< Ufunuo 14 >

1 Nilitazama na nikaona Mwana Kondoo amesimama mbele yangu juu ya Mlima Sayuni. Pamoja naye walikuwa 144, 000 wenye jina lake na jina la Baba yake limeandikwa katika vipaji vya nyuso zao.
And I looked, and lo, there was the Lamb standing on Mount Zion, and with were a hundred and forty and four thousand who had his name and his Father’s name written on their foreheads.
2 Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisikika kama ngurumo za maji mengi na sauti kubwa ya radi. Sauti niliyoisikia ni kama wapiga vinubi wapigao vinubi vyao.
And I heard a voice from heaven like the voice of many waters, and the voice of a great thunder; and I heard the voice of harpers harping on their harps.
3 Wakiimba wimbo mpya mbele za kiti cha enzi na mbele za wenye uhai wanne na wazee. Hakuna hata mwenye uwezo wa kujifunza huo wimbo isipokuwa kwa 144, 000 ambao wamekombolewa kutoka duniani.
They were singing a new song before the throne, and before the four Living Creatures and the Elders; and none can learn that song, except the one hundred and forty and four thousand, who had been redeemed from the earth.
4 Hawa ni wale ambao hawakujichafua wenyewe kwa wanawake, maana walijitunza wenyewe dhidi ya matendo ya zinaa. Ni hawa ambao walimfuata Mwana Kondoo popote alipoenda. Hawa walikombolewa kutoka kwa wanadamu wakiwa matunda ya kwanza kwa Mungu na kwa Mwana Kondoo.
These are they who were not defiled with women; for they are celibates. They follow the Lamb wherever he goes. They have been redeemed from among men to be the first-fruits unto God and the Lamb.
5 Hakuna uongo uliopatikana katika vinywa vyao; hawalaumiwi.
No lie was ever found on their lips; they are spotless.
6 Nikaona malaika mwingine akiruka katikati ya mbingu, ambaye mwenye ujumbe wa mbinguni wa habari njema kwa kuwatangazia wenye kuishi duniani kwa kila taifa, kabila, lugha, na watu. (aiōnios g166)
Then I saw another angel who was flying in mid-heaven. He had an eternal evangel, to evangelize all the dwellers on the earth, of every nation and tribe and tongue and people. (aiōnios g166)
7 Akawaita kwa sauti kuu, “Mwogopeni Mungu na mpeni utukufu. Kwa maana muda wa hukumu umekaribia. Mwabuduni yeye, yeye aliyeumba mbingu, na dunia, na bahari, na chemchemi za maji.”
And he cried with a loud voice. "Fear God and give him glory, Because the hour of his judgment is come. And worship Him who made the heavens and the earth And the sea and springs of waters."
8 Malaika mwingine - malaika wa pili - akafuata akisema, “Umeanguka, umeanguka Babeli mkuu, ambaye uliwanywesha mataifa divai ya ukahaba, divai ambayo ilileta ghadhabu juu yake.”
Then a second angel followed, crying, "Fallen, fallen is Babylon the Great, Who has made all the nations drink the wine Of the frenzy of her fornication."
9 Malaika mwingine - malaika wa tatu - aliwafuata, akasema kwa sauti kuu, “Yeyote atakayemwabudu huyo mnyama na sanamu yake, na kupokea alama katika paji lake la uso au mkononi,
And another angel, a third, followed them, crying with a mighty voice. "Whoever worships the beast and his image, And receives a brand on his forehead or on his hand,
10 yeye pia atakunywa divai ya ghadhabu ya Mungu, divai ambayo imeandaliwa na kumwagwa bila kuchanganywa katika kikombe cha hasira yake. Mtu atakayekunywa atateswa kwa moto na moto wa kiberiti mbele za malaika zake watakatifu na mbele za Mwana Kondoo.
He also shall drink of the wine of the wrath of God, Poured out unmixed in the cup of his anger; And he shall be tormented with fire and brimstone In the presence of the holy angels, And in the presence of the Lamb,
11 Na moshi wa maumivu yao ukaenda milele na milele, na hawakuwa na mapumziko mchana au usiku - hao waabuduo mnyama na sanamu yake, na kila mtu aliyepokea alama ya jina lake. (aiōn g165)
And the smoke of their torment ascends forever and ever; And they have no rest day or night, Who worship the beast and his image, And all who receive the brand of his name." (aiōn g165)
12 Huu ni wito wa subira na uvumilivu kwa waamini, wale ambao hutii amri za Mungu na imani katika Yesu.”
Here is the endurance of the saints, those who keep the commandments of God, and the faith of Jesus.
13 Nilisikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika haya: Heri wafu wafao katika Bwana.” “Ndiyo,” asema Roho, “ili waweze kupumzika kutoka kwenye kazi zao, maana matendo yao yatawafuata.”
And I heard a voice from heaven, saying, "Write, Blessed are the dead that die in the Lord from henceforth! Yea, says the Spirit, that they may rest from their labors, For their deeds do follow them."
14 Nilitazama na nikaona kulikuwa na wingu jeupe, na aliyeketi kwenye wingu ni mmoja aliyekuwa na mfano wa Mwana wa Mtu. Alikuwa na taji ya dhahabu katika kichwa chake na mundu mkali katika mkono wake.
And I looked, and lo, a white cloud; and on the cloud I saw One sitting like to a son of man, with a golden crown on his head, and a sharp sickle in his hand.
15 Malaika mwingine tena alikuja kutoka kwenye hekalu na aliita kwa sauti kuu kwenda kwa yule aliyekaa katika wingu: “Chukua mundu wako na uanze kuvuna. Kwa kuwa muda wa mavuno umeshawadia, maana mavuno yaliyo katika dunia yameshaiva.”
And another angel came out of the temple, shouting with a loud voice to him who sat on the cloud. "Thrust in your sickle, and reap; for the time to reap is come. The harvest of the earth is overripe."
16 Tena yule aliyekuwa kwenye wingu aliupitisha mundu wake juu ya dunia, na dunia ikavunwa.
And he who sat on the cloud thrust in his sickle upon the earth; and the earth was reaped.
17 Na malaika mwingine akaja kutoka kwenye hekalu la mbinguni; naye alikuwa na mundu mkali.
And another angel came out of the temple which is in heaven, and he, too, had a sharp sickle.
18 Na bado malaika mwingine akaja kutoka kwenye madhabahu, na malaika aliyekuwa na mamlaka juu ya moto. Akamwita kwa sauti kuu malaika ambaye alikuwa na mundu mkali, “Chukua mundu mkali na uyakusanye matawi ya mzabibu kutoka kwenye mzabibu wa nchi, kwa kuwa zabibu sasa zimeiva.”
And another angel came from the altar, the angel who has power over fire, and he called with a loud voice to the one who had the sharp sickle, saying, "Thrust in your sharp sickle, And gather the clusters of the vine of the earth, For its grapes are fully ripe."
19 Malaika alipeleka mundu wake katika dunia na alikusanya mavuno ya zabibu ya dunia na alirusha katika pipa kubwa la divai ya ghadhabu ya Mungu.
So the angel thrust his sickle into the earth and gathered the clusters of the vine of the earth, and threw them into the winepress, the great winepress of the wrath of God.
20 Chujio la divai lilipondwapondwa nje ya mji na damu ikamwagika kutoka katika hicho kimo cha hatamu ya farasi, kwa stadia 1, 600.
And the winepress was trodden outside the city, and blood gushed out of the winepress, even to the bridles of the horses, as far as two hundred miles.

< Ufunuo 14 >