< Ufunuo 21 >
1 Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya, kwa kuwa mbingu ya kwanza na nchi ya kwanza zimekwishapita, na bahari haikuwepo tena.
And I sawe a newe heven and a newe erth For the fyrst heven and the fyrst erth were vanysshed awaye and there was no more see.
2 Niliona mji mtakatifu, Yerusalemu mpya, ambao ulikuja chini kutoka mbinguni kwa Mungu, ulioandaliwa kama bibi harusi aliyepambwa kwa ajili ya mumewe.
And I Iho sawe that holy cite newe Ierusalem come doune from God oute of heven prepared as a bryde garnysshed for hyr husband.
3 Nilisikia sauti kubwa kutoka kwenye kiti cha enzi ikisema, “Tazama! Makao ya Mungu yapo pamoja na wanadamu, naye ataishi pamoja nao. Watakuwa watu wake, na Mungu mwenyewe atakuwa nao na atakuwa Mungu wao.
And I herde a grett voyce out of heaven sayinge: beholde the tabernacle of God is with men and he will dwell with the And they shalbe his people and God him sylffe shalbe with the and be their god.
4 Atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na hapatakuwa na kifo tena, au kuomboleza, au kulia, au maumivu. Mambo ya zamani yamekwishakupita.
And God shall wype awaye all teares fro their eyes. And there shalbe nomore deeth nether sorowe nether cryinge nether shall there be eny more payne for the olde thynges are gone.
5 Yeye ambaye alikuwa ameketi juu ya kiti cha enzi alisema, “Tazama! Nafanya mambo yote kuwa mapya.” Alisema, “Andika hili kwa sababu maneno haya ni ya hakika na kweli.”
And he that sate apon the seate sayde: Behold I make all thynges newe. And he sayde vnto me: wryte for these wordes are faythfull and true.
6 Aliniambia, “Mambo haya yalikwisha kupita! Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. Kwa yeyote aonaye kiu nitampatia kinywaji bila gharama kutoka katika chemchemi za maji ya uzima.
And he sayde vnto me: it is done I am Alpha and Omega the begynnynge and the ende. I will geve to him yt is a thyrst of the well of the water of lyfe fre.
7 Yeye ashindaye atayarithi mambo haya, na nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
He that overcometh shall inheret all thynges and I will be his God and he shalbe my sonne.
8 Lakini kama ilivyo kwa waoga, wasioamini, wachukizao, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, na waongo wote, sehemu yao itakuwa katika ziwa la moto wa kiberiti uunguzao. Hiyo ndiyo mauti ya pili.” (Limnē Pyr )
But the fearefull and vnbelevynge and the abhominable and murdrers and whormongers and sorcerers and ydolaters and all lyars shall have their parte in the lake which burnyth with fyre and brymstone which is the seconde deth. (Limnē Pyr )
9 Mmoja wa malaika saba alikuja kwangu, mmoja ambaye alikuwa na mabakuli saba yaliyojaa mapigo saba ya mwisho na alisema, “Njoo hapa. Nitakuonesha bibi harusi, mke wa mwana kondoo.”
And there cam vnto me one of the vii. angels which had the vii. vyals full of the vii. laste plages: and talked with me sayinge: come hydder I will shewe the the bryde the lambes wyfe.
10 Kisha alinichukua mbali katika Roho kwenye mlima mkubwa na mrefu na alinionesha mji mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka chini kutoka mbinguni kwa Mungu.
And he caryed me awaye in the sprete to a grett and an hye mountayne and he shewed me the grett cite holy Ierusalem descendinge out of heven fro God
11 Yerusalemu ulikuwa na utukufu wa Mungu, na uzuri wake ulikuwa kama kito cha thamani, kama jiwe la kioo safi la yaspi.
havynge the brightnes of God. And her shynynge was lyke vnto a stone moste precious even a Iaspar cleare as cristall:
12 Ulikuwa na ukuta mkubwa, mrefu wenye milango kumi na miwili, pamoja na malaika kumi na wawili milangoni. Juu ya milango palikuwa pameandikwa majina ya makabila kumi na mawili ya wana wa Israeli.
and had walles grett and hye and had xii gates and at the gates xii. angels: and names written which are the xii. trybes of Israell:
13 Upande wa mashariki palikuwa na milango mitatu, upande wa kusini milango mitatu, upande wa kaskazini milango mitatu, na upande wa magharibi milango mitatu.
on the est parte iii gatis and on the north syde iii gates and to wardes the south iii gates and from the west iii gates:
14 Kuta za mji zilikuwa na misingi kumi na miwili, na juu yake palikuwa na majina kumi na mawili ya mitume kumi na wawili wa Mwana Kondoo.
and the wall of the cite had xii foundacions and in them the names of the lambes. xii. Apostles.
15 Mmoja aliyeongea nami alikuwa na kipimo cha fimbo iliyotengenezwa kwa dhahabu kwa ajili ya kupima mji, milango yake na kuta zake.
And he that talked with me had a golden read to measure the cite with all and the gates therof and the wall therof.
16 Mji uliwekwa ndani ya mraba; urefu wake ulikuwa sawa na upana wake. Alipima mji kwa kipimio cha fimbo, stadia 12, 000 kwa urefu (urefu wake, upana, na kimo vilifanana).
And the cite was bylt iiii. square and the length was as large as the bredth of it and he measured the cite with the rede. xii M. fur longes: and the lenght and the bredth and ye heyth of it were equall.
17 Vilevile alipima ukuta wake, unene wake ulikuwa dhiraa 144 kwa vipimo vya kibinadamu (ambavyo pia ni vipimo vya malaika).
And he measured the wall therof. an cxliiii. cubittes: the measure that ye angell had was after the measure that man vseth.
18 Ukuta ulikuwa umejengwa kwa yaspi na mji wenye dhahabu safi, kama kioo safi.
And the byldinge of the wall of it was of iaspar. And the cite was pure gold lyke vnto cleare glasse
19 Misingi ya ukuta ilikuwa imepambwa na kila aina ya jiwe la thamani. La kwanza lilikuwa yaspi, la pili lilikuwa yakuti samawi, la tatu lilikuwa kalkedon, la nne zumaridi,
and the foundacions of the wall of ye cite was garnisshed with all maner of precious stones The fyrste foundacion was iaspar the seconde saphyre the thyrde a calcedony the fourth an emeralde:
20 la tano sardoniki, la sita akiki, la saba krisolitho, la nane zabarajadi, la tisa yakuti ya manjano, la kumi krisopraso, la kumi na moja hiakintho, la kumi na mbili amethisto.
the fyft sardonix: the sixt sardeos: the seventh crysolite the ayght berall: the nynth a topas: the tenth a crysoprasos: the eleventh a iacyncte: the twelfe an amatist.
21 Milango kumi na miwili ilikuwa lulu kumi na mbili, kila mlango ulitengenezwa kutoka kwenye lulu moja. Mitaa ya mji ilikuwa dhahabu safi, ikionekana kama kioo safi.
The xii. gates were xii pearles every gate was of one pearle and the strete of the cite was pure golde as thorowe shynynge glasse.
22 Sikuona hekalu lolote ndani ya mji, kwa kuwa Bwana Mungu, ambaye anatawala juu ya vyote, na Mwana Kondoo ni hekalu lake.
And there was no temple therin. For the lord god allmyghty and the lambe are the temple of it
23 Mji haukuhitaji jua au mwezi ili kungaza juu yake kwa sababu utukufu wa Mungu uliangaza juu yake, na taa yake ni Mwana Kondoo.
and the cite hath no nede of the sonne nether of the mone to lyghten it. For the bryghtnes of God dyd light it: and the lambe was the light of it.
24 Mataifa watatembea kwa mwanga wa mji huo. Wafalme wa dunia wataleta fahari zao ndani yake.
And the people which are saved shall walke in the light of it: and the kynges of the erth shall brynge their glory vnto it.
25 Milango yake haitafungwa wakati wa mchana, na hapatakuwa na usiku pale.
And ye gates of it are not shut by daye. For there shalbe no nyght there.
26 Wataleta fahari na heshima ya mataifa ndani yake,
27 na hakuna kichafu kitakachoingia ndani yake. Wala yeyote ambaye afanyaye jambo lolote la aibu au udanganyifu hataingia, bali ni wale tu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana Kondoo.
And there shall entre into it none vnclene thynge: nether what soever worketh abhominacion: or maketh lyes: but they only which are wrytten in the lambes boke of lyfe.