< Ufunuo 5 >

1 Kisha nikaona katika mkono wa kulia wa yule aliyekuwa amekaa katika kiti cha enzi, gombo lililoandikwa mbele na nyuma, na lilikuwa limetiwa mihuri saba.
And I saw upon the right hand of Him who is sitting upon the throne a scroll, written within and on the back, sealed with seven seals;
2 Nilimwona malaika mwenye nguvu akihubiri kwa sauti kubwa, “Nani astahiliye kulifungua gombo na kuzivunja mihuri yake?”
and I saw a strong messenger crying with a great voice, 'Who is worthy to open the scroll and to loose the seals of it?'
3 Hakuna mtu mbinguni au duniani au chini ya dunia aliyeweza kulifungua gombo au kulisoma.
and no one was able in the heaven, nor upon the earth, nor under the earth, to open the scroll, nor to behold it.
4 Nililia kwa uchungu kwa kuwa hakupatikana yeyote aliyestahili kulifungua gombo au kulisoma.
And I was weeping much, because no one was found worthy to open and to read the scroll, nor to behold it,
5 Lakini mmoja wa wazee akaniambia, “Usilie. Tazama! Simba wa kabila ya Yuda, shina la Daudi, ameshinda, na anaweza kulifungua gombo na mihuri yake saba.”
and one of the elders saith to me, 'Weep not; lo, overcome did the Lion, who is of the tribe of Judah, the root of David, to open the scroll, and to loose the seven seals of it;
6 Kati ya kiti cha enzi na wenye uhai wanne na miongoni mwa wazee, niliona mwanakondoo amesimama, akionekana kama aliye uawa. Alikuwa na pembe saba na macho saba - hizi ni roho saba za Mungu zilizotumwa duniani kote.
and I saw, and lo, in the midst of the throne, and of the four living creatures, and in the midst of the elders, a Lamb hath stood as it had been slain, having seven horns and seven eyes, which are the Seven Spirits of God, which are sent to all the earth,
7 Akaenda akalichukua gombo kutoka katika mkono wa kuume wa yule aliye kaa katika kiti cha enzi.
and he came and took the scroll out of the right hand of Him who is sitting upon the throne.
8 Alipolichukua gombo, wenye uhai wanne na wazee ishirini na wanne wakainama hadi nchi mbele ya mwanakondoo. Kila mmoja alikuwa na kinubi na bakuli ya dhahabu iliyojaa uvumba ambayo ni maombi ya waamini.
And when he took the scroll, the four living creatures and the twenty-four elders fell before the Lamb, having each one harps and golden vials full of perfumes, which are the prayers of the saints,
9 Waliimba wimbo mpya: “Unastahili kulitwaa gombo na kuzifungua muhuri zake. Kwa kuwa ulichinjwa, na kwa damu yako ukamnunulia Mungu watu wa kila kabila, lugha, jamaa na taifa.
and they sing a new song, saying, 'Worthy art thou to take the scroll, and to open the seals of it, because thou wast slain, and didst redeem us to God in thy blood, out of every tribe, and tongue, and people, and nation,
10 Ukawafanya ufalme na makuhani kwa ajili ya kumtumikia Mungu wetu, nao watatawala juu ya nchi.”
and didst make us to our God kings and priests, and we shall reign upon the earth.'
11 Kisha nilitazama na nikasikia sauti ya malaika wengi kuzunguka kiti cha enzi - idadi yao ilikuwa 200, 000, 000 na wenye uhai na wazee.
And I saw, and I heard the voice of many messengers round the throne, and the living creatures, and the elders — and the number of them was myriads of myriads, and thousands of thousands —
12 Wakasema kwa sauti kuu, “Astahili mwanakondoo ambaye amechinjwa kupokea uwezo, utajiri, hekima, nguvu, heshima, utukufu, na sifa.”
saying with a great voice, 'Worthy is the Lamb that was slain to receive the power, and riches, and wisdom, and strength, and honour, and glory, and blessing!'
13 Nikasikia kila kilichoumbwa kilichokuwa mbinguni na duniani na chini ya nchi na juu ya bahari, kila kitu ndani yake kikisema, “Kwake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi na kwa mwanakondoo, kuwe sifa, heshima, utukufu na nguvu ya kutawala milele na milele.” (aiōn g165)
and every creature that is in the heaven, and in the earth, and under the earth, and the things that are upon the sea, and the all things in them, heard I saying, 'To Him who is sitting upon the throne, and to the Lamb, [is] the blessing, and the honour, and the glory, and the might — to the ages of the ages!' (aiōn g165)
14 Wenye uhai wanne wakasema, “Amina!” na wazee wakainama chini na kuabudu.
and the four living creatures said, 'Amen!' and the twenty-four elders fell down and they bow before Him who is living to the ages of the ages.

< Ufunuo 5 >