< Ufunuo 12 >

1 Ishara kuu ilionekana mbinguni: mwanamke aliyefunikwa na jua, na akiwa na mwezi chini ya miguu yake; na taji ya nyota kumi na mbili ilikuwa juu ya kichwa chake.
And a great sign was seen in heaven. A woman clothed with the sun, and the moon under her feet, and a crown of twelve stars upon her head.
2 Alikuwa na mimba na alikuwa analia kwa ajili ya maumivu ya kuzaa—katika uchungu wa kujifungua.
And having in her womb, she cried out, suffering birth pains, and suffering to give birth.
3 Na ishara nyingine ilionekana mbinguni: Tazama! Kulikuwa na joka mwekundu mkubwa ambaye alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na kulikuwa na taji saba kwenye vichwa vyake.
And another sign was seen in heaven. And behold, a great fiery red dragon, having seven heads and ten horns, and seven diadems upon his heads.
4 Mkia wake ulikokota theluthi moja ya nyota mbinguni na kuzitupa chini duniani. Joka alisimama mbele ya mwanamke aliyekuwa anakaribia kuzaa, ili kwamba wakati anazaa, apate kummeza mtoto wake.
And his tail drags the third part of the stars of the sky, and cast them to the earth. And the dragon stood before the woman who was going to give birth, so that when she gave birth he might devour her child.
5 Alimzaa mwana, mtoto wa kiume, ambaye atayatawala mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Mtoto wake alinyakuliwa juu kwa Mungu na kwenye kiti chake cha enzi,
And she gave birth to a son, a male who was going to tend all the nations with an iron rod. And her child was taken up to God and to his throne.
6 na mwanamke alikimbilia nyikani, mahali ambapo Mungu alikuwa ameandaa eneo kwa ajili yake, ili aweze kuhudumiwa kwa siku 1, 260.
And the woman fled into the wilderness where she has a place there prepared by God, so that they may nourish her there a thousand two hundred sixty days.
7 Sasa kulikuwa na vita mbinguni. Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka; naye joka mkubwa na malaika zake wakapigana nao.
And war developed in heaven: Michael and his agents to fight with the dragon. And the dragon and his agents fought.
8 Lakini joka hakuwa na nguvu za kutosha kushinda. Kwa hiyo haikuwepo tena nafasi mbinguni kwa ajili yake na malaika zake.
And he did not prevail, nor was a place found for him any more in heaven.
9 Joka mkubwa—yule nyoka wa zamani aitwaye ibilisi au Shetani ambaye hudanganya - dunia nzima akatupwa chini katika dunia, na malaika zake wakatupwa chini pamoja naye.
And the great dragon was cast out, the ancient serpent, called the Devil and Satan, he who leads the whole world astray. He was cast out to the earth, and his agents were cast out with him.
10 Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni: “Sasa wokovu umekuja, nguvu—na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake. Kwa kuwa mshitaki wa ndugu zetu ametupwa chini—ambaye aliwashitaki mbele za Mungu wetu mchana na usiku.
And I heard a great voice in heaven, saying, Now it came to pass, the salvation, and the power, and the kingdom of our God, and the authority of his Christ. Because the accuser of our brothers was cast out, who accuses them before our God day and night.
11 Walimshinda kwa damu ya Mwanakondoo na kwa neno la ushuhuda wao, kwa maana hawakupenda sana maisha yao, hata kufa.
And they overcame him by the blood of the Lamb, and by the word of their testimony. And they loved not their life to the point of death.
12 Kwa hiyo, shangilieni, ninyi mbingu, na wote mnaokaa ndani yake. Lakini ole wa nchi na bahari kwa sababu mwovu ameshuka kwenu. Amejawa na hasira kali, kwa sababu anajua kwamba ana muda mchache tu.
Rejoice because of this, O heavens, and ye who dwell in them. Woe to the earth and the sea, because the devil has come down to you, having great wrath, knowing that he has little time.
13 Wakati joka alipotambua kuwa ametupwa chini kwenye nchi, alimfuata mwanamke ambaye alikuwa amezaa mtoto wa kiume.
And when the dragon saw that he was cast to the earth, he persecuted the woman who gave birth to the male.
14 Lakini mwanamke alipewa mabawa mawili ya tai mkubwa, ili kwamba aweze kuruka hadi kwenye eneo lililoandaliwa kwa ajili yake kule jangwani, eneo ambalo angeweza kutunzwa, kwa wakati, nyakati na nusu wakati-mahali asipoweza kupafikia huyo nyoka.
And two wings of the great eagle were given to the woman, so that she might fly into the wilderness to her place. So that she might be nourished there for a time, and times, and half a time, from the face of the serpent.
15 Nyoka alimwaga maji kutoka mdomoni mwake kama mto, ili afanye gharika ya kumgharikisha.
And the serpent cast water like a river out of his mouth after the woman, so that he might make her carried away by the flood.
16 Lakini ardhi ilimsaidia mwanamke. Ilifunua kinywa chake na kuumeza mto alioutema joka kutoka kinywani mwake.
And the earth helped the woman. And the earth opened its mouth and swallowed the river that the dragon cast out of his mouth.
17 Kisha joka akamkasirikia mwanamke naye aliondoka na kufanya vita na uzao wake wote—wale wanaotii amri za Mungu na kushikilia ushuhuda kuhusu Yesu.
And the dragon was angry toward the woman, and went to make war with the remnant of her seed, those keeping the commandments of God, and having the testimony of Jesus.

< Ufunuo 12 >