< Ufunuo 21 >

1 Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya, kwa kuwa mbingu ya kwanza na nchi ya kwanza zimekwishapita, na bahari haikuwepo tena.
And I saw a new heaven and a new earth, for the first heaven and the first earth passed away, and the sea is no more.
2 Niliona mji mtakatifu, Yerusalemu mpya, ambao ulikuja chini kutoka mbinguni kwa Mungu, ulioandaliwa kama bibi harusi aliyepambwa kwa ajili ya mumewe.
And I saw the holy city, new Jerusalem, coming down out of heaven from God, having been prepared as a bride adorned for her husband.
3 Nilisikia sauti kubwa kutoka kwenye kiti cha enzi ikisema, “Tazama! Makao ya Mungu yapo pamoja na wanadamu, naye ataishi pamoja nao. Watakuwa watu wake, na Mungu mwenyewe atakuwa nao na atakuwa Mungu wao.
And I heard a great voice out of heaven saying, Behold, the tabernacle of God is with men, and he will dwell with them, and they will be his people. And God himself will be with them.
4 Atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na hapatakuwa na kifo tena, au kuomboleza, au kulia, au maumivu. Mambo ya zamani yamekwishakupita.
And he will wipe away every tear from their eyes. And there will not be any more death, nor grief, nor crying, nor will there be any more anguish, because the former things are gone.
5 Yeye ambaye alikuwa ameketi juu ya kiti cha enzi alisema, “Tazama! Nafanya mambo yote kuwa mapya.” Alisema, “Andika hili kwa sababu maneno haya ni ya hakika na kweli.”
And he who sits upon the throne said, Behold, I make all things new. And he says to me, Write, because these words are true and faithful.
6 Aliniambia, “Mambo haya yalikwisha kupita! Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. Kwa yeyote aonaye kiu nitampatia kinywaji bila gharama kutoka katika chemchemi za maji ya uzima.
And he said to me, I have become, I, the Alpha and the Omega, the beginning and the end. I will give to him who is thirsty of the fountain of the water of life freely.
7 Yeye ashindaye atayarithi mambo haya, na nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
He who overcomes will inherit these things, and I will be God to him, and he will be a son to me.
8 Lakini kama ilivyo kwa waoga, wasioamini, wachukizao, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, na waongo wote, sehemu yao itakuwa katika ziwa la moto wa kiberiti uunguzao. Hiyo ndiyo mauti ya pili.” (Limnē Pyr g3041 g4442)
But for the cowards, and unbelieving, and sinful, and abominable, and murderers, and fornicators, and sorcerers, and idolaters, and all liars, their part is in the lake that burns with fire and brimstone, which is the second death. (Limnē Pyr g3041 g4442)
9 Mmoja wa malaika saba alikuja kwangu, mmoja ambaye alikuwa na mabakuli saba yaliyojaa mapigo saba ya mwisho na alisema, “Njoo hapa. Nitakuonesha bibi harusi, mke wa mwana kondoo.”
And there came one of the seven agents who had the seven bowls containing the seven last plagues, and he spoke with me, saying, Come, I will show thee the woman, the bride of the Lamb.
10 Kisha alinichukua mbali katika Roho kwenye mlima mkubwa na mrefu na alinionesha mji mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka chini kutoka mbinguni kwa Mungu.
And he carried me away in spirit to a great and high mountain, and showed me the great city, holy Jerusalem, coming down out of heaven from God,
11 Yerusalemu ulikuwa na utukufu wa Mungu, na uzuri wake ulikuwa kama kito cha thamani, kama jiwe la kioo safi la yaspi.
having the glory of God, the light of it similar to a most precious stone, like a jasper stone being crystal clear,
12 Ulikuwa na ukuta mkubwa, mrefu wenye milango kumi na miwili, pamoja na malaika kumi na wawili milangoni. Juu ya milango palikuwa pameandikwa majina ya makabila kumi na mawili ya wana wa Israeli.
which has a great and high wall having twelve gates, and at the gates twelve agents, and names inscribed, which are the names of the twelve tribes of the sons of Israel:
13 Upande wa mashariki palikuwa na milango mitatu, upande wa kusini milango mitatu, upande wa kaskazini milango mitatu, na upande wa magharibi milango mitatu.
from the east, three gates, and from the north, three gates, and from the south, three gates, and from the west, three gates.
14 Kuta za mji zilikuwa na misingi kumi na miwili, na juu yake palikuwa na majina kumi na mawili ya mitume kumi na wawili wa Mwana Kondoo.
And the wall of the city having twelve foundations, and on them the twelve names of the twelve apostles of the Lamb.
15 Mmoja aliyeongea nami alikuwa na kipimo cha fimbo iliyotengenezwa kwa dhahabu kwa ajili ya kupima mji, milango yake na kuta zake.
And he who spoke with me had a measure, a golden reed, so that he might measure the city, and the gates of it, and the walls of it.
16 Mji uliwekwa ndani ya mraba; urefu wake ulikuwa sawa na upana wake. Alipima mji kwa kipimio cha fimbo, stadia 12, 000 kwa urefu (urefu wake, upana, na kimo vilifanana).
And the city lies foursquare, and the length of it is as great as the breadth. And he measured the city with the reed, twelve thousand furlongs, the length and the breadth and the height of it being equal.
17 Vilevile alipima ukuta wake, unene wake ulikuwa dhiraa 144 kwa vipimo vya kibinadamu (ambavyo pia ni vipimo vya malaika).
And he measured the wall of it, a hundred and forty-four forearms, a measure of a man, that is, of an agent.
18 Ukuta ulikuwa umejengwa kwa yaspi na mji wenye dhahabu safi, kama kioo safi.
And the structure of its wall was jasper. And the city was pure gold, similar to clear glass.
19 Misingi ya ukuta ilikuwa imepambwa na kila aina ya jiwe la thamani. La kwanza lilikuwa yaspi, la pili lilikuwa yakuti samawi, la tatu lilikuwa kalkedon, la nne zumaridi,
And the foundations of the wall of the city adorned with every precious stone. The first foundation was jasper, the second, sapphire, the third, chalcedony, the fourth, emerald,
20 la tano sardoniki, la sita akiki, la saba krisolitho, la nane zabarajadi, la tisa yakuti ya manjano, la kumi krisopraso, la kumi na moja hiakintho, la kumi na mbili amethisto.
the fifth, sardonyx, the sixth, sardius, the seventh, chrysolite, the eighth, beryl, the ninth, topaz, the tenth, chrysoprase, the eleventh, jacinth, the twelfth, amethyst.
21 Milango kumi na miwili ilikuwa lulu kumi na mbili, kila mlango ulitengenezwa kutoka kwenye lulu moja. Mitaa ya mji ilikuwa dhahabu safi, ikionekana kama kioo safi.
And the twelve gates were twelve pearls apiece, each one of the gates was of one pearl. And the thoroughfare of the city was pure gold, like transparent glass.
22 Sikuona hekalu lolote ndani ya mji, kwa kuwa Bwana Mungu, ambaye anatawala juu ya vyote, na Mwana Kondoo ni hekalu lake.
And I saw no temple in it, for the Lord God Almighty is the temple of it, and the Lamb.
23 Mji haukuhitaji jua au mwezi ili kungaza juu yake kwa sababu utukufu wa Mungu uliangaza juu yake, na taa yake ni Mwana Kondoo.
And the city has no need of the sun, nor of the moon, so that they might shine in it, for the glory of God illuminated it, and the light of it is the Lamb.
24 Mataifa watatembea kwa mwanga wa mji huo. Wafalme wa dunia wataleta fahari zao ndani yake.
And the nations will walk by the light of it. And the kings of the earth bring to them the splendor and worth of the nations into it.
25 Milango yake haitafungwa wakati wa mchana, na hapatakuwa na usiku pale.
And the gates of it will, no, not be locked by day, for there will be no night there.
26 Wataleta fahari na heshima ya mataifa ndani yake,
And they will bring the splendor and the worth of the nations into it.
27 na hakuna kichafu kitakachoingia ndani yake. Wala yeyote ambaye afanyaye jambo lolote la aibu au udanganyifu hataingia, bali ni wale tu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana Kondoo.
And there will, no, not enter into it anything profane, and doing an abomination and a lie, since they are not written in the Lamb's book of life.

< Ufunuo 21 >