< Ufunuo 19 >
1 Baada ya mambo haya nilisikia sauti kama ya mlio mkubwa wa kundi kubwa la watu mbinguni ikisema, “Haleluya. Wokovu, utukufu, na nguvu ni vya Mungu wetu.
Aftir these thingis Y herde as a greet vois of many trumpis in heuene, seiynge, Alleluya; heriynge, and glorie, and vertu is to oure God;
2 Hukumu zake ni kweli na za haki, kwa kuwa amemhukumu kahaba mkuu aliyeiharibu nchi kwa uzinzi wake. Amefanya kisasi kwa damu ya watumishi wake, ambayo aliimwaga yeye mwenyewe.”
for trewe and iust ben the domes of hym, whiche demede of the greet hoore, that defoulide the erthe in her letcherye, and vengide the blood of hise seruauntis, of the hondis of hir.
3 Kwa mara ya pili walisema, “Haleluya! Moshi hutoka kwake milele na milele.” (aiōn )
And eft thei seiden, Alleluya. And the smoke of it stieth vp, in to worldis of worldis. (aiōn )
4 Wale wazee ishirini na wanne na viumbe hai wanne wakasujudu na kumwabudu Mungu akaaye kwenye kiti cha enzi. Walikuwa wakisema, “Amina. Haleluya!”
And the foure and twenti senyouris and foure beestis felden doun, and worschipiden God sittynge on the trone, and seiden, Amen, Alleluya.
5 Ndipo sauti ilitoka kwenye kiti cha enzi, ikisema, “Msifuni Mungu wetu, enyi watumishi wake wote, ninyi mnaomcha yeye, wote wasio na umuhimu na wenye nguvu.”
And a vois wente out of the trone, and seide, Alle the seruauntis of oure God, seie ye heriyngus to oure God, and ye that dreden God, smale and grete.
6 Ndipo nilisikia sauti kama sauti ya kundi kubwa la watu, kama sauti ya ngurumo ya maji mengi, na kama ngurumo ya radi, ikisema, “Haleluya! Bwana ni Mungu wetu, mtawala juu ya wote, hutawala.
And Y herde a vois of a grete trumpe, as the vois of many watris, and as the vois of grete thundris, seiynge, Alleluya; for oure Lord God almyyti hath regned.
7 Na tushangilie na kufurahi na kumpa utukufu kwa sababu harusi na sherehe ya Mwana Kondoo imekuja, na bibi harusi yuko tayari.”
Ioye we, and make we myrthe, and yyue glorie to hym; for the weddingis of the lomb camen, and the wijf of hym made redy hir silf.
8 Aliruhusiwa kuvalishwa kitani safi na yenye kung'aa (kitani safi ni matendo ya haki ya waumini).
And it is youun to hir, that sche kyuere hir with white bissyn schynynge; for whi bissyn is iustifiyngis of seyntis.
9 Malaika akasema nami, “Yaandike haya: Wamebarikiwa walioalikwa kwenye sherehe ya harusi ya Mwana kondoo.” Vilevile akaniambia, “Haya ni maneno ya kweli ya Mungu.”
And he seide to me, Write thou, Blessid ben thei that ben clepid to the soper of weddyngis of the lomb. And he seide to me, These wordis of God ben trewe.
10 Nilisujudu mbele ya miguu yake nikamwabudu, lakini akaniambia, “Usifanye hivi! Mimi ni mtumishi mwenzako na wa ndugu zako mwenye kuushika ushuhuda wa Yesu. Mwabudu Mungu, kwa kuwa ushuhuda wa Yesu ni roho ya unabii.”
And Y felde doun bifore hise feet, to worschipe hym. And he seide to me, Se thou, that thou do not; Y am a seruaunt with thee, and of thi britheren, hauynge the witnessyng of Jhesu; worschipe thou God. For the witnessing of Jhesu is spirit of profesie.
11 Kisha niliona mbingu zimefunguka, na tazama kulikuwa na farasi mweupe! Na yule aliyekuwa amempanda anaitwa Mwaminifu na wa Kweli. Huhukumu kwa haki na kufanya vita.
And Y say heuene openyd, and lo! a whit hors, and he that sat on hym was clepid Feithful and sothefast; and with riytwisnesse he demeth, and fiytith.
12 Macho yake ni kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake ana taji nyingi. Ana jina lililoandikwa juu yake asilolifahamu mtu yeyote isipokuwa yeye mwenyewe.
And `the iyen of hym weren as flawme of fier, and in his heed many diademys; and he hadde a name writun, which no man knew, but he.
13 Amevaa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aliitwa Neno la Mungu.
And he was clothid in a cloth spreynt with blood; and the name of hym was clepid The sone of God.
14 Majeshi ya mbinguni yalikuwa yakimfuata juu ya farasi weupe, walivalishwa kitani nzuri, nyeupe na safi.
And the oostis that ben in heuene, sueden hym on white horsis, clothid with bissyn, white and clene.
15 Kinywani mwake hutoka upanga mkali ambao huyaangamiza mataifa, naye atawatawala kwa fimbo ya chuma. Naye hukanyaga vyombo vya mvinyo kwa hasira kali ya Mungu, hutawala juu ya wote.
And a swerd scharp on ech side cam forth of his mouth, that with it he smyte folkis; and he shal reule hem with an yren yerde. And he tredith the pressour of wyn of stronge veniaunce of the wraththe of almyyti God.
16 Naye ameandikwa juu ya vazi lake na katika paja lake jina, MFALME WA WAFALME NA BWANA WA MABWANA.
And he hath writun in his cloth, and in the hemme, Kyng of kyngis and Lord of lordis.
17 Niliona malaika amesimama katika jua. Aliwaita kwa sauti kuu ndege wote warukao juu, “Njoni, kusanyikeni pamoja kwenye chakula kikuu cha Mungu.
And Y say an aungel, stondynge in the sunne; and he criede with greet vois, and seide to alle briddis that flowen bi the myddil of heuene, Come ye, and be ye gaderid to the greet soper of God,
18 Njoni mle nyama ya wafalme, nyama ya majemedari, nyama ya watu wakubwa, nyama ya farasi na wapanda farasi, na nyama ya watu wote, walio huru na watumwa, wasio na umuhimu na wenye nguvu.”
that ye ete the fleisch of kingis, and fleisch of tribunes, and fleisch of stronge men, and fleisch of horsis, and of tho that sitten on hem, and the fleisch of alle fre men and bonde men, and of smale and of grete.
19 Nilimwona mnyama na wafalme wa nchi pamoja na majeshi yao. Walikuwa wamejipanga kwa ajili ya kufanya vita na mmoja aliyepanda farasi na jeshi lake.
And Y sai the beeste, and the kyngis of the erthe, and the oostis of hem gaderid, to make batel with hym, that sat on the hors, and with his oost.
20 Mnyama alikamatwa na nabii wake wa uongo aliyezifanya ishara katika uwepo wake. Kwa ishara hizi aliwadanganya wale walioipokea chapa ya mnyama na walioisujudia sanamu yake. Wote wawili walitupwa wangali hai katika ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti. (Limnē Pyr )
And the beeste was cauyt, and with hir the false prophete, that made signes bifor hir; in whiche he disseyuede hem that token the carect of the beeste, and that worschipiden the ymage of it. These tweyne weren sent quyke in to the pool of fier, brennynge with brymstoon. (Limnē Pyr )
21 Wale waliobaki waliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa mmoja aliyepanda juu ya farasi. Ndege wote walikula mizoga ya miili yao.
And the othere weren slayn of swerd of hym that sat on the hors, that cometh forth of the mouth of hym; and alle briddis weren fillid with the fleisch of hem.