< Ufunuo 12 >

1 Ishara kuu ilionekana mbinguni: mwanamke aliyefunikwa na jua, na akiwa na mwezi chini ya miguu yake; na taji ya nyota kumi na mbili ilikuwa juu ya kichwa chake.
Et il parut dans le ciel un grand prodige, une femme enveloppée de la lumière du soleil, ayant la lune sous ses pieds, et sur sa tête une couronne de douze étoiles.
2 Alikuwa na mimba na alikuwa analia kwa ajili ya maumivu ya kuzaa—katika uchungu wa kujifungua.
Elle était enceinte, et elle criait, parce qu'elle était dans le travail et les douleurs de l'enfantement.
3 Na ishara nyingine ilionekana mbinguni: Tazama! Kulikuwa na joka mwekundu mkubwa ambaye alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na kulikuwa na taji saba kwenye vichwa vyake.
Un autre prodige parut aussi dans le ciel: tout à coup on vit un grand dragon rouge; il avait sept têtes et dix cornes, et sur ses têtes sept diadèmes;
4 Mkia wake ulikokota theluthi moja ya nyota mbinguni na kuzitupa chini duniani. Joka alisimama mbele ya mwanamke aliyekuwa anakaribia kuzaa, ili kwamba wakati anazaa, apate kummeza mtoto wake.
de sa queue, il entraînait le tiers des étoiles du ciel, et il les jeta sur la terre; et il se dressa devant la femme qui allait enfanter, afin de dévorer son enfant, dès qu'elle l'aurait mis au monde.
5 Alimzaa mwana, mtoto wa kiume, ambaye atayatawala mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Mtoto wake alinyakuliwa juu kwa Mungu na kwenye kiti chake cha enzi,
La femme donna le jour à un fils, un enfant mâle, qui devait gouverner toutes les nations avec une verge de fer. L'enfant fut enlevé auprès de Dieu et vers son trône,
6 na mwanamke alikimbilia nyikani, mahali ambapo Mungu alikuwa ameandaa eneo kwa ajili yake, ili aweze kuhudumiwa kwa siku 1, 260.
et la femme s'enfuit au désert, où Dieu lui avait préparé une retraite, afin qu'elle y fût nourrie pendant douze cent soixante jours.
7 Sasa kulikuwa na vita mbinguni. Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka; naye joka mkubwa na malaika zake wakapigana nao.
Alors il y eut un combat dans le ciel: Michel et ses anges s'avancèrent pour combattre le dragon; et le dragon et ses anges combattirent,
8 Lakini joka hakuwa na nguvu za kutosha kushinda. Kwa hiyo haikuwepo tena nafasi mbinguni kwa ajili yake na malaika zake.
mais ils ne purent vaincre, et la place même qu'ils occupaient ne se retrouva plus dans le ciel.
9 Joka mkubwa—yule nyoka wa zamani aitwaye ibilisi au Shetani ambaye hudanganya - dunia nzima akatupwa chini katika dunia, na malaika zake wakatupwa chini pamoja naye.
Il fut précipité, le grand dragon, le serpent ancien, celui qui est appelé le diable et Satan, le séducteur de toute la terre, il fut précipité sur la terre, et ses anges avec lui.
10 Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni: “Sasa wokovu umekuja, nguvu—na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake. Kwa kuwa mshitaki wa ndugu zetu ametupwa chini—ambaye aliwashitaki mbele za Mungu wetu mchana na usiku.
Et j'entendis dans le ciel une voix forte, qui disait: «Maintenant, le salut, la puissance et l'empire appartiennent à notre Dieu, et l'autorité, à son Oint; car il a été précipité, l'accusateur de nos frères, celui qui les accusait jour et nuit devant notre Dieu.
11 Walimshinda kwa damu ya Mwanakondoo na kwa neno la ushuhuda wao, kwa maana hawakupenda sana maisha yao, hata kufa.
Eux aussi l'ont vaincu par le sang de l'agneau et par la fermeté de leur témoignage, ayant renoncé à l'amour de la vie, jusqu’à souffrir la mort.
12 Kwa hiyo, shangilieni, ninyi mbingu, na wote mnaokaa ndani yake. Lakini ole wa nchi na bahari kwa sababu mwovu ameshuka kwenu. Amejawa na hasira kali, kwa sababu anajua kwamba ana muda mchache tu.
C'est pourquoi, tressaillez de joie, cieux, et vous qui les habitez! Malheur à la terre et à la mer! parce que le diable est descendu vers vous, plein d'une grande fureur, sachant qu'il ne lui reste que peu de temps.»
13 Wakati joka alipotambua kuwa ametupwa chini kwenye nchi, alimfuata mwanamke ambaye alikuwa amezaa mtoto wa kiume.
Lorsque le dragon se vit précipité sur la terre, il poursuivit la femme qui avait mis au monde l'enfant mâle;
14 Lakini mwanamke alipewa mabawa mawili ya tai mkubwa, ili kwamba aweze kuruka hadi kwenye eneo lililoandaliwa kwa ajili yake kule jangwani, eneo ambalo angeweza kutunzwa, kwa wakati, nyakati na nusu wakati-mahali asipoweza kupafikia huyo nyoka.
mais la femme reçut deux ailes de grand aigle, pour s'envoler au désert, en sa retraite, où elle devait être nourrie pendant un temps, des temps et la moitié d'un temps, loin de la vue du dragon.
15 Nyoka alimwaga maji kutoka mdomoni mwake kama mto, ili afanye gharika ya kumgharikisha.
Alors le dragon lança de sa gueule, après la femme, de l'eau comme un fleuve, pour l'entraîner dans le fleuve;
16 Lakini ardhi ilimsaidia mwanamke. Ilifunua kinywa chake na kuumeza mto alioutema joka kutoka kinywani mwake.
mais la terre vint au secours de la femme, elle s'entr'ouvrit, et engloutit le fleuve que le dragon avait vomi de sa gueule.
17 Kisha joka akamkasirikia mwanamke naye aliondoka na kufanya vita na uzao wake wote—wale wanaotii amri za Mungu na kushikilia ushuhuda kuhusu Yesu.
Et le dragon fut transporté de fureur contre la femme; il alla faire la guerre au reste de ses enfants, à ceux qui observent les commandements de Dieu et qui gardent le témoignage de Jésus; et il s'arrêta sur le sable de la mer.

< Ufunuo 12 >