< Ufunuo 1 >

1 Huu ni ufunuo wa Yesu Kristo ambao Mungu alimpa ili kuwaonesha watumishi wake mambo ambayo lazima yatokee karibuni. Aliyafanya yajulikane kwa kumtuma malaika wake kwa mtumishi wake Yohana.
The revelation given by Jesus Christ, which God granted Him, that He might make known to His servants certain events which must shortly come to pass: and He sent His angel and communicated it to His servant John.
2 Yohana alitoa ushuhuda wa kila kitu alichoona kuhusiana na neno la Mungu na kwa ushuhuda uliotolewa kuhusu Yesu Kristo.
This is the John who taught the truth concerning the Word of God and the truth told us by Jesus Christ-- a faithful account of what he had seen.
3 Amebarikiwa yeye asomaye kwa sauti na wale wote wanaoyasikia maneno ya unabii huu na kutii kilichoandikwa humo, kwa sababu muda umekaribia.
Blessed is he who reads and blessed are those who listen to the words of this prophecy and lay to heart what is written in it; for the time for its fulfillment is now close at hand.
4 Yohana, kwa makanisa saba yaliyoko Asia: neema iwe kwenu na amani kutoka kwake aliyepo, aliyekuwepo, na atakayekuja, na kutoka kwa roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi,
John sends greetings to the seven Churches in the province of Asia. May grace be granted to you, and peace, from Him who is and was and evermore will be; and from the seven Spirits which are before His throne;
5 na kutoka kwa Yesu Kristo ambaye ni shahidi mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mtawala wa wafalme wa dunia hii. Kwake yeye atupendaye na ametuweka huru kutoka katika dhambi zetu kwa damu yake,
and from Jesus Christ, the truthful witness, the first of the dead to be born to Life, and the Ruler of the kings of the earth. To Him who loves us and has freed us from our sins with His own blood,
6 ametufanya kuwa ufalme, makuhani wa Mungu na Baba yake - kwake kuwa utukufu na nguvu milele daima. Amina. (aiōn g165)
and has formed us into a Kingdom, to be priests to God, His Father--to Him be ascribed the glory and the power until the Ages of the Ages. Amen. (aiōn g165)
7 Tazama, anakuja na mawingu; kila jicho litamwona, pamoja na wote waliomchoma. Na kabila zote za dunia wataomboleza kwake. Ndiyo, Amina.
He is coming in the clouds, and every eye will see Him, and so will those who pierced Him; and all the nations of the earth will gaze on Him and mourn. Even so. Amen.
8 “Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu, “Yeye aliyepo, na aliyekuwepo, na ambaye anakuja, Mwenye nguvu.”
"I am the Alpha and the Omega," says the Lord God, "He who is and was and evermore will be--the Ruler of all."
9 Mimi, Yohana - ndugu yenu na mmoja anayeshiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na uvumilivu thabiti ulio katika Yesu; nilikuwa katika kisiwa kiitwacho Patimo kwa sababu ya neno la Mungu na ushuhuda kuhusu Yesu.
I John, your brother, and a sharer with you in the sorrows and Kingship and patient endurance of Jesus, found myself in the island of Patmos, on account of the Word of God and the truth told us by Jesus.
10 Nilikuwa katika Roho siku ya Bwana. Nilisikia nyuma yangu sauti ya juu kama ya tarumbeta,
In the Spirit I found myself present on the day of the Lord, and I heard behind me a loud voice which resembled the blast of a trumpet.
11 ikisema, “andika katika kitabu unayo yaona, na uyatume kwa makanisa saba, kwenda Efeso, kwenda Smirna, kwenda Pergamo, kwenda Thiatira, kwenda Sardi, kwenda Philadelphia, na kwenda Laodikia.”
It said, "Write forthwith in a roll an account of what you see, and send it to the seven Churches--to Ephesus, Smyrna, Pergamum, Thyateira, Sardis, Philadelphia and Laodicea."
12 Nikageuka kuona ni sauti ya nani aliyekuwa akiongea nami, na nilipogeuka niliona kinara cha dhahabu cha taa saba.
I turned to see who it was that was speaking to me; and then I saw seven golden lampstands,
13 Katikati ya kinara cha taa alikuwemo mmoja kama Mwana wa Adamu, amevaa kanzu ndefu iliyofika chini ya miguu yake, na mkanda wa dhababu kuzunguka kifua chake.
and in the center of the lampstands some One resembling the Son of Man, clothed in a robe which reached to His feet, and with a girdle of gold across His breast.
14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe kama theluji, na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto.
His head and His hair were white, like white wool--as white as snow; and His eyes resembled a flame of fire.
15 Nyayo zake zilikuwa kama shaba iliyosuguliwa sana, kama shaba ambayo imekwisha pitishwa katika moto, na sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji mengi yanayotiririka kwa kasi.
His feet were like silver-bronze, when it is white-hot in a furnace; and His voice resembled the sound of many waters.
16 Alikuwa ameshikilia nyota saba katika mkono wake wa kuume, na kutoka kinywani mwake kulikuwa na upanga mkali wenye makali kuwili. Uso wake ulikuwa uking'aa kama mwanga mkali wa jua.
In His right hand He held seven stars, and a sharp, two-edged sword was seen coming from His mouth; and His glance resembled the sun when it is shining with its full strength.
17 Nilipomwona, nikaanguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kulia juu yangu na kusema, “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa Mwisho,
When I saw Him, I fell at His feet as if I were dead. But He laid His right hand upon me and said, "Do not be afraid: I am the First and the Last, and the ever-living One.
18 na ambaye ninaishi. Nalikuwa nimekufa, lakini tazama, ninaishi milele! Na ninazo funguo za mauti na kuzimu. (aiōn g165, Hadēs g86)
I died; but I am now alive until the Ages of the Ages, and I have the keys of the gates of Death and of Hades! (aiōn g165, Hadēs g86)
19 Kwa hiyo, yaandike uliyoyaona, yaliyopo sasa, na yale yatakayotokea baada ya haya.
Write down therefore the things you have just seen, and those which are now taking place, and those which are soon to follow:
20 Kwa maana iliyojificha kuhusu nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume, na kile kinara cha dhahabu cha taa saba: nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba, na kinara cha taa saba ni yale makanisa saba.”
the secret meaning of the seven stars which you have seen in My right hand, and of the seven lampstands of gold. The seven stars are the ministers of the seven Churches, and the seven lampstands are the seven Churches.

< Ufunuo 1 >