< Warumi 10 >
1 Ndugu, nia ya moyo wangu na ombi langu kwa Mungu ni kwa ajili yao, kwa ajili ya wokovu wao.
Braæo! želja je mojega srca i molitva k Bogu za spasenije Izrailja.
2 Kwa kuwa nawashuhudia kwamba wanajuhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si kwa ajili ya ufahamu.
Jer im svjedoèim da imaju revnost za Boga, ali ne po razumu.
3 Kwa kuwa hawajui haki ya Mungu, na wanatafuta kujenga haki yao wenyewe. Hawakuwa watiifu kwa haki ya Mungu.
Jer ne poznajuæi pravde Božije i gledajuæi da svoju pravdu utvrde ne pokoravaju se pravdi Božijoj.
4 Kwa kuwa Kristo ndiye utimilifu wa sheria kwa ajili ya haki ya kila mtu aaminiye.
Jer je Hristos svršetak zakona: koji ga god vjeruje opravdan je.
5 Kwa kuwa Musa anaandika kuhusu haki ambayo huja kutokana na sheria: “Mtu ambaye hutenda haki ya sheria ataishi kwa haki hii.”
Jer Mojsije piše za pravdu koja je od zakona: koji èovjek to èini življeæe u tom.
6 Lakini haki ambayo inatokana na imani husema hivi, “Usiseme moyoni mwako, 'Nani atapaa kwenda mbinguni?' (Hii ni kumleta Kristo chini).
A pravda koja je od vjere ovako govori: da ne reèeš u srcu svojemu: ko æe iziæi na nebo? to jest da svede Hrista;
7 Na usiseme, 'Nani atashuka katika shimo?”' (Hii ni, kumleta Kristo juu kutoka kwa wafu). (Abyssos )
Ili: ko æe siæi u bezdan? to jest da izvede Hrista iz mrtvijeh. (Abyssos )
8 Lakini inasema nini? “Neno liko karibu na wewe, katika kinywa chako na katika moyo wako.” Hilo ni neno la imani, ambalo tunatangaza.
Ali šta govori pismo? Blizu ti je rijeè u ustima tvojima i u srcu tvojemu, to jest rijeè vjere koju propovijedamo.
9 Kwa kuwa kama kwa kinywa chako unamkiri Yesu ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokoka.
Jer ako priznaješ ustima svojima da je Isus Gospod, i vjeruješ u srcu svojemu da ga Bog podiže iz mrtvijeh, biæeš spasen.
10 Kwa kuwa kwa moyo mtu huamini na kupata haki, na kwa kinywa hukiri na kupata wokovu.
Jer se srcem vjeruje za pravdu a ustima se priznaje za spasenije.
11 Kwa kuwa andiko lasema, “Kila amwaminiye hata aibika.”
Jer pismo govori: koji ga god vjeruje neæe se postidjeti.
12 kwa kuwa hakuna tofauti kati ya Myahudi na Myunani. Kwa kuwa Bwana yule yule ni Bwana wa wote, na ni tajiri kwa wote wamwitao.
Jer nema razlike meðu Jevrejinom i Grkom: jer je on Bog sviju, i bogat za sve koji ga prizivlju.
13 Kwa kuwa kila mtu ambaye huliitia jina la Bwana ataokoka.
Jer koji god prizove ime Gospodnje spašæe se.
14 Kwa jinsi gani wanaweza kumwita yeye ambaye hawajamwamini? Na jinsi gani wanaweza kuamini katika yeye ambaye hawajamsikia? Na watasikiaje pasipo muhubiri?
Kako æe dakle prizvati koga ne vjerovaše? A kako æe vjerovati koga ne èuše? A kako æe èuti bez propovjednika?
15 Na jinsi gani wanaweza kuhubiri, isipokuwa wametumwa? - Kama ilivyoandikwa, “Jinsi gani ni mizuri miguu ya wale ambao wanatangaza habari za furaha za mambo mema!”
A kako æe propovijedati ako ne budu poslani? Kao što stoji napisano: kako su krasne noge onijeh koji donose glas za mir, koji donose glas za dobro!
16 Lakini wote hawakusikiliza injili. Kwa kuwa Isaya hunena, “Bwana, ni nani aliyesikia ujumbe wetu?”
Ali svi ne poslušaše jevanðelja: jer Isaija govori: Gospode! ko vjerova našemu propovijedanju?
17 Hivyo imani huja kutokana na kusikia, na kusikia kwa neno la Kristo.
Tako dakle vjera biva od propovijedanja, a propovijedanje rijeèju Božijom.
18 Lakini nasema, “Je hawakusikia?” Ndiyo, kwa hakika sana. “Sauti yao imekwisha toka nje katika nchi yote, na maneno yao kwenda miisho ya dunia.”
Nego velim: zar ne èuše? Još otide po svoj zemlji glas njihov, i po krajevima vasionoga svijeta rijeèi njihove.
19 Zaidi ya yote, Ninasema, “Je Israel hakujua?” Kwanza Musa hunena, “Nitawachokoza kuwatia wivu kwa watu ambao si taifa. Kwa njia ya taifa lisilo na uelewa, nitawachochea hadi mkasirike.”
Nego velim: zar ne razumje Izrailj? Prvi Mojsije govori: ja æu vas razdražiti, ne svojijem narodom, nerazumnijem narodom rasrdiæu vas.
20 Na Isaya ni jasiri sana na husema, “Nilipatikana na wale ambao hawakunitafuta. Nilionekana kwa wale ambao hawakunihitaji.”
A Isaija govori slobodno: naðoše me koji me ne traže; i javih se onima koji za me ne pitaju.
21 Lakini kwa Israel husema, “Siku zote nilinyoosha mikono yangu kwa wasiotii na kwa watu wagumu.”
A k Izrailju govori: vas dan pružah ruke svoje k narodu koji ne da da mu se kaže i odgovara nasuprot.