< Ufunuo 19 >
1 Baada ya mambo haya nilisikia sauti kama ya mlio mkubwa wa kundi kubwa la watu mbinguni ikisema, “Haleluya. Wokovu, utukufu, na nguvu ni vya Mungu wetu.
And after yt I herde ye voyce of moche people in heven sayinge: Alleluia. Saluacion and glory and honour and power be ascribed to ye lorde oure god
2 Hukumu zake ni kweli na za haki, kwa kuwa amemhukumu kahaba mkuu aliyeiharibu nchi kwa uzinzi wake. Amefanya kisasi kwa damu ya watumishi wake, ambayo aliimwaga yeye mwenyewe.”
for true and ryghteous are his iudgmentes for he hath iudged ye grett whore which did corrupt the erth with her fornicacion and hath avenged the bloud of his servauntes of her hond.
3 Kwa mara ya pili walisema, “Haleluya! Moshi hutoka kwake milele na milele.” (aiōn )
And agayne they said: Alleluya. And smoke rose vp for evermore. (aiōn )
4 Wale wazee ishirini na wanne na viumbe hai wanne wakasujudu na kumwabudu Mungu akaaye kwenye kiti cha enzi. Walikuwa wakisema, “Amina. Haleluya!”
And the xxiiii. elders and the iiii. bestes fell doune and worshypped god that sate on the seate sayinge: Amen Alleluya.
5 Ndipo sauti ilitoka kwenye kiti cha enzi, ikisema, “Msifuni Mungu wetu, enyi watumishi wake wote, ninyi mnaomcha yeye, wote wasio na umuhimu na wenye nguvu.”
And a voyce cam out of the seate saying: prayse oure lorde god all ye that are his servauntes and ye that feare him both small and grett.
6 Ndipo nilisikia sauti kama sauti ya kundi kubwa la watu, kama sauti ya ngurumo ya maji mengi, na kama ngurumo ya radi, ikisema, “Haleluya! Bwana ni Mungu wetu, mtawala juu ya wote, hutawala.
And I herde the voyce of moche people eve as the voyce of many waters and as the voyce of stronge thondrynges sayinge: Alleluya for god omnipotent raigneth.
7 Na tushangilie na kufurahi na kumpa utukufu kwa sababu harusi na sherehe ya Mwana Kondoo imekuja, na bibi harusi yuko tayari.”
Let vs be glad and reioyce and geve honour to him: for the mariage of the lambe is come and hys wyffe made her sylfe reddy.
8 Aliruhusiwa kuvalishwa kitani safi na yenye kung'aa (kitani safi ni matendo ya haki ya waumini).
And to her was graunted that she shulde be arayed with pure and goodly raynes. For the raynes is the ryghtewesnes of saynctes.
9 Malaika akasema nami, “Yaandike haya: Wamebarikiwa walioalikwa kwenye sherehe ya harusi ya Mwana kondoo.” Vilevile akaniambia, “Haya ni maneno ya kweli ya Mungu.”
And he sayde vnto me: happy are they which are called vnto the Labes supper. And he sayde vnto me: these are the true sayinges of God.
10 Nilisujudu mbele ya miguu yake nikamwabudu, lakini akaniambia, “Usifanye hivi! Mimi ni mtumishi mwenzako na wa ndugu zako mwenye kuushika ushuhuda wa Yesu. Mwabudu Mungu, kwa kuwa ushuhuda wa Yesu ni roho ya unabii.”
And I fell at his fete to worshyppe him. And he sayde vnto me se thou do it not. For I am thy felowe seruaunt and one of thy brethern and of them that have the testimony of Iesus. Worshyppe God. For the testymony of Iesus ys the sprete of prophesy.
11 Kisha niliona mbingu zimefunguka, na tazama kulikuwa na farasi mweupe! Na yule aliyekuwa amempanda anaitwa Mwaminifu na wa Kweli. Huhukumu kwa haki na kufanya vita.
And I sawe heven open and beholde a whyte horsse: and he that sat apon him was faythfull and true and in ryghtewesnes dyd iudge and make battayle.
12 Macho yake ni kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake ana taji nyingi. Ana jina lililoandikwa juu yake asilolifahamu mtu yeyote isipokuwa yeye mwenyewe.
His eyes were as a flame of fyre: and on his heed were many crounes: and he had a name written yt noman knewe but him sylfe.
13 Amevaa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aliitwa Neno la Mungu.
And he was clothed with a vesture dipt in bloud and and hys name ys called the worde of God.
14 Majeshi ya mbinguni yalikuwa yakimfuata juu ya farasi weupe, walivalishwa kitani nzuri, nyeupe na safi.
And the warriers which were in heven folowed him apon whyte horsses clothed with whyte and pure raynes:
15 Kinywani mwake hutoka upanga mkali ambao huyaangamiza mataifa, naye atawatawala kwa fimbo ya chuma. Naye hukanyaga vyombo vya mvinyo kwa hasira kali ya Mungu, hutawala juu ya wote.
and out of his mouthe went out a sharppe swerde that with yt he shuld smyte the hethen. And he shall rule them with a rodde of yron and he trode the wynefatt of fearsnes and wrath of almyghty god.
16 Naye ameandikwa juu ya vazi lake na katika paja lake jina, MFALME WA WAFALME NA BWANA WA MABWANA.
And hath on his vesture and on his thygh a name written: kynge of kynges and lorde of lordes.
17 Niliona malaika amesimama katika jua. Aliwaita kwa sauti kuu ndege wote warukao juu, “Njoni, kusanyikeni pamoja kwenye chakula kikuu cha Mungu.
And I sawe an angell stonde in the sunne and he cryed with a lowde voyce sayinge to all the fowles that flye by ye myddes of heve come and gaddre youre selves to gedder vnto the supper of the gret god
18 Njoni mle nyama ya wafalme, nyama ya majemedari, nyama ya watu wakubwa, nyama ya farasi na wapanda farasi, na nyama ya watu wote, walio huru na watumwa, wasio na umuhimu na wenye nguvu.”
that ye maye eate the flesshe of kynges and of hye captaynes and the flesshe of myghty men and the flesshe of horsses and of them that sytt on them and the flesshe of all free men and bond men and of small and gret.
19 Nilimwona mnyama na wafalme wa nchi pamoja na majeshi yao. Walikuwa wamejipanga kwa ajili ya kufanya vita na mmoja aliyepanda farasi na jeshi lake.
And I sawe the beste and the kynges of the erth and their warriers gaddred to gedder to make battayle agaynste him that satt on the horsse and agaynst his sowdiers.
20 Mnyama alikamatwa na nabii wake wa uongo aliyezifanya ishara katika uwepo wake. Kwa ishara hizi aliwadanganya wale walioipokea chapa ya mnyama na walioisujudia sanamu yake. Wote wawili walitupwa wangali hai katika ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti. (Limnē Pyr )
And the beste was take and with him that falce prophett that wrought myracles before him with which he desceaved the that receaved ye beestes marke and them that worshipped his ymage. These both were cast into a pode of fyre burnyge with brymstone: (Limnē Pyr )
21 Wale waliobaki waliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa mmoja aliyepanda juu ya farasi. Ndege wote walikula mizoga ya miili yao.
and ye remnaunte were slayne with ye swearde of him that sat apon the horsse which swearde proceded out of his mouthe and all the foules were fulfilled with their flesshe.