Myahudi aliye kwa ndani, na tohara ni ya moyo, katika roho, si katika andiko. Sifa ya mtu wa namna hiyo haitokani na watu bali yatoka kwa Mungu.
and the real circumcision is the circumcision of the heart, a spiritual and not a literal thing. Such a man wins praise from God, though not from men.