< Ufunuo 12 >
1 Ishara kuu ilionekana mbinguni: mwanamke aliyefunikwa na jua, na akiwa na mwezi chini ya miguu yake; na taji ya nyota kumi na mbili ilikuwa juu ya kichwa chake.
And a great sign was seen in heaven; a woman clothed with the sun, and the moon under her feet, and upon her head a crown of twelve stars;
2 Alikuwa na mimba na alikuwa analia kwa ajili ya maumivu ya kuzaa—katika uchungu wa kujifungua.
and being with child she crieth out, travailing in birth, and pained to be delivered.
3 Na ishara nyingine ilionekana mbinguni: Tazama! Kulikuwa na joka mwekundu mkubwa ambaye alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na kulikuwa na taji saba kwenye vichwa vyake.
And another sign was seen in heaven; and behold, a great red dragon, having seven heads and ten horns, and on his heads seven diadems;
4 Mkia wake ulikokota theluthi moja ya nyota mbinguni na kuzitupa chini duniani. Joka alisimama mbele ya mwanamke aliyekuwa anakaribia kuzaa, ili kwamba wakati anazaa, apate kummeza mtoto wake.
and his tail dragged the third part of the stars of heaven, and cast them to the earth. And the dragon standeth before the woman who was about to bring forth, that when she hath brought forth he may devour her child.
5 Alimzaa mwana, mtoto wa kiume, ambaye atayatawala mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Mtoto wake alinyakuliwa juu kwa Mungu na kwenye kiti chake cha enzi,
And she brought forth a man-child, who is to rule all the nations with a rod of iron; and her child was caught up to God, and to his throne.
6 na mwanamke alikimbilia nyikani, mahali ambapo Mungu alikuwa ameandaa eneo kwa ajili yake, ili aweze kuhudumiwa kwa siku 1, 260.
And the woman fled into the wilderness, where she hath a place prepared by God, that they should nourish her there a thousand two hundred and sixty days.
7 Sasa kulikuwa na vita mbinguni. Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka; naye joka mkubwa na malaika zake wakapigana nao.
And there was war in heaven; Michael and his angels fought against the dragon; and the dragon fought and his angels,
8 Lakini joka hakuwa na nguvu za kutosha kushinda. Kwa hiyo haikuwepo tena nafasi mbinguni kwa ajili yake na malaika zake.
and prevailed not; neither was their place found any more in heaven.
9 Joka mkubwa—yule nyoka wa zamani aitwaye ibilisi au Shetani ambaye hudanganya - dunia nzima akatupwa chini katika dunia, na malaika zake wakatupwa chini pamoja naye.
And the great dragon was cast down, the old serpent, called the Devil and Satan, who deceiveth the whole world; he was cast down to the earth, and his angels were cast down with him.
10 Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni: “Sasa wokovu umekuja, nguvu—na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake. Kwa kuwa mshitaki wa ndugu zetu ametupwa chini—ambaye aliwashitaki mbele za Mungu wetu mchana na usiku.
And I heard a loud voice in heaven, saying, Now is come the salvation and the power and the kingdom of our God, and the authority of his Christ; for the accuser of our brethren is cast down, who accused them before our God day and night;
11 Walimshinda kwa damu ya Mwanakondoo na kwa neno la ushuhuda wao, kwa maana hawakupenda sana maisha yao, hata kufa.
and they conquered him because of the blood of the Lamb, and because of the word of their testimony; and they loved not their lives, even to death.
12 Kwa hiyo, shangilieni, ninyi mbingu, na wote mnaokaa ndani yake. Lakini ole wa nchi na bahari kwa sababu mwovu ameshuka kwenu. Amejawa na hasira kali, kwa sababu anajua kwamba ana muda mchache tu.
Therefore rejoice, ye heavens, and ye that dwell in them. Woe to the earth and the sea! for the Devil is come down to you, having great wrath, because he knoweth that he hath but a short time.
13 Wakati joka alipotambua kuwa ametupwa chini kwenye nchi, alimfuata mwanamke ambaye alikuwa amezaa mtoto wa kiume.
And when the dragon saw that he was cast down to the earth, he persecuted the woman who brought forth the man-child.
14 Lakini mwanamke alipewa mabawa mawili ya tai mkubwa, ili kwamba aweze kuruka hadi kwenye eneo lililoandaliwa kwa ajili yake kule jangwani, eneo ambalo angeweza kutunzwa, kwa wakati, nyakati na nusu wakati-mahali asipoweza kupafikia huyo nyoka.
And to the woman were given the two wings of a great eagle, that she might fly into the wilderness, into her place, where she is nourished for a time, and times, and half a time, from the face of the serpent.
15 Nyoka alimwaga maji kutoka mdomoni mwake kama mto, ili afanye gharika ya kumgharikisha.
And the serpent cast out of his mouth water as a river, after the woman, that he might cause her to be carried away by the river.
16 Lakini ardhi ilimsaidia mwanamke. Ilifunua kinywa chake na kuumeza mto alioutema joka kutoka kinywani mwake.
And the earth helped the woman, and the earth opened her mouth, and swallowed up the river which the dragon cast out of his mouth.
17 Kisha joka akamkasirikia mwanamke naye aliondoka na kufanya vita na uzao wake wote—wale wanaotii amri za Mungu na kushikilia ushuhuda kuhusu Yesu.
And the dragon was enraged at the woman, and went away to make war with the rest of her offspring, who keep the commandments of God, and maintain the testimony to Jesus.