< Ufunuo 13 >

1 Kisha joka alisimama juu ya mchanga ufukwe wa bahari. Kisha nikaona mnyama akitoka kwenye bahari. Alikuwa na pembe kumi na vichwa saba. Katika pembe zake kulikuwa na taji kumi, na katika kichwa chake kulikuwa na maneno ya kufuru kwa Mungu.
And I saw, out of the sea, a wild-beast coming up; having ten horns, and seven heads, and, upon his horns, ten diadems, and, upon his head, names of blasphemy.
2 Huyu mnyama niliyemuona ni kama chui. Miguu yake ilikuwa kama ya dubu, na mdomo wake ulikuwa kama wa simba. Yule joka akampa nguvu, na katika kiti chake cha enzi, na mamlaka yenye nguvu sana ya kutawala.
And, the beast which I saw, was like unto a leopard; and, his feet, as of a bear, and, his mouth, as the mouth of a lion. And the dragon gave unto him his power, and his throne, and great authority.
3 Kichwa cha mnyama mmojawapo kilionekana kuwa na jeraha kubwa ambalo lingesababisha mauti yake. Lakini jeraha lake likapona, na dunia yote ikashangazwa na ikamfuata mnyama.
And [I saw] one of his heads, showing that it had been slain unto death, and, the stroke of his death, was healed. And the whole earth marveled after the wild-beast,
4 Pia wakamwabudu joka, maana alimpa mamlaka yule mnyama. Wakamwabudu mnyama pia, na wakaendelea kusema, “Nani kama mnyama? na “Nani atapigana naye?”
and did homage unto the dragon, because he gave his authority unto the wild-beast; and they did homage unto the wild-beast, saying—Who is like unto the wild-beast? and Who can make war with him?
5 Mnyama akapewa mdomo ili azungumze maneno ya kujisifu na matusi. Aliruhusiwa kuwa na mamlaka kwa miezi arobaini na miwili.
And there was given unto him, a mouth speaking great things and blasphemies; and it was given unto him to act, forty and two months.
6 Hivyo mnyama alifungua mdomo wake kuongea matusi dhidi ya Mungu, akalitukana jina lake, eneo alililokuwa akiishi na wale wanaoishi mbinguni.
And he opened his mouth for blasphemy against God, to blaspheme his name, and his tent, —them, who, in heaven were tabernacling.
7 Mnyama aliruhusiwa kufanya vita na waamini na kuwashinda. Pia, alipewa mamlaka juu ya kila kabila, watu, lugha na taifa.
[And it was given unto him, to make war with the saints, and to overcome them; ] and there was given him, authority against every tribe and people and tongue and nation.
8 Wote walioishi duniani watamwabudu yeye, kila mmoja ambaye jina lake halijaandikwa, toka uumbaji wa dunia, katika kitabu cha uzima, ambacho ni cha Mwana Kondoo, ambaye alichinjwa.
And all they who are dwelling upon the earth will do homage unto him, —[every one] whose name is not written in the scroll of life of the Lamb slain from the foundation of the world.
9 Ikiwa yeyote ana sikio, na asikilize.
If anyone hath an ear: let him hear.
10 Ikiwa mmojawapo amechukuliwa mateka, na kwenye mateka ataenda. Ikiwa mmojawapo ataua kwa upanga, kwa upanga atauawa. Huu ni mwito wa utulivu na uvumilivu na imani kwa hao walio watakatifu.
If anyone [carrieth] into captivity, into captivity, he goeth away. If anyone, with a sword, doth slay, he must, with a sword, be slain. Here, is the endurance and the faith of the saints.
11 Tena nikaona mnyama mwingine anakuja kutoka katika nchi. Alikuwa mwenye pembe mbili kama kondoo na akazungumza kama joka.
And I saw another wild-beast, coming up out of the earth; and he had two horns, like unto a lamb, and began speaking as a dragon.
12 Alionyesha mamlaka yote katika mnyama yule wa kwanza katika uwepo wake, na kufanya katika dunia na wale walioishi wakimuabudu yule mnyama wa kwanza, yule ambaye jeraha lake limepona.
And, all the authority of the first wild-beast, he useth before him; and causeth the earth, and them who, therein, are dwelling, that they shall do homage unto the first wild-beast, whose stroke of death, was healed.
13 Akafanya miujiza yenye nguvu, hata akafanya moto ushuke katika dunia kutoka mbinguni mbele ya watu,
And he doeth great signs, so that, even fire, he causeth to be coming down unto the earth before men;
14 na kwa ishara aliruhusiwa kufanya, akawadanganya hao wakaao katika dunia, akiwaambia kutengeneza sanamu kwa heshima ya mnyama ambaye alikuwa amejeruhiwa kwa upanga, lakini bado aliishi.
and he deceiveth them who are dwelling upon the earth, by reason of the signs which it was given him to do before the wild-beast, —saying unto them who are dwelling upon the earth, that they should make an image unto the wild-beast who hath the stroke of the sword, and yet did live.
15 Aliruhusiwa kutoa pumzi katika ile sanamu ya mnyama ili sanamu iweze kusema na kusababisha wale wote waliokataa kumwabudu mnyama wauawe.
And it was given unto it, to give spirit unto the image of the wild-beast, in order that the image of the wild-beast should both speak and should cause that, as many as should not do homage unto the image of the wild-beast, should be slain.
16 Pia akalazimisha kila mmoja, asiye na thamani na mwenye nguvu, tajiri na maskini, huru na mtumwa, kupokea alama katika mkono wa kuume au katika paji la uso.
And he causeth all—the small and the great, and the rich and the poor, and the free and the bond, —that they should give unto them a mark, upon their right hand or upon their forehead;
17 Ilikuwa haiwezekani kwa kila mtu kuuza au kununua isipokuwa mwenye alama ya mnyama, na hii ni namba yenye kuwakilisha jina lake.
[and] that no one should be able to buy or to sell, save he that hath the mark, the name of the beast, or the number of his name.
18 Hii inahitaji busara. Ikiwa yeyote ana ufahamu, mwache aweze kufanya hesabu ya namba ya mnyama. Maana ni namba ya kibinadamu. Namba yake ni 666.
Here, is, wisdom: he that hath understanding, let him count the number of the beast, for it is, the number of a man; and, his number, is 666.

< Ufunuo 13 >