< Ufunuo 7 >

1 Baada ya haya niliona malaika wanne wamesimama kwenye kona nne za dunia, wamezuia pepo nne za nchi kwa nguvu ili kwamba pasiwe na upepo unaovuma katika nchi, juu ya bahari au dhidi ya mti wowote.
After this I saw four angels, standing at the four corners of the earth, restraining the four winds from blowing on the earth, or on the sea, or on any tree.
2 Nikaona malaika mwingine akija kutoka mashariki, aliyekuwa na muhuri wa Mungu aliye hai. Akalia kwa sauti kuu kwa malaika wanne ambao walipewa ruhusa ya kudhuru nchi na bahari:
And I saw another angel ascend from the sunrising, having a seal of the living God; and he cried with a great voice to the four angels to whom it was given to injure the earth and the sea,
3 “Msiidhuru nchi, bahari, au miti mpaka tutakapokuwa tumekwishaweka muhuri katika paji za vichwa vya watumishi wa Mungu wetu.”
saying, "Do no harm to the earth, or the sea, or the trees, Until we have sealed the slaves of our God on their foreheads."
4 Nikasikia idadi ya wale waliotiwa muhuri: 144, 000, ambao walitiwa muhuri kutoka kila kabila ya watu wa Israel:
And I heard the number of those who were sealed, a hundred and forty and four thousand, sealed out of every tribe of the children of Israel.
5 12, 000 kutoka katika kabila ya Yuda walitiwa muhuri, 12, 000 kutoka katika kabila ya Rubeni, 12, 000 kutoka katika kabila ya Gadi.
Of the tribe of Judah, twelve thousand were sealed; Of the tribe of Reuben, twelve thousand; Of the tribe of Gad, twelve thousand;
6 12, 000 kutoka katika kabila ya Asheri, 12, 000 kutoka katika kabila ya Naftali, 12, 000 kutoka katika kabila ya Manase.
Of the tribe of Asher, twelve thousand; Of the tribe of Naphtali, twelve thousand; Of the tribe of Manasseh, twelve thousand;
7 12, 000 kutoka kabila ya Simioni, 12, 000 kutoka kabila ya Lawi, 12, 000 kutoka kabila ya Isakari,
Of the tribe of Symeon, twelve thousand; Of the tribe of Levi, twelve thousand; Of the tribe of Issachar, twelve thousand;
8 12, 000 kutoka kabila ya Zebuloni, 12, 000 kutoka kabila ya Yusufu, na 12, 000 kutoka kabila ya Benyamini walitiwa muhuri.
Of the tribe of Zebulun, twelve thousand; Of the tribe of Joseph, twelve thousand; Of the tribe of Benjamin, twelve thousand;
9 Baada ya mambo haya nilitazama, na kulikuwa na umati mkubwa ambao hapana mtu angeweza kuuhesabu - kutoka kila taifa, kabila, jamaa, na lugha - wamesimama mbele ya kiti cha enzi na mbele ya Mwanakondoo. Walikuwa wamevaa kanzu nyeupe na wana matawi ya mitende mikononi mwao,
After this I looked, and behold a great multitude, whom no man could number, out of every nation and tribe and people and tongue, standing before the throne and before the Lamb, clothed in white robes, with palm branches in their hands;
10 na walikuwa wakiita kwa sauti ya juu: “Wokovu ni kwa Mungu ambaye ameketi katika kiti cha enzi, na kwa Mwanakondoo!”
and they cried with a loud voice, saying "Salvation to our God, who sits on the throne, And to the Lamb!"
11 Malaika wote waliokuwa wamesimama kuzunguka kiti cha enzi na kuwazunguka wale wazee pamoja na wenye uhai wanne, wakainama chini ardhini na wakaweka nyuso zao juu ya ardhi mbele ya kiti cha enzi na wakamwabudu Mungu,
And all the angels stood encircling the throne, and the Elders and the Living Creatures; and they fell on their faces before the throne, worshiping God,
12 wakisema, “Amina! Sifa, utukufu, hekima, shukurani, heshima, uwezo na nguvu viwe kwa Mungu wetu milele na milele! Amina!” (aiōn g165)
and crying, "Even so! The blessing and the glory and the wisdom And the thanksgiving and the honor and the power and the might Be to our God forever and ever. Amen." (aiōn g165)
13 Kisha mmoja wa wale wazee akaniuliza, “hawa ni akina nani waliovaa kanzu nyeupe, na wametoka wapi?
And one of the Elders spoke to me, saying. "Who are these, clad in white robes? Whence come they?"
14 Nikamwambia, “Bwana mkubwa, unajua wewe,” na akaniambia, “Hawa ni wale waliotoka katika dhiki kuu. Wamezifua kanzu zao na kuzifanya nyeupe kwa damu ya Mwanakondoo.
And I said to him, "You know, my Lord." And he said to me, "These are those who have come out of the great persecution, and have washed their robes and made them white in the blood of the Lamb.
15 Kwa sababu hii, wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, na wanamwabudu yeye usiku na mchana katika hekalu lake. Yeye aliye keti juu ya kiti cha enzi atasambaza hema yake juu yao.
For this they are now before the throne of God, and are serving him day and night in his temple. "And He who sits on the throne Will spread his tabernacle over them.
16 Hawataona njaa tena, wala kiu tena. Jua halitawachoma, wala joto la kuunguza.
They hunger no more, Neither thirst any more; Neither will the sun strike upon them, Nor any scorching heat;
17 Kwa kuwa Mwanakondoo aliye katikati ya kiti cha enzi atakuwa mchungaji wao, na atawaongoza katika chemchemi ya maji ya uzima, na Mungu atafuta kila chozi katika macho yao.”
For the Lamb in the midst of the throne Will shepherd them, And will lead them to fountains of living water; And God will wipe away every tear from their eyes."

< Ufunuo 7 >