< Warumi 15 >
1 Sasa sisi tulio na nguvu tunapaswa kuuchukua udhaifu wa walio dhaifu, na hatupaswi kujipendeza wenyewe.
A tak powinniśmy znosić, my, którzyśmy mocni, mdłości słabych, a nie podobać się samym sobie.
2 Kila mmoja wetu ampendeze jirani yake kwani ni jambo jema, kwa lengo la kumjenga.
Przetoż każdy z nas niech się bliźniemu podoba ku dobremu dla zbudowania;
3 Kwani hata Kristo hakujipendeza mwenyewe. Badala yake, ilikuwa kama ilivyoandikwa, “Matusi ya wale waliokutukana yamenipata mimi.”
Ponieważ i Chrystus nie podobał się samemu sobie, ale jako napisano: Urągania urągających tobie przypadły na mię.
4 Kwa chochote kilichotangulia kuandikwa, kiliandikwa kwa kutuelekeza, kwa kusudi kwamba kupitia uvumilivu na kupitia kutiwa moyo na maandiko tungekuwa na ujasiri.
Bo cokolwiek przedtem napisano, ku naszej nauce napisano, abyśmy przez cierpliwość i przez pociechę Pism nadzieję mieli.
5 Sasa Mungu wa uvumilivu na wa kutia moyo awape kuwa na nia sawa kwa kila mmoja kulingana na Yesu Kristo.
A Bóg cierpliwości i pociechy niech wam da, abyście byli jednomyślni między sobą według Chrystusa Jezusa.
6 Aweze kufanya hivi kwa nia moja muweze kumsifu kwa kinywa kimoja Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo.
Abyście jednomyślnie jednemi usty wysławiali Boga, Ojca Pana naszego Jezusa Chrystusa.
7 Kwa hiyo mpokeeni kila mmoja, kama vile Kristo alivyowapokea, kwa utukufu wa Mungu.
Przetoż przyjmujcie jedni drugich, jako i Chrystus przyjął nas do chwały Bożej.
8 Kwani nasema kwamba Kristo amefanywa mtumishi wa tohara kwa niaba ya ukweli wa Mungu. Alifanya hivi ili kwamba aweze kuthibitisha ahadi zilizotolewa kwa mababa,
Bo powiadam, iż Jezus Chrystus był sługą obrzezki dla prawdy Bożej, aby potwierdził obietnice ojcom uczynione,
9 na kwa mataifa kumtukuza Mungu kwa neema yake. Kama ambavyo imeandikwa, “Kwa hiyo nitatoa sifa kwako miongoni mwa mataifa na kuimba sifa katika jina lako.”
A poganie żeby za miłosierdzie chwalili Boga, jako napisano: Dlatego będę cię wysławiał między pogany i imieniowi twemu śpiewać będę.
10 Tena inasema, “Furahini, ninyi watu wa mataifa, pamoja na watu wake.”
I zasię mówi: Weselcie się poganie z ludem jego.
11 Na tena, “Msifuni Bwana, ninyi mataifa yote; acha watu wa mataifa yote wamsifu yeye.”
I zasię: Chwalcie Pana wszyscy poganie, a wysławiajcie go wszyscy ludzie.
12 Tena Isaya asema, “Kutakuwa na shina la Yese, na mmoja atakayeinuka kutawala juu ya mataifa. Mataifa watakuwa na tumaini katika yeye.”
I zasię Izajasz mówi: Będzie korzeń Jessego, a który powstanie, aby panował nad pogany, w nim poganie nadzieję pokładać będą.
13 Sasa Mungu wa tumaini awajaze na furaha yote na amani kwa kuamini, ili kwamba muweze kuzidi katika tumaini, kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.
A Bóg nadziei niech was napełni wszelką radością i pokojem w wierze, abyście obfitowali w nadziei przez moc Ducha Świętego.
14 Mimi mwenyewe pia nimeshawishiwa nanyi, ndugu zangu. Nimeshawishiwa kwamba pia ninyi wenyewe mmejazwa na wema, mmejazwa na maarifa yote. Ninashawishiwa kwamba, ninyi mwaweza pia kuhimizana kila mmoja na mwenzake.
A pewienem, bracia moi! i ja sam o was, że jesteście i wy sami pełni dobroci, napełnieni wszelką znajomością, i możecie jedni drugich napominać.
15 Lakini ninaandika kwa ujasiri zaidi kwenu juu ya mambo fulani ili kuwakumbusha tena, sababu ya kipawa nilichopewa na Mungu.
A pisałem do was, bracia! poniekąd śmielej, jakoby was napominając przez łaskę, która mi jest dana od Boga.
16 Kipawa hiki kilikuwa kwamba niweze kuwa mtumishi wa Yesu Kristo aliyetumwa kwa mataifa, kujitoa kama kuhani wa injili ya Mungu. Ningeweza kufanya hivi ili kujitoa kwangu kwa mataifa kuwe kumekubaliwa, kumetengwa na Mungu kwa njia ya Roho Mtakatifu.
Na to, abym był sługą Jezusa Chrystusa między pogany, świętobliwie pracując w Ewangielii Bożej, aby ofiara pogan stała się przyjemna, poświęcona przez Ducha Świętego.
17 Hivyo furaha yangu iko katika Kristo Yesu na katika mambo ya Mungu.
Mam się tedy czem chlubić w Chrystusie Jezusie, w rzeczach Bożych.
18 Kwani sitaweza kuthubutu kunena lolote isipokuwa kwamba Kristo amekamilisha kupitia kwangu utii wa mataifa. Haya mambo yametimizwa kwa neno na tendo,
Albowiem nie śmiałbym mówić tego, czego by nie sprawował Chrystus przez mię w przywodzeniu ku posłuszeństwu pogan, przez słowo i przez uczynek,
19 kwa nguvu za ishara na maajabu, na kwa nguvu za Roho Mtakatifu. Hii ilikuwa ili kwamba kutoka Yerusalem, na kuzungukia mbali kama Iliriko, niweze kuichukua nje kwa ukamilifu injili ya Kristo.
Przez moc znamion i cudów, przez moc Ducha Bożego, tak iżem od Jeruzalemu i okolicznych krain aż do Iliryku napełnił Ewangieliją Chrystusową;
20 Kwa njia hii, nia yangu imekuwa kuitangaza injili, lakini si mahali Kristo anajulikana kwa jina, ili kwamba nisiweze kujenga juu ya msingi wa mtu mwingine.
A to tak usiłując kazać Ewangieliję, gdzie i mianowany nie był Chrystus, abym na cudzym fundamencie nie budował.
21 Kama ilivyoandikwa: “Ambao kwa yeye hawana habari zake alikuja watamwona, na wale ambao hawakumsikia watamfahamu.”
Ale jako napisano: Którym nie powiadano o nim, oglądają; a którzy o nim nie słyszeli, zrozumieją.
22 Kwahiyo nilikuwa pia nimezuiliwa mara nyingi kuja kwenu.
Dlaczegom też często miewał przeszkody, żem do was przyjść nie mógł.
23 Lakini sasa, sina tena sehemu yoyote katika mikoa hii, na nimekuwa nikitamani kwa miaka mingi kuja kwenu.
Lecz teraz nie mam więcej miejsca w tych samych krainach, a mając chęć przyjść do was od wielu lat.
24 Hivyo mara zote nikienda Hispania, ninatumaini kuwaona nikipita, na kuweza kupelekwa njia yangu na ninyi, baada ya kuwa nimefurahia ushirika na ninyi kwa muda.
Kiedykolwiek pójdę do Hiszpanii, przyjdę do was: bo się spodziewam, że tamtędy idąc ujrzę was, a że wy mię tam poprowadzicie, kiedy się pierwej z wami troszeczkę ucieszę.
25 Lakini sasa ninakwenda Yerusalemu kuwahudumia waumini.
A teraz idę do Jeruzalemu, usługując świętym.
26 Maana iliwapendeza watu wa Makedonia na Akaya kufanya changizo maalumu kwa masikini miongoni mwa waumini huko Yerusalemu.
Albowiem się upodobało Macedonii i Achai, nieco spólnie złożyć na ubogich świętych, którzy są w Jeruzalemie.
27 Ndiyo, ilikuwa kwa upendo wao, na hakika, wamekuwa wadeni wao. Maana ikiwa mataifa wameshiriki katika mambo yao ya kiroho, wanadaiwa na wao pia kuwahudumia katika mahitaji ya vitu.
Owa podobało się im i są ich dłużnikami; bo ponieważ dóbr ich duchownych poganie się uczestnikami stali, powinni im też są cielesnemi usługiwać.
28 Kwahiyo, wakati nimekamilisha hivi na kuwa na utoshelevu wa tunda hili kwao, mimi nitakwenda njiani pamoja nanyi huko Hispania.
Przetoż gdy to wykonam, a onym jako zapieczętowany ten pożytek oddam, pójdę przez was do Hiszpanii;
29 Najua kwamba, wakati nikija kwenu, nitakuja katika utimilifu wa baraka za Kristo.
A wiem, iż gdy przyjdę do was, z hojnem błogosławieństwem Ewangielii Chrystusowej przyjdę.
30 Sasa ninawasihi, ndugu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo, na kwa upendo wa Roho, kwamba mshiriki pamoja nami katika maombi yenu kwa Mungu kwa ajili yangu.
A proszę was, bracia! przez Pana naszego Jezusa Chrystusa i przez miłość Ducha, abyście wespół ze mną pracowali w modlitwach za mię do Boga,
31 Ombeni kwamba niweze kuokolewa kutoka kwao wasio na utii katika Yudea, na kwamba huduma yangu huko Yerusalemu iweze kupokelewa na waumini.
Abym był wybawiony od tych, którzy są niewiernymi w ziemi Judzkiej, a iżby usługa moja, którą wykonywam przeciw Jeruzalemowi, przyjemna była świętym;
32 Ombeni kwamba ninaweza kuja kwenu kwa furaha kupitia mapenzi ya Mungu, na kwamba niweze kuwa pamoja nanyi, kupata kupumzika.
Abym z radością przyszedł do was za wolą Bożą i z wami się wespół ucieszył.
33 Na Mungu wa amani awe pamoja nanyi nyote. Amina
A Bóg pokoju niech będzie z wami wszystkimi. Amen.