< Ufunuo 12 >
1 Ishara kuu ilionekana mbinguni: mwanamke aliyefunikwa na jua, na akiwa na mwezi chini ya miguu yake; na taji ya nyota kumi na mbili ilikuwa juu ya kichwa chake.
Then a great portent was seen in the heavens – a woman whose robe was the sun, and who had the moon under her feet, and on her head a crown of twelve stars.
2 Alikuwa na mimba na alikuwa analia kwa ajili ya maumivu ya kuzaa—katika uchungu wa kujifungua.
She was pregnant; and she is crying out in the pain and agony of childbirth.
3 Na ishara nyingine ilionekana mbinguni: Tazama! Kulikuwa na joka mwekundu mkubwa ambaye alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na kulikuwa na taji saba kwenye vichwa vyake.
Another portent also was seen in the heavens There was a great red Dragon, with seven heads and ten horns, and on his heads were seven diadems.
4 Mkia wake ulikokota theluthi moja ya nyota mbinguni na kuzitupa chini duniani. Joka alisimama mbele ya mwanamke aliyekuwa anakaribia kuzaa, ili kwamba wakati anazaa, apate kummeza mtoto wake.
His tail draws after it a third of the stars in the heavens, and it hurled them down on the earth. The Dragon is standing in front of the woman who is about to give birth to the child, so that he may devour it as soon as it is born.
5 Alimzaa mwana, mtoto wa kiume, ambaye atayatawala mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Mtoto wake alinyakuliwa juu kwa Mungu na kwenye kiti chake cha enzi,
The woman gave birth to a son, a male child, who is destined to rule all the nations with an iron rod; and her child was at once caught up to God on his throne.
6 na mwanamke alikimbilia nyikani, mahali ambapo Mungu alikuwa ameandaa eneo kwa ajili yake, ili aweze kuhudumiwa kwa siku 1, 260.
But the woman fled into the wilderness, where there is a place prepared for her by God, to be tended there for twelve hundred and sixty days.
7 Sasa kulikuwa na vita mbinguni. Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka; naye joka mkubwa na malaika zake wakapigana nao.
Then a battle took place in the heavens. Michael and his angels fought with the Dragon. But though the Dragon, with his angels, fought,
8 Lakini joka hakuwa na nguvu za kutosha kushinda. Kwa hiyo haikuwepo tena nafasi mbinguni kwa ajili yake na malaika zake.
he did not prevail; and there was no place left for them any longer in the heavens.
9 Joka mkubwa—yule nyoka wa zamani aitwaye ibilisi au Shetani ambaye hudanganya - dunia nzima akatupwa chini katika dunia, na malaika zake wakatupwa chini pamoja naye.
Then the great Dragon, the primeval snake, known as the ‘devil’ and ‘Satan,’ who deceives all the world, was hurled down to the earth, and his angels were hurled down with him.
10 Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni: “Sasa wokovu umekuja, nguvu—na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake. Kwa kuwa mshitaki wa ndugu zetu ametupwa chini—ambaye aliwashitaki mbele za Mungu wetu mchana na usiku.
And I heard a loud voice in heaven which said – ‘Now has begun the day of the salvation, and Power, and Dominion of our God, and the Rule of his Christ; for the Accuser of our people has been hurled down, he who has been accusing them before our God day and night.
11 Walimshinda kwa damu ya Mwanakondoo na kwa neno la ushuhuda wao, kwa maana hawakupenda sana maisha yao, hata kufa.
Their victory was due to the blood of the Lamb, and to the message to which they bore their testimony. In their love of life they shrank not from death.
12 Kwa hiyo, shangilieni, ninyi mbingu, na wote mnaokaa ndani yake. Lakini ole wa nchi na bahari kwa sababu mwovu ameshuka kwenu. Amejawa na hasira kali, kwa sababu anajua kwamba ana muda mchache tu.
Therefore, be glad, heaven, and all who live in heaven! Alas for the earth and for the sea, for the devil has gone down to you in great fury, knowing that he has but little time.’
13 Wakati joka alipotambua kuwa ametupwa chini kwenye nchi, alimfuata mwanamke ambaye alikuwa amezaa mtoto wa kiume.
When the Dragon saw that he was hurled down to the earth, he pursued the woman who had given birth to the male child.
14 Lakini mwanamke alipewa mabawa mawili ya tai mkubwa, ili kwamba aweze kuruka hadi kwenye eneo lililoandaliwa kwa ajili yake kule jangwani, eneo ambalo angeweza kutunzwa, kwa wakati, nyakati na nusu wakati-mahali asipoweza kupafikia huyo nyoka.
But to the woman were given the two wings of the great eagle, so that she might fly to her place in the wilderness, where she is being tended for one year, and for two years, and for half a year in safety from the snake.
15 Nyoka alimwaga maji kutoka mdomoni mwake kama mto, ili afanye gharika ya kumgharikisha.
Then the snake poured water from its mouth after the woman, like a river, so that it might sweep her away.
16 Lakini ardhi ilimsaidia mwanamke. Ilifunua kinywa chake na kuumeza mto alioutema joka kutoka kinywani mwake.
But Earth came to her help, and opened her mouth and drank up the river which the Dragon had poured out of its mouth.
17 Kisha joka akamkasirikia mwanamke naye aliondoka na kufanya vita na uzao wake wote—wale wanaotii amri za Mungu na kushikilia ushuhuda kuhusu Yesu.
The Dragon was enraged at the woman, and went to fight with the rest of her offspring – those who lay to heart the commands of God and bear their testimony to Jesus;