< Ufunuo 16 >
1 Nikasikia sauti kubwa ikiita kutoka kwenye sehemu ya patakatifu na ikasema kwa wale malaika saba, “Nenda na ukamwage juu ya dunia mabakuli saba ya ghadhabu ya Mungu.”
Then I heard a loud voice which came out of the temple, saying to the seven angels, "Go, empty the seven bowls of the wrath of God upon the earth."
2 Malaika wa kwanza alienda na kumwaga bakuli lake katika dunia; majeraha mabaya na yenye maumivu makali yalikuja kwa watu wenye alama ya mnyama, kwa wale ambao waliabudu sanamu yake.
The first angel went and poured out his bowl upon the earth. And it was turned to loathsome and painful sores upon all who bore the brand of the beast, and who worshiped his image.
3 Malaika wa pili alimwaga bakuli lake katika bahari; ikawa kama damu ya mtu aliyekufa, na kila kiumbe hai katika bahari kilikufa.
And the second angel poured out his bowl upon the sea; and it became blood, like the blood of a corpse, and every living creature died - everything in the sea.
4 Malaika wa tatu akamwaga bakuli lake katika mito na katika chemichemi za maji; zikawa damu.
And the third poured out his bowl into the rivers and springs of waters; and they were turned into blood.
5 Nikasikia malaika wa maji akisema, “Wewe ni mwaminifu - mmoja uliyepo na uliyekuwako, Mtakatifu - kwa sababu umezileta hukumu hizi.
And I heard the angel of the waters saying. "Righteous art thou, thou who art and wast, The Holy One, Because thou didst inflict this judgment.
6 Kwa sababu walimwaga damu za waamini na manabii, umewapa wao kunywa damu; ndicho wanachostahili.”
For men poured out the blood of thy saints and prophets, And thou hast given them blood to drink. And this they deserved."
7 Nikasikia madhabahu ikijibu, “Ndiyo! Bwana Mungu mwenye kutawala juu ya vyote, hukumu zako ni kweli na za haki.”
And I heard the altar saying, "Yea, O Lord, the Almighty, True and righteous are thy judgments."
8 Malaika wa nne akamwaga kutoka kwenye bakuli lake juu ya jua, na likapewa ruhusa kuunguza watu kwa moto.
And the fourth angel poured out his bowl upon the sun, and the sun was permitted to scorch men with fire.
9 Waliunguzwa kwa joto lenye kutisha, na wakalikufuru neno la Mungu, mwenye nguvu juu ya mapigo yote. Hawakutubu wala kumpa yeye utukufu.
And men were scorched with the terrible heat; and they blasphemed the name of the God who had the power over these plagues; yet they repented not, to give him glory.
10 Malaika wa tano akamwaga kutoka kwenye bakuli lake katika kiti cha enzi cha mnyama, na giza likaufunika ufalme wake. Walisaga meno katika maumivu makali.
And the fifth poured out his bowl upon the throne of the beast; and his kingdom became darkened, and men gnawed their tongues for pain,
11 Wakamtukana Mungu wa mbinguni kwa sababu ya maumivu yao na majeraha yao, na bado waliendelea kutokutubu kwa kile walichotenda.
and they blasphemed the God of heaven, because of their pains and their sores; yet of their deeds they did not repent.
12 Malaika wa sita alimwaga kutoka kwenye bakuli lake katika mto mkubwa, Frati, na maji yake yakakauka ili kuweza kuandaa njia kwa wafalme watakaokuja kutoka mashariki.
And the sixth poured his bowl upon the great river, the River Euphrates, and its water was dried up so as to make ready the way for the kings that come from the sunrising.
13 Nikaona roho tatu chafu zilizoonekana kama chura watokao nje ya mdomo wa yule joka, yule mnyama, na yule nabii wa uongo.
And I saw three unclean spirits, like frogs, coming out of the dragon’s mouth, and the beast’s mouth, and the false prophet’s mouth.
14 Ni roho za pepo zitendazo ishara na miujiza. Walikuwa wakienda kwa wafalme wa dunia yote ili kuweza kuwakusanya pamoja kwa vita katika siku kuu ya Mungu, mwenye kutawala juu ya vyote.
For these are the spirits of demons performing miracles, who go forth to the kings of the habitable earth, to gather them together for the battle of the great Day of God, the Almighty.
15 (“Tazama! Ninakuja kama mwizi! Heri yule adumuye katika kukesha, atunzaye mavazi yake ili asiweze kwenda nje uchi na kuiona aibu yake.”)
Lo, I am coming like a thief. Blessed is the who is on the watch and guarding his clothing, so that he may not walk naked, and they gaze on his shame.
16 Waliwaleta pamoja katika sehemu iliyoitwa katika kiebrania Amagedoni.
And the spirits gathered the kings together at the place called in Hebrew, Armageddon.
17 Malaika wa saba alimwaga kutoka kwenye bakuli lake katika anga. Kisha sauti kuu ikasikika kutoka pakatifu na kutoka kwenye kiti cha enzi, ikisema, “Imekwisha!”
And the seventh poured out his bowl upon the air, and a great voice came forth out of the temple from the throne, saying, "It is finished!"
18 Kulikuwa na miale ya mwanga wa radi, ngurumo, vishindo vya radi, na tetemeko la kutisha - tetemeko kubwa la ardhi ambalo halijawahi kutokea duniani tangu wanadamu wamekuwepo duniani, hivyo ni tetemeko kubwa zaidi.
And lightnings and voices and thunders and a great earthquake such as had not happened since man began to be upon the earth, so great an earthquake, so mighty;
19 Mji mkuu uligawanyika katika sehemu tatu, na miji ya mataifa ikaanguka. Kisha Mungu akamkumbusha Babeli mkuu, na akaupa mji huo kikombe kilichokuwa kimejaa divai kutoka kwenye ghadhabu yake iliyo kali.
and the great city was shattered into three parts, and the cities of the nations fell, and great Babylon came to mind before the face of God, to give her the cup of the wine of the passion of his anger.
20 Kila kisiwa kikapotea na milima haikuonekana tena.
And every island fled away, and the mountains sank from sight.
21 Mvua kubwa ya mawe, ikiwa na uzito wa talanta, ikashuka kutoka mbinguni juu ya watu, na wakamlaani Mungu kwa mapigo ya mvua ya mawe kwa sababu lile pigo lilikuwa baya sana.
And there fell upon men a great hail out of heaven, every stone about the weight of a talent; and men blasphemed God because of the plague of the hail, for the plague of it is very great.