< Warumi 12 >

1 Kwa hiyo nawasihi, ndugu, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, inayokubalika kwa Mungu. Hii ndiyo ibada yenu yenye maana.
I beseech you, therefore, brethren, by the mercies of God, that you present your bodies a living sacrifice, holy, acceptable to God, which is your reasonable service.
2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu. Fanyeni hivi mpate kujua mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yakumpendeza na kamilifu. (aiōn g165)
And be not conformed to this age, but be transformed by the renewing of your mind, that you may learn what the will of God is―the good, and the acceptable, and the perfect. (aiōn g165)
3 Kwa maana nasema, kwa sababu ya neema niliyopewa, kwamba kila mtu ambaye yupo miongoni mwenu hapaswi kufikiri zaidi juu yake mwenyewe kuliko inavyompasa kufikiri. Bali, imempasa kufikiri kwa hekima, kama ambavyo Mungu amewapa kila mmoja kiasi fulani cha imani.
For I say, through the grace given to me, to every one that is among you, that he must not think of himself more highly than he ought to think; but that he be disposed to think modestly, as God has distributed to each a measure of faith.
4 Kwa kuwa tuna viungo vingi katika mwili mmoja, lakini si viungo vyote vina kazi moja.
For as we have many members in one body, and all the members have not the same office,
5 Vivyo hivyo, sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo kila mmoja kwa mwenzake.
so we, the many, are one body in Christ, and members one of another.
6 Tuna karama zilizo mbalimbali kwa kadiri ya neema mliyopewa. Ikiwa karama ya mtu ni unabii, na itendeke kwa kadiri ya imani yake.
Since, then, we have gifts which differ according to the grace that is given to us, whether we have the gift of prophecy, let us prophesy according to the proportion of our faith;
7 Ikiwa karama ya mtu ni huduma, na atumike. Ikiwa mwingine ana karama ya kufundisha, basi, afundishe.
or, if we have a ministry, let us be active in our ministry; if any one teaches, let him attend to his teaching;
8 Ikiwa karama ya mtu ni faraja, basi, afariji. Ikiwa karama ya mtu ni kutoa, afanye hivyo kwa ukarimu. Ikiwa karama ya mtu ni kuongoza, na litendeke kwa uangalifu. Ikiwa karama ya mtu ni katika kuonesha huruma, na litendeke kwa furaha.
or, if any exhorts, let him attend to exhortation; if any one gives, let him do it with sincerity; he that rules, with diligence: he that shows mercy, with cheerfulness.
9 Pendo lisiwe na unafiki. Chukieni uovu; mshikilie yaliyo mema.
Let love be without hypocrisy. Abhor that which is evil; cleave to that which is good;
10 Kuhusu upendo wa ndugu, pendaneni ninyi kwa ninyi. Kuhusu heshima, heshimianeni ninyi kwa ninyi.
in love to the brotherhood, be kindly affectionate one to another; in showing honor, be examples one to another;
11 Kuhusu bidii, msiwe walegevu. Kuhusu roho, iweni na shauku. Kuhusu Bwana, mtumikieni.
in what requires diligence, be not slothful; in spirit, be fervent; in service, be devoted to the Lord;
12 Furahini katika ujasiri mlionao kuhusu siku zijazo. Muwe na subira katika matatizo yenu. Mdumu katika kuomba.
in hope, be joyful; in affliction, be patient; in prayer, be persevering;
13 Mshiriki katika mahitaji ya waumini. Tafuteni njia nyingi za kuonesha ukarimu.
administer to the necessities of the saints; be careful to entertain strangers;
14 Watakieni baraka wote wanaowatesa ninyi; muwabariki na wala msiwalaani.
bless them that persecute you; bless, and curse not;
15 Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
rejoice with them that rejoice, and weep with them that weep;
16 Muwe na nia moja ninyi kwa ninyi. Msifikiri kwa kujivuna, lakini wakubalini watu wa hali ya chini. Msiwe na hekima juu ya mawazo yenu wenyewe.
cultivate the same disposition, one toward another: mind not high things, but conform yourselves to things that are lowly. Be not wise in your own conceits;
17 Msimlipe mtu yeyote ovu kwa ovu. Fanyeni mambo mema machoni pa watu wote.
repay to no one evil for evil; practice that which is honorable in the sight of all men.
18 Kama inawezekana, kama ilivyowekwa kwenu, muwe na amani na watu wote.
If possible, as far as may be in your power, be at peace with all men.
19 Wapenzi, msijilipizie kisasi wenyewe, lakini ipisheni ghadhabu ya Mungu. Kwa maana imeandikwa, '' 'kisasi ni changu; Mimi nitalipa,' asema Bwana.”
Beloved, avenge not yourselves, but give place to the wrath of God; for it is written: Vengeance is mine, I will repay, says the Lord.
20 “Lakini ikiwa adui yako ana njaa, mlishe. Akiwa na kiu, mnyweshe. Kwa maana ukifanya hivyo, utampalia makaa ya moto juu ya kichwa chake.”
If, therefore, your enemy is hungry, feed him; if he is thirsty, give him drink; for by doing this, you will heap coals of fire on his head.
21 Usishindwe na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.
Be not overcome by evil; but overcome evil with good.

< Warumi 12 >