< Ufunuo 4 >
1 Baada ya mambo haya nilitazama, nikaona kuwa mlango ulikuwa umefunguliwa mbinguni. Ile sauti ya kwanza, ikizungumza nami kama tarumbeta, ikisema, “Njoo hapa, nitakuonesha yatakayotokea baada ya mambo haya.”
After these things I saw, and behold, a door was opened in heaven; and the first voice which I heard, like the voice of a trumpet speaking with me, said: Come up hither, and I will show you things that must be hereafter.
2 Mara moja nilikuwa katika Roho, niliona kulikuwa na kiti cha enzi kimewekwa mbinguni, na mtu amekikalia.
And immediately I was in spirit; and behold, a throne was set in heaven, and one sat on the throne;
3 Mmoja aliyekuwa amekikalia alionekana kama jiwe la yaspi na akiki. Kulikuwa na upinde wa mvua umekizunguka kiti cha enzi. Upinde wa mvua ulionekana kama zumaridi.
and he that sat was, in appearance, like a jasper and sardine-stone: and there was round about the throne a rainbow, in appearance like an emerald.
4 Kukizunguka kiti cha enzi kulikuwa na viti vya enzi vingine ishirini na vinne, na waliokaa kwenye viti vya enzi walikuwa wazee ishirini na wanne, wamevikwa mavazi meupe na taji za dhahabu vichwani mwao.
And round about the throne were twenty-four thrones; and on the thrones there sat twenty-four elders, clothed in white raiment; and on their heads were crowns of gold.
5 Kutoka katika kiti cha enzi kulitoka miale ya radi, muungurumo na radi. Taa saba zilikuwa zikiwaka mbele ya kiti cha enzi, taa ambazo ni roho saba za Mungu.
And out of the throne there went lightnings and thunderings and voices; and seven lamps of fire were burning before the throne: these are the seven spirits of God.
6 Tena mbele ya kiti cha enzi kulikuwa na bahari, iliyowazi kama kioo. Wote kuzunguka kiti cha enzi kulikuwa na wenye uhai wanne, waliojaa macho mbele na nyuma.
And before the throne there was a sea of glass, like crystal. And in the midst of the throne, and round about the throne, were four living creatures full of eyes before and behind.
7 Kiumbe wa kwanza mwenye uhai alikuwa kama simba, kiumbe wa pili mwenye uhai alikuwa kama ndama, kiumbe wa tatu mwenye uhai alikuwa na uso kama wa mwanadamu, na yule mwenye uhai wa nne alikuwa kama tai apaaye.
And the first living creature was like a lion, and the second living creature was like a calf, and the third living creature had the face of a man, and the fourth living creature was like a flying eagle.
8 Viumbe wenye uhai wanne kila mmoja alikuwa na mabawa sita, wamejaa macho juu na chini yake. Usiku na mchana hawakomi kusema, “Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Bwana Mungu, mtawala juu ya wote, aliyekuwepo, na aliyepo na atakayekuja.”
And the four living creatures had each of them six wings about him; and they are full of eyes within; and they have no rest day and night, saying, Holy, holy, holy is the Lord God, the Almighty, who was, and is, and is to come.
9 Kila wakati viumbe wenye uhai walipotoa utukufu, heshima, na kushukuru mbele za aliyekuwa ameketi kwenye hicho kiti cha enzi, yeye aishiye milele na daima, (aiōn )
And when the living creatures give glory and honor and thanks to him that sits on the throne, who lives from age to age, (aiōn )
10 wazee ishirini na wanne walisujudu wenyewe mbele yake aliyekikalia kiti cha enzi. Waliinama chini kwake aishiye milele na daima na kutupa chini taji zao mbele ya kiti cha enzi wakisema, (aiōn )
the twenty-four elders fall down before him that sits on the throne, and worship him that lives from age to age, and throw their crowns before the throne, saying: (aiōn )
11 “Wastahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu. Kwa kuwa uliviumba vitu vyote, na kwa mapenzi yako, vilikuwepo na viliumbwa.”
Thou art worthy, O Lord, to receive glory and honor and power: for thou hast created all things, and by thy will they exist, and were created.