< Ufunuo 9 >
1 Kisha malaika wa tano alipiga tarumbeta yake. Niliona nyota kutoka mbinguni iliyokuwa imeanguka kwenye dunia. Nyota ilipewa ufunguo wa shimo linaloelekea kwenye shimo lisilo na mwisho. (Abyssos )
And the fifth angel sounded, and I saw a star fallen out of heaven to the earth, and to him was given the key of the pit of the abyss; (Abyssos )
2 Alifungua shimo lisilo na kikomo, na moshi ukapanda juu kwa safu kutoka ndani ya shimo kama moshi kutoka katika tanuru kubwa. Jua na anga vilibadilika vikawa giza kwa sababu ya moshi uliotoka shimoni. (Abyssos )
and he opened the pit of the abyss. And there went up a smoke out of the pit, as the smoke of a great furnace, and the sun and the air were darkened by reason of the smoke of the pit. (Abyssos )
3 Ndani ya moshi nzige walitoka kuja juu ya dunia, nao walipewa nguvu kama ile ya nge juu ya dunia.
And out of the smoke went forth locusts upon the earth, and to them was given power, as the scorpions of the earth have power;
4 Waliambiwa kutokudhuru majani katika nchi au mmea wowote wa kijani au mti, isipokuwa tu watu ambao hawakuwa na muhuri wa Mungu katika paji za nyuso zao.
and it was commanded them that they should not hurt the grass of the earth, nor any green thing, nor any tree, but only those men who have not the seal of God upon their foreheads;
5 Hawakupewa ruhusa ya kuwaua hao watu, bali kuwatesa tu kwa miezi mitano. Uchungu wao ulikuwa kama ule wa kuumwa na nge amwumapo mtu.
and it was given to them that they should not kill them, but that they should be tormented five months; and their torment was as the torment of a scorpion, when it hath struck a man.
6 Katika siku hizo watu watatafuta kifo, lakini hawatakipata. Watatamani kufa, lakini kifo kitawakimbia.
And in those days men will seek death, and shall not find it; and will desire to die, and death will flee from them.
7 Nzige walifanana na farasi walioandaliwa kwa vita. Kwenye vichwa vyao kulikuwa na kitu kama taji ya dhahabu na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu.
And the shapes of the locusts were like horses prepared for battle; and on their heads were as it were crowns like gold, and their faces were as the faces of men;
8 Walikuwa na nywele kama za wanawake na meno yao yalikuwa kama ya simba.
and they had hair as the hair of women, and their teeth were as the teeth of lions.
9 Walikuwa na vifua kama vifua vya chuma na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya magari mengi ya vita na farasi wakimbiao kwenda vitani.
And they had breastplates like breastplates of iron, and the sound of their wings was as the sound of chariots of many horses running to battle.
10 Walikuwa na mikia inayouma kama nge; katika mikia yao walikuwa na nguvu ya kudhuru watu kwa miezi mitano.
And they have tails like scorpions, and stings; and in their tails is their power to hurt men five months.
11 Walikuwa naye kama mfalme juu yao malaika wa shimo lisilokuwa na mwisho. Jina lake katika Kiebrania ni Abadoni, na katika Kiyunani ana jina Apolioni. (Abyssos )
They have over them a king, the angel of the abyss, whose name in the Hebrew tongue is Abaddon, but in the Greek he hath for his name Apollyon. (Abyssos )
12 Ole ya kwanza imepita. Angalia! Baada ya hili kuna maafa mawili yaja.
The first woe is past; behold, two woes more are yet to come.
13 Malaika wa sita alipiga tarumbeta yake, na nikasikia sauti ikitoka katika pembe ya madhabahu ya dhahabu ambayo iko mbele za Mungu.
And the sixth angel sounded, and I heard a voice out of the four horns of the golden altar, which is before God,
14 Sauti ilimwambia malaika wa sita aliyekuwa na tarumbeta, “Waachie malaika wanne ambao wamefungwa katika mto mkubwa Efrata.”
saying to the sixth angel who had the trumpet, Loose the four angels who are bound at the great river Euphrates.
15 Malaika wale wanne waliokuwa wameandaliwa kwa saa hiyo maalumu, siku hiyo, mwezi huo, na mwaka huo, waliachiwa wawaue theluthi ya wanadamu.
And the four angels were loosed, who were in readiness for the hour, and day, and month, and year, to slay the third part of men.
16 Idadi ya maaskari waliokuwa juu ya farasi ilikuwa 200, 000, 000. Nilisikia idadi yao.
And the number of the armies of the horsemen was two hundred thousand thousand; I heard the number of them.
17 Hivi ndivyo nilivyoona farasi katika maono yangu na wale waliopanda juu yao: Vifua vyao vilikuwa vyekundu kama moto, bluu iliyoiva na njano isiyoiva. Vichwa vya farasi vilifanana na vichwa vya simba, na midomoni mwao ulitoka moto, moshi na salfa.
And thus I saw the horses in the vision, and those who sat on them, having breastplates of a fiery, and a dark blue, and a brimstone color; and the heads of the horses were as the heads of lions, and out of their mouths issued fire, and smoke, and brimstone.
18 Theluthi ya wanadamu waliuawa na haya mapigo matatu: moto, moshi, na salfa iliyotoka katika midomo yao.
By these three plagues was the third part of men killed, by the fire, and the smoke, and the brimstone, which issued out of their mouths.
19 Kwa kuwa nguvu ya farasi ilikuwa katika midomo yao na katika mikia yao—kwa kuwa mikia yao ilikuwa kama nyoka, na walikuwa na vichwa ambavyo walitumia kuwatia majeraha wanadamu.
For the power of the horses is in their mouth, and in their tails; for their tails are like to serpents, having heads; and with them they do hurt.
20 Watu waliobaki, wale ambao walikuwa hawajauawa na mapigo haya, hawakutubia matendo yao waliyokuwa wamefanya, wala hawakuacha kuabudu mapepo na miungu ya dhahabu, fedha, shaba, mawe na miti—vitu ambavyo haviwezi kuona, kusikia au kutembea.
And the rest of men, who were not killed by these plagues, did not repent of the works of their hands, that they should not worship demons, and idols of gold, and of silver, and of brass, and of stone, and of wood, which can neither see; nor hear, nor walk;
21 Wala hawakutubia uuaji wao, uchawi wao, uasherati wao au njia zao za wizi.
and they did not repent of their murders, nor of their sorceries, nor of their fornication, nor of their thefts.