< Warumi 14 >
1 Mpokeeni yeyote ambaye ni dhaifu katika imani, bila kutoa hukumu kuhusu mawazo yake.
But receive to yourselves him who is weak in faith, not into disputations of doubtful matters.
2 Mtu mmoja ana imani ya kula chochote, mwingine ambaye ni dhaifu anakula mboga tu.
One indeed believes he is to eat all things: another who is weak, vegetables.
3 Mtu ambaye anakula kila kitu asimdharau yeye asiyekula kila kitu. Na yeye ambaye hali kila kitu asimuhukumu mwingine ambaye hula kila kitu. Kwa kuwa Mungu amekwisha mpokea.
Let not the one eating snub the one not eating. Let not the one not eating judge the one eating; for God received him.
4 Wewe ni nani, wewe ambaye unamuhukumu mtumishi ambaye ni miliki ya mtu mwingine? Ni mbele ya Bwana wake kwamba husimama au huanguka. Lakini atainuliwa, kwa kuwa Bwana anaweza kumfanya asimame.
Who art thou judging another man's servant? to his own master he stands or falls: but he shall stand; for God is able to make him stand.
5 Mtu mmoja huthamini siku moja kuliko nyingine. Mwingine huthamini kila siku sawa sawa. Hebu kila mtu na ashawishike katika akili yake mwenyewe.
For one indeed judges a day above a day: another judges every day (alike); let each one be fully persuaded in his own mind.
6 Yeye ambaye anashika siku, anashika kwa ajili ya Bwana. Na kwa yeye alaye, hula kwa ajili ya Bwana, kwa kuwa anampa Mungu shukrani. Yeye ambaye hali, hujizuia kutokula kwa ajili ya Bwana. Yeye pia hutoa shukrani kwa Mungu.
The one regarding the day, regards it to the Lord: the one eating, eats to the Lord, for he gives thanks to God; and the one not eating, eats not to the Lord, and gives thanks to God.
7 Kwa kuwa hakuna aishie kwa nafsi yake, na hakuna afae kwa ajili yake mwenyewe.
For no one of us lives to himself, and no one dies to himself:
8 Kwa kuwa ikiwa tunaishi, tunaishi kwa ajili ya Bwana. Na ikiwa tunakufa, tunakufa kwa ajili ya Bwana. Basi ikiwa tunaishi au tunakufa tu mali ya Bwana.
for if indeed we live, we live to the Lord; and if we die, we die to the Lord. Then indeed if we live, and if we die, we are the Lord's.
9 Kwa kuwa ni kwa kusudi hili Kristo alikufa na kuishi tena, kwamba awe Bwana wa wote wafu na waishio.
For unto this Christ died, and lives, in order that He may be Lord of the dead and of the living.
10 Lakini wewe, kwa nini unamuhukumu ndugu yako? Na wewe, kwa nini unamdharau ndugu yako? Kwa kuwa sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu.
But why do you judge your neighbor, or indeed why do you discount your brother? for we shall all stand before the judgment-seat of God.
11 Kwa kuwa imeandikwa, “Kama niishivyo,” asema Bwana, “Kwangu mimi kila goti litapigwa, na kila ulimi utatoa sifa kwa Mungu.”
For it has been written; As I live, says the Lord, every knee shall bow to me, and every tongue shall confess to God.
12 Hivyo basi, kila mmoja wetu atatoa hesabu yake mwenyewe kwa Mungu.
Then therefore each one of us shall give an account to God for himself.
13 Kwa hiyo, tusiendelee tena kuhukumiana, lakini badala yake amua hivi, kwamba hakuna atakaye weka kikwazo au mtego kwa ndugu yake.
Then let us no longer judge one another: but rather judge this, not to place before a brother an offence for a stumblingblock.
14 Ninajua na nimeshawishika katika Bwana Yesu, kwamba hakuna kitu kilicho najisi chenyewe. Ni kwa yeye tu anayedhani kuwa chochote ni najisi, kwa kuwa kwake ni najisi.
I know, and am persuaded in the Lord Jesus, that there is nothing unclean of itself: except to him who considers it unclean, to him it is unclean.
15 Ikiwa kwa sababu ya chakula ndugu yako anahuzunika, hautembei tena katika upendo. Usimharibu kwa chakula chako mtu ambaye kwa ajili yake Kristo alikufa.
But if your brother is grieved on account of your meat, you are no longer walking in divine love. Do not by your meat destroy him for whom Christ died.
16 Hivyo msiruhusu matendo yenu mema yakasababisha watu kuwadhihaki.
Let not your good be blasphemed.
17 Kwa kuwa ufalme wa Mungu si kwa ajili ya chakula na kinywaji, bali ni kwa ajili ya haki, amani, na furaha katika Roho Mtakatifu.
For the kingdom of God is not meat and drink, but righteousness and peace and joy in the Holy Ghost.
18 Kwa kuwa yeye amtumikiaye Kristo kwa jinsi hii amekubalika kwa Mungu na amekubalika kwa watu.
For in this the one serving Christ is acceptable to God, and approved unto men.
19 Kwa hiyo basi, na tufuate mambo ya amani na mambo ambayo humjenga mtu na mwingine.
Then therefore we pursue the things belonging to peace, and edification towards one another.
20 Usiharibu kazi ya Mungu kwa sababu ya chakula. Vitu vyote kwa kweli ni safi, lakini ni vibaya kwa mtu yule ambaye hula na kumsababisha yeye kujikwaa.
Do not destroy the work of God on account of meat. All things are pure; but it is evil to the man who eats with offence:
21 Ni vyema kutokula nyama, wala kunywa divai, wala chochote ambacho kwa hicho ndugu yako hukwazwa.
it is good neither to eat flesh, nor to drink wine, nor anything by which your brother stumbles.
22 Hizi imani maalumu ulizo nazo, ziweke kati yako mwenyewe na Mungu. Amebalikiwa yule ambaye hajihukumu mwenyewe katika kile anachokikubali.
The faith which you have, have it with yourself before God. Happy is the one not judging himself in that which he approves:
23 Aliye na mashaka amehukumiwa ikiwa anakula, kwa sababu haitokani na imani. Na chochote kisichotokana na imani ni dhambi.
but if he may eat doubting, he has been condemned, because it is not of faith; but every thing which is not of faith is sin.