< Ufunuo 1 >

1 Huu ni ufunuo wa Yesu Kristo ambao Mungu alimpa ili kuwaonesha watumishi wake mambo ambayo lazima yatokee karibuni. Aliyafanya yajulikane kwa kumtuma malaika wake kwa mtumishi wake Yohana.
THE UNVEILING APOCALYPSE OF JESUS CHRIST which God gave him to show to his slaves the things which must soon come to pass; and he sent and made it known by his angel to his slave John.
2 Yohana alitoa ushuhuda wa kila kitu alichoona kuhusiana na neno la Mungu na kwa ushuhuda uliotolewa kuhusu Yesu Kristo.
He bore witness of the Word of God, and of the testimony of Jesus Christ, even of all the things that he saw.
3 Amebarikiwa yeye asomaye kwa sauti na wale wote wanaoyasikia maneno ya unabii huu na kutii kilichoandikwa humo, kwa sababu muda umekaribia.
Blessed is he who reads, and they who hear the words of the prophecy, and keep what is written in it. FOR THE CRISIS IS AT HAND.
4 Yohana, kwa makanisa saba yaliyoko Asia: neema iwe kwenu na amani kutoka kwake aliyepo, aliyekuwepo, na atakayekuja, na kutoka kwa roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi,
From John to the seven churches that are in Asia the Roman Province. Grace to you, and peace from Him that is and was and is to be, and from the Seven Spirits that are before his throne,
5 na kutoka kwa Yesu Kristo ambaye ni shahidi mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mtawala wa wafalme wa dunia hii. Kwake yeye atupendaye na ametuweka huru kutoka katika dhambi zetu kwa damu yake,
and from Jesus Christ, the faithful witness, the firstborn of the dead, and the Ruler of the kings of the earth. To Him who loves us and has loosed us from our sins in his own blood;
6 ametufanya kuwa ufalme, makuhani wa Mungu na Baba yake - kwake kuwa utukufu na nguvu milele daima. Amina. (aiōn g165)
and has made us to be a kingdom of priests unto his God and Father; to him be the glory and the dominion forever and ever, Amen. (aiōn g165)
7 Tazama, anakuja na mawingu; kila jicho litamwona, pamoja na wote waliomchoma. Na kabila zote za dunia wataomboleza kwake. Ndiyo, Amina.
Behold, he is about to come among the clouds; and every eye will see him, and all the tribes of the earth will mourn over him. So shall it be, Amen.
8 “Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu, “Yeye aliyepo, na aliyekuwepo, na ambaye anakuja, Mwenye nguvu.”
"I am the Alpha and the Omega," says the Lord God, who is, and who was, and who is to come, the Almighty.
9 Mimi, Yohana - ndugu yenu na mmoja anayeshiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na uvumilivu thabiti ulio katika Yesu; nilikuwa katika kisiwa kiitwacho Patimo kwa sababu ya neno la Mungu na ushuhuda kuhusu Yesu.
I, John, who am your brother and who share with you in the woes and kingdom and stedfastness of Jesus, found myself in the island called Patmos, for the sake of the word of God and the testimony of Jesus.
10 Nilikuwa katika Roho siku ya Bwana. Nilisikia nyuma yangu sauti ya juu kama ya tarumbeta,
I was in the Spirit on the Lord’s day, and I heard a loud voice behind me, like a trumpet,
11 ikisema, “andika katika kitabu unayo yaona, na uyatume kwa makanisa saba, kwenda Efeso, kwenda Smirna, kwenda Pergamo, kwenda Thiatira, kwenda Sardi, kwenda Philadelphia, na kwenda Laodikia.”
saying, "Write in a book what you see, and send it to the seven churches; to Ephesus and to Smyrna and to Pergamum and to Thyatira and Sardis and Philadelphia and Laodicea."
12 Nikageuka kuona ni sauti ya nani aliyekuwa akiongea nami, na nilipogeuka niliona kinara cha dhahabu cha taa saba.
And I turned to see the Voice which was speaking to me, and as I turned I saw seven golden candlesticks;
13 Katikati ya kinara cha taa alikuwemo mmoja kama Mwana wa Adamu, amevaa kanzu ndefu iliyofika chini ya miguu yake, na mkanda wa dhababu kuzunguka kifua chake.
and in the midst of the candlesticks One like to a son of man, clothed with a robe down to the feet, and with a golden girdle round his breast.
14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe kama theluji, na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto.
His head and his hair were as white as wool, as white as snow; his eyes were like a flame of fire,
15 Nyayo zake zilikuwa kama shaba iliyosuguliwa sana, kama shaba ambayo imekwisha pitishwa katika moto, na sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji mengi yanayotiririka kwa kasi.
and his feet like burnished brass, as if molten in a furnace; and his voice like the voice of many waters.
16 Alikuwa ameshikilia nyota saba katika mkono wake wa kuume, na kutoka kinywani mwake kulikuwa na upanga mkali wenye makali kuwili. Uso wake ulikuwa uking'aa kama mwanga mkali wa jua.
In his right hand he held seven stars; and out of mouth went a sharp, two-edged sword, and his face was as the sun shining in his strength.
17 Nilipomwona, nikaanguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kulia juu yangu na kusema, “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa Mwisho,
When I saw him, I fell at his feet as one dead. And he laid his right hand upon me, saying. "Fear not; I am the first and the last, and the Living One.
18 na ambaye ninaishi. Nalikuwa nimekufa, lakini tazama, ninaishi milele! Na ninazo funguo za mauti na kuzimu. (aiōn g165, Hadēs g86)
I was dead, and behold, I am alive forevermore; and hold the keys of death and of Hades. (aiōn g165, Hadēs g86)
19 Kwa hiyo, yaandike uliyoyaona, yaliyopo sasa, na yale yatakayotokea baada ya haya.
So write the things which you saw, and the things which are, and the things that will come to pass hereafter.
20 Kwa maana iliyojificha kuhusu nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume, na kile kinara cha dhahabu cha taa saba: nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba, na kinara cha taa saba ni yale makanisa saba.”
The mystery of the seven stars which you saw in my right hand, and the seven golden candlesticks, is this. The seven stars are the angels of the seven churches, and the seven candlesticks are the seven churches."

< Ufunuo 1 >