< Warumi 12 >

1 Kwa hiyo nawasihi, ndugu, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, inayokubalika kwa Mungu. Hii ndiyo ibada yenu yenye maana.
hE bhrAtara Izvarasya kRpayAhaM yuSmAn vinayE yUyaM svaM svaM zarIraM sajIvaM pavitraM grAhyaM balim Izvaramuddizya samutsRjata, ESA sEvA yuSmAkaM yOgyA|
2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu. Fanyeni hivi mpate kujua mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yakumpendeza na kamilifu. (aiōn g165)
aparaM yUyaM sAMsArikA iva mAcarata, kintu svaM svaM svabhAvaM parAvartya nUtanAcAriNO bhavata, tata Izvarasya nidEzaH kIdRg uttamO grahaNIyaH sampUrNazcEti yuSmAbhiranubhAviSyatE| (aiōn g165)
3 Kwa maana nasema, kwa sababu ya neema niliyopewa, kwamba kila mtu ambaye yupo miongoni mwenu hapaswi kufikiri zaidi juu yake mwenyewe kuliko inavyompasa kufikiri. Bali, imempasa kufikiri kwa hekima, kama ambavyo Mungu amewapa kila mmoja kiasi fulani cha imani.
kazcidapi janO yOgyatvAdadhikaM svaM na manyatAM kintu IzvarO yasmai pratyayasya yatparimANam adadAt sa tadanusAratO yOgyarUpaM svaM manutAm, IzvarAd anugrahaM prAptaH san yuSmAkam EkaikaM janam ityAjnjApayAmi|
4 Kwa kuwa tuna viungo vingi katika mwili mmoja, lakini si viungo vyote vina kazi moja.
yatO yadvadasmAkam Ekasmin zarIrE bahUnyaggAni santi kintu sarvvESAmaggAnAM kAryyaM samAnaM nahi;
5 Vivyo hivyo, sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo kila mmoja kwa mwenzake.
tadvadasmAkaM bahutvE'pi sarvvE vayaM khrISTE EkazarIrAH parasparam aggapratyaggatvEna bhavAmaH|
6 Tuna karama zilizo mbalimbali kwa kadiri ya neema mliyopewa. Ikiwa karama ya mtu ni unabii, na itendeke kwa kadiri ya imani yake.
asmAd IzvarAnugrahENa vizESaM vizESaM dAnam asmAsu prAptESu satsu kOpi yadi bhaviSyadvAkyaM vadati tarhi pratyayasya parimANAnusArataH sa tad vadatu;
7 Ikiwa karama ya mtu ni huduma, na atumike. Ikiwa mwingine ana karama ya kufundisha, basi, afundishe.
yadvA yadi kazcit sEvanakArI bhavati tarhi sa tatsEvanaM karOtu; athavA yadi kazcid adhyApayitA bhavati tarhi sO'dhyApayatu;
8 Ikiwa karama ya mtu ni faraja, basi, afariji. Ikiwa karama ya mtu ni kutoa, afanye hivyo kwa ukarimu. Ikiwa karama ya mtu ni kuongoza, na litendeke kwa uangalifu. Ikiwa karama ya mtu ni katika kuonesha huruma, na litendeke kwa furaha.
tathA ya upadESTA bhavati sa upadizatu yazca dAtA sa saralatayA dadAtu yastvadhipatiH sa yatnEnAdhipatitvaM karOtu yazca dayAluH sa hRSTamanasA dayatAm|
9 Pendo lisiwe na unafiki. Chukieni uovu; mshikilie yaliyo mema.
aparanjca yuSmAkaM prEma kApaTyavarjitaM bhavatu yad abhadraM tad RtIyadhvaM yacca bhadraM tasmin anurajyadhvam|
10 Kuhusu upendo wa ndugu, pendaneni ninyi kwa ninyi. Kuhusu heshima, heshimianeni ninyi kwa ninyi.
aparaM bhrAtRtvaprEmnA parasparaM prIyadhvaM samAdarAd EkO'parajanaM zrESThaM jAnIdhvam|
11 Kuhusu bidii, msiwe walegevu. Kuhusu roho, iweni na shauku. Kuhusu Bwana, mtumikieni.
tathA kAryyE nirAlasyA manasi ca sOdyOgAH santaH prabhuM sEvadhvam|
12 Furahini katika ujasiri mlionao kuhusu siku zijazo. Muwe na subira katika matatizo yenu. Mdumu katika kuomba.
aparaM pratyAzAyAm AnanditA duHkhasamayE ca dhairyyayuktA bhavata; prArthanAyAM satataM pravarttadhvaM|
13 Mshiriki katika mahitaji ya waumini. Tafuteni njia nyingi za kuonesha ukarimu.
pavitrANAM dInatAM dUrIkurudhvam atithisEvAyAm anurajyadhvam|
14 Watakieni baraka wote wanaowatesa ninyi; muwabariki na wala msiwalaani.
yE janA yuSmAn tAPayanti tAn AziSaM vadata zApam adattvA daddhvamAziSam|
15 Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
yE janA Anandanti taiH sArddham Anandata yE ca rudanti taiH saha rudita|
16 Muwe na nia moja ninyi kwa ninyi. Msifikiri kwa kujivuna, lakini wakubalini watu wa hali ya chini. Msiwe na hekima juu ya mawazo yenu wenyewe.
aparanjca yuSmAkaM manasAM parasparam EkObhAvO bhavatu; aparam uccapadam anAkAgkSya nIcalOkaiH sahApi mArdavam Acarata; svAn jnjAninO na manyadhvaM|
17 Msimlipe mtu yeyote ovu kwa ovu. Fanyeni mambo mema machoni pa watu wote.
parasmAd apakAraM prApyApi paraM nApakuruta| sarvvESAM dRSTitO yat karmmOttamaM tadEva kuruta|
18 Kama inawezekana, kama ilivyowekwa kwenu, muwe na amani na watu wote.
yadi bhavituM zakyatE tarhi yathAzakti sarvvalOkaiH saha nirvvirOdhEna kAlaM yApayata|
19 Wapenzi, msijilipizie kisasi wenyewe, lakini ipisheni ghadhabu ya Mungu. Kwa maana imeandikwa, '' 'kisasi ni changu; Mimi nitalipa,' asema Bwana.”
hE priyabandhavaH, kasmaicid apakArasya samucitaM daNPaM svayaM na daddhvaM, kintvIzvarIyakrOdhAya sthAnaM datta yatO likhitamAstE paramEzvaraH kathayati, dAnaM phalasya matkarmma sUcitaM pradadAmyahaM|
20 “Lakini ikiwa adui yako ana njaa, mlishe. Akiwa na kiu, mnyweshe. Kwa maana ukifanya hivyo, utampalia makaa ya moto juu ya kichwa chake.”
itikAraNAd ripu ryadi kSudhArttastE tarhi taM tvaM prabhOjaya| tathA yadi tRSArttaH syAt tarhi taM paripAyaya| tEna tvaM mastakE tasya jvaladagniM nidhAsyasi|
21 Usishindwe na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.
kukriyayA parAjitA na santa uttamakriyayA kukriyAM parAjayata|

< Warumi 12 >