< Ufunuo 13 >
1 Kisha joka alisimama juu ya mchanga ufukwe wa bahari. Kisha nikaona mnyama akitoka kwenye bahari. Alikuwa na pembe kumi na vichwa saba. Katika pembe zake kulikuwa na taji kumi, na katika kichwa chake kulikuwa na maneno ya kufuru kwa Mungu.
Now I was standing on the seashore, and I saw a Beast of prey coming up out of the sea, having seven heads and ten horns, and on his horns ten diadems and on his heads blasphemous names.
2 Huyu mnyama niliyemuona ni kama chui. Miguu yake ilikuwa kama ya dubu, na mdomo wake ulikuwa kama wa simba. Yule joka akampa nguvu, na katika kiti chake cha enzi, na mamlaka yenye nguvu sana ya kutawala.
The beast that I saw was similar to a leopard, his feet were like those of a bear, and his mouth was like a lion's mouth. And the dragon gave him his power and his throne and great authority.
3 Kichwa cha mnyama mmojawapo kilionekana kuwa na jeraha kubwa ambalo lingesababisha mauti yake. Lakini jeraha lake likapona, na dunia yote ikashangazwa na ikamfuata mnyama.
And one of his heads was as if it had been mortally wounded, but his fatal wound was healed. And the whole earth marveled after the Beast.
4 Pia wakamwabudu joka, maana alimpa mamlaka yule mnyama. Wakamwabudu mnyama pia, na wakaendelea kusema, “Nani kama mnyama? na “Nani atapigana naye?”
And they did obeisance to the dragon who had given the authority to the Beast, and they did obeisance to the Beast saying, “Who is like the Beast, and who is able to make war with him?”
5 Mnyama akapewa mdomo ili azungumze maneno ya kujisifu na matusi. Aliruhusiwa kuwa na mamlaka kwa miezi arobaini na miwili.
And he was given a mouth speaking great things, that is, blasphemy; and he was given authority to make war forty-two months.
6 Hivyo mnyama alifungua mdomo wake kuongea matusi dhidi ya Mungu, akalitukana jina lake, eneo alililokuwa akiishi na wale wanaoishi mbinguni.
So he opened that mouth of his in blasphemy against God, to blaspheme His name and His tabernacle, those who dwell in Heaven.
7 Mnyama aliruhusiwa kufanya vita na waamini na kuwashinda. Pia, alipewa mamlaka juu ya kila kabila, watu, lugha na taifa.
And it was given to him to make war with the saints and to conquer them. And authority was given him over every tribe and language and ethnic nation.
8 Wote walioishi duniani watamwabudu yeye, kila mmoja ambaye jina lake halijaandikwa, toka uumbaji wa dunia, katika kitabu cha uzima, ambacho ni cha Mwana Kondoo, ambaye alichinjwa.
All who dwell on the earth will do obeisance to him, whose names have not been written in the Book of Life of the Lamb slaughtered from the foundation of the world.
9 Ikiwa yeyote ana sikio, na asikilize.
If anyone has an ear, let him hear.
10 Ikiwa mmojawapo amechukuliwa mateka, na kwenye mateka ataenda. Ikiwa mmojawapo ataua kwa upanga, kwa upanga atauawa. Huu ni mwito wa utulivu na uvumilivu na imani kwa hao walio watakatifu.
If anyone has captivity, he goes away. If anyone kills with the sword, with the sword he must be killed. Here is the endurance and the faith of the saints.
11 Tena nikaona mnyama mwingine anakuja kutoka katika nchi. Alikuwa mwenye pembe mbili kama kondoo na akazungumza kama joka.
Now I saw another beast of prey coming up out of the land, and he had two horns like a lamb and spoke like a dragon.
12 Alionyesha mamlaka yote katika mnyama yule wa kwanza katika uwepo wake, na kufanya katika dunia na wale walioishi wakimuabudu yule mnyama wa kwanza, yule ambaye jeraha lake limepona.
And he exercises all the authority of the first Beast in his presence; and he started to cause the earth and those who dwell in it to worship the first Beast, whose mortal wound was healed.
13 Akafanya miujiza yenye nguvu, hata akafanya moto ushuke katika dunia kutoka mbinguni mbele ya watu,
And he performs great signs, including that fire should come down from heaven upon the earth before the people.
14 na kwa ishara aliruhusiwa kufanya, akawadanganya hao wakaao katika dunia, akiwaambia kutengeneza sanamu kwa heshima ya mnyama ambaye alikuwa amejeruhiwa kwa upanga, lakini bado aliishi.
And he deceives my own people, those dwelling on the earth, by the signs that it was given to him to perform before the Beast, telling those who dwell on the earth to make an image to the Beast who had the sword wound and lived.
15 Aliruhusiwa kutoa pumzi katika ile sanamu ya mnyama ili sanamu iweze kusema na kusababisha wale wote waliokataa kumwabudu mnyama wauawe.
And it was granted to him to give breath to the image of the Beast, so that the image of the Beast should actually speak, and should cause as many as would not worship the image of the Beast to be killed.
16 Pia akalazimisha kila mmoja, asiye na thamani na mwenye nguvu, tajiri na maskini, huru na mtumwa, kupokea alama katika mkono wa kuume au katika paji la uso.
And he causes everyone—both small and great, both rich and poor, both free and slave—to receive marks on their right hand or on their foreheads,
17 Ilikuwa haiwezekani kwa kila mtu kuuza au kununua isipokuwa mwenye alama ya mnyama, na hii ni namba yenye kuwakilisha jina lake.
so that no one would be able to buy or sell who does not have the mark, the name of the Beast or the number of his name.
18 Hii inahitaji busara. Ikiwa yeyote ana ufahamu, mwache aweze kufanya hesabu ya namba ya mnyama. Maana ni namba ya kibinadamu. Namba yake ni 666.
Here is wisdom: let the one who has understanding evaluate the number of the Beast, for it is the number of man—his number is 666.