< Ufunuo 9 >

1 Kisha malaika wa tano alipiga tarumbeta yake. Niliona nyota kutoka mbinguni iliyokuwa imeanguka kwenye dunia. Nyota ilipewa ufunguo wa shimo linaloelekea kwenye shimo lisilo na mwisho. (Abyssos g12)
Then the fifth angel blew his trumpet, and I saw a star fallen from heaven upon the earth; and to him was given the key to the bottomless pit. (Abyssos g12)
2 Alifungua shimo lisilo na kikomo, na moshi ukapanda juu kwa safu kutoka ndani ya shimo kama moshi kutoka katika tanuru kubwa. Jua na anga vilibadilika vikawa giza kwa sababu ya moshi uliotoka shimoni. (Abyssos g12)
And he opened the bottomless pit, and out of the pit there went up a smoke like the smoke of a great furnace. And the sun and the air grew dark, because of the smoke out of the pit. (Abyssos g12)
3 Ndani ya moshi nzige walitoka kuja juu ya dunia, nao walipewa nguvu kama ile ya nge juu ya dunia.
And out of the smoke came locusts upon the earth; they were given power like that of scorpions on the earth.
4 Waliambiwa kutokudhuru majani katika nchi au mmea wowote wa kijani au mti, isipokuwa tu watu ambao hawakuwa na muhuri wa Mungu katika paji za nyuso zao.
They were told not to hurt the grass of the earth, nor any plant, nor any tree, but only those who have not the seal of God on their foreheads.
5 Hawakupewa ruhusa ya kuwaua hao watu, bali kuwatesa tu kwa miezi mitano. Uchungu wao ulikuwa kama ule wa kuumwa na nge amwumapo mtu.
Yet they were not permitted to kill them, but only to torture them for five months. Their torture was like the torture of a scorpion, when it stings a man.
6 Katika siku hizo watu watatafuta kifo, lakini hawatakipata. Watatamani kufa, lakini kifo kitawakimbia.
In those days men will seek death, and will not find it; they will long to die, but death ever flees from them.
7 Nzige walifanana na farasi walioandaliwa kwa vita. Kwenye vichwa vyao kulikuwa na kitu kama taji ya dhahabu na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu.
The appearance of the locusts was like horses equipped for battle. On their heads there was something like crowns of gold, and their faces were like men’s faces,
8 Walikuwa na nywele kama za wanawake na meno yao yalikuwa kama ya simba.
and they had hair like the hair of women, and their teeth were like lion’s teeth,
9 Walikuwa na vifua kama vifua vya chuma na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya magari mengi ya vita na farasi wakimbiao kwenda vitani.
and they had breastplates something like breastplates of iron; and the noise of their wings was like the noise of chariots, of many horses rushing into battle.
10 Walikuwa na mikia inayouma kama nge; katika mikia yao walikuwa na nguvu ya kudhuru watu kwa miezi mitano.
And they have tails like scorpions, and stings, and their power to torture men five months was in their tails.
11 Walikuwa naye kama mfalme juu yao malaika wa shimo lisilokuwa na mwisho. Jina lake katika Kiebrania ni Abadoni, na katika Kiyunani ana jina Apolioni. (Abyssos g12)
They have a king over them, the angel of the bottomless pit. His name in Hebrew is Abaddon; in Greek he is called Apollyon. (Abyssos g12)
12 Ole ya kwanza imepita. Angalia! Baada ya hili kuna maafa mawili yaja.
"The first woe has passed; and still there are two woes to follow."
13 Malaika wa sita alipiga tarumbeta yake, na nikasikia sauti ikitoka katika pembe ya madhabahu ya dhahabu ambayo iko mbele za Mungu.
Then the sixth angel blew his trumpet; and I heard a voice from the horns of the golden altar which is before God,
14 Sauti ilimwambia malaika wa sita aliyekuwa na tarumbeta, “Waachie malaika wanne ambao wamefungwa katika mto mkubwa Efrata.”
one saying to the sixth angel that had the trumpet, "Loose the four angels which are bound at the great river Euphrates."
15 Malaika wale wanne waliokuwa wameandaliwa kwa saa hiyo maalumu, siku hiyo, mwezi huo, na mwaka huo, waliachiwa wawaue theluthi ya wanadamu.
Then the four angels that were held in readiness for that hour and day and month and year, were let loose, to destroy a third of mankind.
16 Idadi ya maaskari waliokuwa juu ya farasi ilikuwa 200, 000, 000. Nilisikia idadi yao.
The number of the hosts of the horsemen was twice ten thousand times ten thousand. I heard their number;
17 Hivi ndivyo nilivyoona farasi katika maono yangu na wale waliopanda juu yao: Vifua vyao vilikuwa vyekundu kama moto, bluu iliyoiva na njano isiyoiva. Vichwa vya farasi vilifanana na vichwa vya simba, na midomoni mwao ulitoka moto, moshi na salfa.
and thus I saw the horses in the vision and their riders. They had breastplates of fire, "red as fire, dark blue as jacinth, and yellow as sulphur." The heads of the horses were like lions’ heads, and out of their mouths issued fire and smoke and brimstone.
18 Theluthi ya wanadamu waliuawa na haya mapigo matatu: moto, moshi, na salfa iliyotoka katika midomo yao.
By these three plagues a third of mankind were killed; by the fire and the smoke and the brimstone which issued from their mouths.
19 Kwa kuwa nguvu ya farasi ilikuwa katika midomo yao na katika mikia yao—kwa kuwa mikia yao ilikuwa kama nyoka, na walikuwa na vichwa ambavyo walitumia kuwatia majeraha wanadamu.
For the power of the horses is in their mouths and in their tails. For their tails are like serpents with heads, and with them they work woe.
20 Watu waliobaki, wale ambao walikuwa hawajauawa na mapigo haya, hawakutubia matendo yao waliyokuwa wamefanya, wala hawakuacha kuabudu mapepo na miungu ya dhahabu, fedha, shaba, mawe na miti—vitu ambavyo haviwezi kuona, kusikia au kutembea.
And the rest of mankind who were not killed with these plagues, did not repent of the works of their hands. They would not give up the worship of demons and of idols made of gold and silver, and brass, and stone, and wood, which can neither see, nor hear, nor walk.
21 Wala hawakutubia uuaji wao, uchawi wao, uasherati wao au njia zao za wizi.
And they did not repent of their murders, nor of their sorceries, nor of their immorality, nor of their thefts.

< Ufunuo 9 >