< Ufunuo 12 >

1 Ishara kuu ilionekana mbinguni: mwanamke aliyefunikwa na jua, na akiwa na mwezi chini ya miguu yake; na taji ya nyota kumi na mbili ilikuwa juu ya kichwa chake.
And a great sign was seen in the heaven, a woman arrayed with the sun, and the moon under her feet, and upon her head a crown of twelve stars,
2 Alikuwa na mimba na alikuwa analia kwa ajili ya maumivu ya kuzaa—katika uchungu wa kujifungua.
and being with child she doth cry out, travailing and pained to bring forth.
3 Na ishara nyingine ilionekana mbinguni: Tazama! Kulikuwa na joka mwekundu mkubwa ambaye alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na kulikuwa na taji saba kwenye vichwa vyake.
And there was seen another sign in the heaven, and, lo, a great red dragon, having seven heads and ten horns, and upon his head seven diadems,
4 Mkia wake ulikokota theluthi moja ya nyota mbinguni na kuzitupa chini duniani. Joka alisimama mbele ya mwanamke aliyekuwa anakaribia kuzaa, ili kwamba wakati anazaa, apate kummeza mtoto wake.
and his tail doth draw the third of the stars of the heaven, and he did cast them to the earth; and the dragon did stand before the woman who is about to bring forth, that when she may bring forth, her child he may devour;
5 Alimzaa mwana, mtoto wa kiume, ambaye atayatawala mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Mtoto wake alinyakuliwa juu kwa Mungu na kwenye kiti chake cha enzi,
and she brought forth a male child, who is about to rule all the nations with a rod of iron, and caught away was her child unto God and His throne,
6 na mwanamke alikimbilia nyikani, mahali ambapo Mungu alikuwa ameandaa eneo kwa ajili yake, ili aweze kuhudumiwa kwa siku 1, 260.
and the woman did flee to the wilderness, where she hath a place made ready from God, that there they may nourish her — days a thousand, two hundred, sixty.
7 Sasa kulikuwa na vita mbinguni. Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka; naye joka mkubwa na malaika zake wakapigana nao.
And there came war in the heaven; Michael and his messengers did war against the dragon, and the dragon did war, and his messengers,
8 Lakini joka hakuwa na nguvu za kutosha kushinda. Kwa hiyo haikuwepo tena nafasi mbinguni kwa ajili yake na malaika zake.
and they did not prevail, nor was their place found any more in the heaven;
9 Joka mkubwa—yule nyoka wa zamani aitwaye ibilisi au Shetani ambaye hudanganya - dunia nzima akatupwa chini katika dunia, na malaika zake wakatupwa chini pamoja naye.
and the great dragon was cast forth — the old serpent, who is called 'Devil,' and 'the Adversary,' who is leading astray the whole world — he was cast forth to the earth, and his messengers were cast forth with him.
10 Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni: “Sasa wokovu umekuja, nguvu—na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake. Kwa kuwa mshitaki wa ndugu zetu ametupwa chini—ambaye aliwashitaki mbele za Mungu wetu mchana na usiku.
And I heard a great voice saying in the heaven, 'Now did come the salvation, and the power, and the reign, of our God, and the authority of His Christ, because cast down was the accuser of our brethren, who is accusing them before our God day and night;
11 Walimshinda kwa damu ya Mwanakondoo na kwa neno la ushuhuda wao, kwa maana hawakupenda sana maisha yao, hata kufa.
and they did overcome him because of the blood of the Lamb, and because of the word of their testimony, and they did not love their life — unto death;
12 Kwa hiyo, shangilieni, ninyi mbingu, na wote mnaokaa ndani yake. Lakini ole wa nchi na bahari kwa sababu mwovu ameshuka kwenu. Amejawa na hasira kali, kwa sababu anajua kwamba ana muda mchache tu.
because of this be glad, ye heavens, and those in them who do tabernacle; woe to those inhabiting the land and the sea, because the Devil did go down unto you, having great wrath, having known that he hath little time.'
13 Wakati joka alipotambua kuwa ametupwa chini kwenye nchi, alimfuata mwanamke ambaye alikuwa amezaa mtoto wa kiume.
And when the dragon saw that he was cast forth to the earth, he pursued the woman who did bring forth the male,
14 Lakini mwanamke alipewa mabawa mawili ya tai mkubwa, ili kwamba aweze kuruka hadi kwenye eneo lililoandaliwa kwa ajili yake kule jangwani, eneo ambalo angeweza kutunzwa, kwa wakati, nyakati na nusu wakati-mahali asipoweza kupafikia huyo nyoka.
and there were given to the woman two wings of the great eagle, that she may fly to the wilderness, to her place, where she is nourished a time, and times, and half a time, from the face of the serpent;
15 Nyoka alimwaga maji kutoka mdomoni mwake kama mto, ili afanye gharika ya kumgharikisha.
and the serpent did cast forth after the woman, out of his mouth, water as a river, that he may cause her to be carried away by the river,
16 Lakini ardhi ilimsaidia mwanamke. Ilifunua kinywa chake na kuumeza mto alioutema joka kutoka kinywani mwake.
and the land did help the woman, and the land did open its mouth and did swallow up the river, that the dragon did cast forth out of his mouth;
17 Kisha joka akamkasirikia mwanamke naye aliondoka na kufanya vita na uzao wake wote—wale wanaotii amri za Mungu na kushikilia ushuhuda kuhusu Yesu.
and the dragon was angry against the woman, and went away to make war with the rest of her seed, those keeping the commands of God, and having the testimony of Jesus Christ.

< Ufunuo 12 >