< Ufunuo 18 >

1 Baada ya vitu hivi nilimwona malaika mwingine akishuka chini kutoka mbinguni. Yeye alikuwa na mamlaka kuu, na nchi iliangazwa kwa utukufu wake.
After these things I saw another angel coming down out of heaven. He had great authority, and the earth was illumined by his glory.
2 Alilia kwa sauti kuu, akisema, “Umeanguka, umeanguka, ule mji mkuu Babeli! Umekuwa sehemu yakaapo mapepo, na sehemu ikaapo kila roho chafu, na sehemu akaapo kila mchafu na ndege achukizaye.
He cried out with a mighty voice, saying, “Fallen, fallen is Babylon the great! She has become a dwelling place for demons, a refuge for every unclean spirit, and a refuge for every unclean and detestable bird.
3 Kwa kuwa mataifa yote yamekunywa mvinyo ya tamaa ya uasherati wake ambayo humletea ghadhabu. Wafalme wa nchi wamezini naye. Wafanyabiashara wa nchi wamekuwa matajiri kwa nguvu ya maisha yake ya anasa.”
For all the nations have drunk the wine of her immoral passion. The kings of the earth have committed immorality with her. The merchants of the earth have become rich from the power of her sensual way of living.”
4 Kisha nilisikia sauti nyingine kutoka mbinguni iikisema, “Tokeni kwake watu wangu, ili msije mkashiriki katika dhambi zake, na ili msije mkapokea mapigo yake yoyote.
Then I heard another voice from heaven say, “Come out from her, my people, so that you will not share in her sins, and so that you will not receive any of her plagues.
5 Dhambi zake zimerundikana juu kama mbingu, na Mungu ameyakumbuka matendo yake maovu.
Her sins have piled up as high as heaven, and God has remembered her evil actions.
6 Mlipeni kama alivyowalipa wengine, na mkamlipe mara mbili kwa jinsi alivyotenda; katika kikombe alichokichanganya, mchanganyishieni mara mbili kwa ajili yake.
Pay her back as she has paid others back, and repay her double for what she has done; in the cup she mixed, mix double the amount for her.
7 Kama alivyojitukuza yeye mwenyewe, na aliishi kwa anasa, mpeni mateso mengi na huzuni. Kwa kuwa husema moyoni mwake, 'Nimekaa kama malkia; wala siyo mjane, na wala sitaona maombolezo.'
As she glorified herself and lived in luxury, give her just as much torture and grief. For she says in her heart, 'I am seated as a queen; I am not a widow, and I will never see mourning.'
8 Kwa hiyo ndani ya siku moja mapigo yake yatamlemea: kifo, maombolezo, na njaa. Atateketezwa kwa moto, kwa kuwa Bwana Mungu ni mwenye nguvu, na ni mhukumu wake.”
Therefore in one day her plagues will come: death, mourning, and famine. She will be consumed by fire, for the Lord God is mighty, and he is her judge.”
9 Wafalme wa nchi waliozini na kuchanganyikiwa pamoja naye watalia na kumwombolezea watakapouona moshi wa kuungua kwake.
The kings of the earth who committed sexual immorality and went out of control with her will weep and wail over her when they see the smoke of her burning.
10 Watasimama mbali naye, kwa hofu ya maumivu yake wakisema, “Ole, ole kwa mji mkuu, Babeli, mji wenye nguvu! Kwa saa moja hukumu yako imekuja.”
They will stand off at a distance, afraid of her torment, saying, “Woe, woe to the great city, Babylon, the powerful city! For in a single hour your punishment has come.”
11 Wafanyabiashara wa nchi lieni na kuomboleza kwa ajili yake, kwa kuwa hakuna hata mmoja anunuaye bidhaa zake tena -
The merchants of the earth weep and mourn for her, since no one buys her merchandise anymore—
12 bidhaa za dhahabu, fedha, mawe ya thamani, lulu, kitani nzuri, zambarau, hariri, nyekundu, aina zote za miti ya harufu nzuri, kila chombo cha pembe za ndovu, kila chombo kilichotengenezwa kwa miti ya thamani, shaba, chuma, jiwe,
merchandise of gold, silver, precious stone, pearls, fine linen, purple, silk, scarlet, all kinds of scented wood, every vessel of ivory, every vessel made of most precious wood, bronze, iron, marble,
13 mdalasini, viungo, uvumba, manemane, ubani, mvinyo, mafuta, unga mzuri, ngano, ng'ombe na kondoo, farasi na magari, na watumwa, na roho za watu.
cinnamon, spice, incense, myrrh, frankincense, wine, oil, fine flour, wheat, cattle and sheep, horses and chariots, and slaves and human souls.
14 Matunda uliyoyatamani kwa nguvu zako yameondoka kutoka kwako. Anasa zako zote na mapambo yametoweka, hayatapatikana tena.
The fruit that you longed for with all your might is gone from you. All your luxury and splendor have vanished, never to be found again.
15 Wafanyabiashara wa vitu hivi waliopata utajiri kwa mapenzi yake watasimama mbali kutoka kwake kwa sababu ya hofu ya maumivu yake, wakilia na sauti ya maombolezo.
The merchants of these goods who became rich by her will stand away from her at a distance because of the fear of her torment, weeping and mourning loudly.
16 Wakisema, “Ole, ole mji ule mkuu uliovikwa kitani nzuri, zambarau, na nyekundu, na kupambwa kwa dhahabu, na vito vya thamani na lulu!”
They will say, “Woe, woe to the great city that was dressed in fine linen, in purple, and in scarlet, and was adorned with gold, precious jewels, and pearls!
17 Ndani ya saa moja utajiri wote huo ulitoweka. Kila nahodha wa meli, kila baharia, na wote wanamaji, na wote wafanyao kazi baharini, walisimama mbali.
In a single hour all that wealth has been wasted.” Every ship's captain, every seafaring man, sailors, and all whose living is made from the sea, stood off at a distance.
18 Walilia walipouona moshi wa kuungua kwake. Walisema, “Ni mji gani unafanana na mji huu mkubwa?”
They cried out as they saw the smoke of her burning. They said, “What city is like the great city?”
19 Walitupa mavumbi juu ya vichwa vyao, na walilia, wakitokwa machozi na kuomboleza, “Ole, ole mji mkubwa mahali wote waliokuwa na meli zao baharini walikuwa matajiri kutokana na mali zake. Ndani ya saa moja umeangamizwa.”
They threw dust on their heads, and cried out, weeping and mourning, “Woe, woe to the great city where all who had their ships at sea became rich from her wealth. For in a single hour she has been destroyed.”
20 “Furahini juu yake, mbingu, ninyi waumini, mitume, na manabii, kwa maana Mungu ameleta hukumu yenu juu yake!”
“Rejoice over her, heaven, you believers, apostles, and prophets, for God has brought your judgment on her!”
21 Malaika mwenye nguvu aliinua jiwe kama jiwe kuu la kusagia na alilitupa baharini, akisema, “Kwa njia hii, Babeli, ule mji mkuu, utatupwa chini kwa ukatili na hautaonekana tena.
A mighty angel took up a stone like a great millstone and threw it into the sea, saying, “In this way, Babylon, the great city, will be thrown down with violence and will not be seen anymore.
22 Sauti ya vinanda, wanamuziki, wacheza filimbi, na tarumbeta hawatasikika tena kwenu. Wala fundi wa aina yoyote hataonekana kwenu. Wala sauti ya kinu haitasikika tena kwenu.
The sound made by harpists, musicians, flute players, and trumpeters will not be heard anymore in you. No craftsman of any kind will be found in you. No sound of a mill will be heard anymore in you.
23 Mwanga wa taa hautaangaza ndani yako. Sauti ya bwana harusi na bibi harusi hazitasikiwa tena ndani yako, maana wafanyabiashara wako walikuwa wakuu wa nchi, na wa mataifa, wamedanganywa kwa uchawi wako.
The light of a lamp will not shine in you anymore. The voices of the bridegroom and the bride will not be heard in you anymore, for your merchants were the princes of the earth, and the nations were deceived by your sorcery.
24 Ndani yake damu ya manabii na waamini ilionekana, na damu ya wote waliouawa juu ya nchi.”
In her the blood of prophets and saints was found, and the blood of all who have been killed on the earth.”

< Ufunuo 18 >