< Warumi 2 >

1 Kwa hiyo hauna udhuru, wewe uhukumuye, kwa maana katika yale uhukumuyo mwingine wajitia hatiani mwenyewe. Kwa maana wewe uhukumuye unafanya mambo yale yale.
Now then, you there, whoever you are who judges someone else for things you practice yourself—you condemn yourself and are inexcusable.
2 Lakini twajua kwamba hukumu ya Mungu ni ya kweli juu yao wafanyao mambo kama hayo.
Further, we know that God's judgment against those who practice such things is according to truth.
3 Lakini wewe tafakari hili, wewe ambaye unahukumu wale wanaotenda mambo hayo ingawa nawe unafanya mambo yayo hayo. Je utaepuka hukumu ya Mungu?
So then, you there, you who judge those who practice such things while doing the same, do you really imagine that you will escape God's judgment?
4 Au unafikiri kidogo sana juu ya wingi wa wema wake, kuchelewa kwa adhabu yake, na uvumilivu wake? Je, hujui kwamba wema wake unapaswa kukuelekeza katika toba?
Or do you scorn the riches of His kindness, tolerance and longsuffering, not recognizing that the goodness of God is leading you toward repentance?
5 Bali kwa kadiri ya ugumu wako na kwa moyo wako usio na toba wajiwekea mwenyewe akiba ya ghadhabu kwa siku ile ya ghadhabu, yaani, siku ile ya ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu.
Rather, due to your hardness and unrepentant heart, you are treasuring up wrath for yourself in the day of God's wrath and revelation and righteous judgment,
6 Yeye atamlipa kila mtu kipimo sawa na matendo yake:
who will repay each one according to his works:
7 kwa wale ambao kwa uthabiti wa matendo mema wametafuta sifa, heshima na kutokuharibika, atawapa uzima wa milele. (aiōnios g166)
to those who seek for glory, honor and incorruption, by persevering in doing good—eternal life; (aiōnios g166)
8 Lakini kwa wale ambao ni wabinafsi, wasioitii kweli bali hutii dhuluma, ghadhabu na hasira kali itakuja.
but to those who, due to self-seeking, are actually disobeying the truth (while obeying the unrighteousness)—fury and wrath,
9 Mungu ataleta dhiki na shida juu ya kila nafsi ya binadamu aliyefanya uovu, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia.
tribulation and anguish, upon every human soul who works at the evil, whether Jew (first) or Greek;
10 Lakini sifa, heshima na amani itakuja kwa kila mtu atendaye mema, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia.
but glory, honor and peace to everyone who works the good, whether Jew (first) or Greek.
11 Kwa maana hakuna upendeleo kwa Mungu.
Now there is no favoritism with God.
12 Kwa maana kama vile wengi waliokosa pasipo sheria watapotea pasipo sheria, na kama vile wengi waliokosa kulingana na sheria watahukumiwa kwa sheria.
For as many as have sinned without law will also perish without law; while as many as have sinned with law will be judged by law.
13 Maana si wasikiaji wa sheria walio wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale waitendao sheria watakaohesabiwa haki.
For it is not the hearers of the law who are righteous before God, but the doers of the law will be justified
14 Kwa maana watu wa Mataifa, ambao hawana sheria, wanafanya kwa asili mambo ya sheria, wao, wamekuwa sheria kwa nafsi zao, ingawa wao hawana sheria.
(indeed, whenever the ethnic nations that do not have law do by nature the things of the law, these, although not having law, are a law to themselves;
15 Kwa hili wanaonesha kwamba matendo yanayohitajika kwa mujibu wa sheria yameandikwa ndani ya mioyo yao. Dhamiri zao pia zinawashuhudia wao, na mawazo yao wenyewe ama huwashitaki au huwalinda wao wenyewe
who show the work of the law written in their hearts, their conscience also bearing witness, and their reasonings among themselves accusing or even excusing)
16 na pia kwa Mungu. Haya yatatokea katika siku ambayo Mungu atazihukumu siri za watu wote, sawasawa na injili yangu, kwa njia ya Yesu Kristo.
in the day when God, according to my Gospel, will judge people's secrets by Jesus Christ.
17 Tuseme kwamba unajiita mwenyewe Myahudi, aliyekaa katika sheria, shangilia kwa kujisifu katika Mungu,
Look, you declare yourself a Jew, and rest on the Law, and boast in God,
18 yajue mapenzi yake, na kupima mambo ambayo yanatofautiana nayo, baada ya kuagizwa na sheria.
and know the Will, and approve the superior things, being instructed out of the Law.
19 Na tuseme kwamba una ujasiri kwamba wewe mwenyewe ni kiongozi wa kipofu, mwanga kwa wale walio gizani,
Further, you are confident that you yourself are a guide to the blind, a light to those in darkness,
20 msahihishaji wa wajinga, mwalimu wa watoto, na kwamba unayo katika sheria jinsi ya elimu na kweli.
an instructor of the foolish, a teacher of the immature, having in the Law the embodiment of knowledge and truth.
21 Wewe basi, uhubiriye mwingine, je, hujifundishi mwenyewe? Wewe uhubiriye kutokuiba, je wewe huiba?
You then, who teach another, do you not teach yourself? You who preach not to steal, do you steal?
22 Wewe usemae usizini, je unazini? Wewe uchukiaye sanamu, je unaiba hekaluni?
You who say not to commit adultery, do you adulterate? You who abhor idols, do you rob temples?
23 Wewe ujisifuye katika sheria, je haumfedheheshi Mungu katika kuvunja sheria?
You who boast in the Law, do you dishonor God through the transgression of the Law?
24 Kwa maana “jina la Mungu linafedheheshwa kati ya watu wa mataifa kwa sababu yenu,” kama ilivyoandikwa.
For, just as it is written: “The name of God is blasphemed among the Gentiles because of you.”
25 Kwa maana Kutahiriwa kweli kwafaa kama ukitii sheria, lakini kama wewe ni mkiukaji wa sheria, kutahiriwa kwako kunakuwa kutokutahiriwa.
Now circumcision does have value if you keep the Law, but if you are a transgressor of the Law, your circumcision has become uncircumcision.
26 Basi, ikiwa, mtu asiyetahiriwa anaendelea kushika matakwa ya sheria, je kutokutahiriwa kwake hakutachukuliwa kana kwamba ametahiriwa?
So if the uncircumcised keeps the righteous requirements of the Law, will not his uncircumcision be counted as circumcision?
27 Na yeye asiyetahiriwa kwa asili hatakuhukumu kama akitimiza sheria? Hii ni kwa sababu una maandiko yaliyoandikwa na tohara pia lakini bado u mkiukaji wa sheria!
And will not the physically uncircumcised who fulfills the law judge you, complete with written code and circumcision, who are a transgressor of the Law?
28 Kwa maana yeye si Myahudi aliye kwa hali ya nje; wala kutahiriwa si kule ambako ni kwa nje tu katika mwili.
Because a person is not a [true] Jew who is only one outwardly, nor is [true] circumcision something outward in the flesh;
29 Lakini yeye ni Myahudi aliye kwa ndani, na tohara ni ya moyo, katika roho, si katika andiko. Sifa ya mtu wa namna hiyo haitokani na watu bali yatoka kwa Mungu.
but he is a Jew who is one inwardly, and circumcision is of the heart—in spirit, not letter—whose praise is not from men but from God.

< Warumi 2 >