< Ufunuo 10 >

1 Kisha nikaona malaika mwingine mkuu akishuka chini kutoka mbinguni. Alikuwa amefungwa katika wingu, na kulikuwa na upinde wa mvua juu ya kichwa chake. Uso wake ulikuwa kama jua na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto.
Then I saw another strong angel coming down from Heaven. He was robed in a cloud, and over his head was the rainbow. His face was like the sun, and his feet resembled pillars of fire.
2 Alishikilia gombo dogo katika mkono wake lililokuwa limefunuliwa, naye aliweka mguu wake wa kulia juu ya bahari na mguu wake wa kushoto juu ya nchi kavu.
In his hand he held a small scroll unrolled; and, planting his right foot on the sea and his left foot on the land,
3 Kisha alipaza sauti ya juu kama simba aungurumapo, na wakati alipopaza sauti radi saba ziliunguruma.
he cried out in a loud voice which resembled the roar of a lion. And when he had cried out, each of the seven peals of thunder uttered its own message.
4 Wakati radi saba zilipounguruma, nilikuwa nakaribia kuandika, lakini nilisikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Tunza iwe siri kile ambacho radi saba zimesema. Usiiandike.”
And when the seven peals of thunder had spoken, I was about to write down what they had said; but I heard a voice from Heaven which told me to keep secret all that the seven peals of thunder had said, and not write it down.
5 Kisha malaika niliyemwona amesimama juu ya bahari na nchi kavu, aliinua mkono wake juu mbinguni
Then the angel that I saw standing on the sea and on the land, lifted his right hand toward Heaven.
6 na kuapa kwa yule aishiye milele na milele —aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, dunia na vyote vilivyomo, na bahari na vyote vilivyomo: “Hakutakuwepo kuchelewa tena. (aiōn g165)
And in the name of Him who lives until the Ages of the Ages, the Creator of Heaven and all that is in it, of the earth and all that is in it, and of the sea and all that is in it, he solemnly declared, (aiōn g165)
7 Lakini katika siku ile, wakati malaika wa saba atakapokaribia kupiga tarumbeta yake, ndipo siri ya Mungu itakuwa imetimizwa, kama alivyotangaza kwa watumishi wake manabii.”
"There shall be no further delay; but in the days when the seventh angel blows his trumpet--when he begins to do so--then the secret purposes of God are realized, in accordance with the good news which He gave to His servants the Prophets."
8 Sauti niliyosikia kutoka mbinguni iliniambia tena: “Nenda, chukua gombo dogo lililofunuliwa ambalo kiko katika mkono wa malaika aliyesimama juu ya bahari na juu ya nchi kavu.”
Then the voice which I had heard speaking from Heaven once more addressed me. It said, "Go and take the little book which lies open in the hand of the angel who is standing on the sea and on the land."
9 Kisha nilikwenda kwa malaika na kumwambia anipe gombo dogo. Aliniambia, “Chukua gombo na ule. Litalifanya tumbo lako liwe na uchungu, lakini katika mdomo wako litakuwa tamu kama asali.”
So I went to the angel and asked him to give me the little book. "Take it," he said, "and eat the whole of it. You will find it bitter when you have eaten it, although in your mouth it will taste as sweet as honey."
10 Nilichukua gombo dogo kutoka mkononi mwa malaika na kulila. Lilikuwa kitamu kama asali katika mdomo wangu, lakini baada ya kula, tumbo langu lilikuwa na uchungu.
So I took the roll out of the angel's hand and ate the whole of it; and in my mouth it was as sweet as honey, but when I had eaten it I found it very bitter.
11 Kisha baadhi ya sauti ziliniambia, “Unapaswa kutabiri tena kuhusu watu wengi, mataifa, lugha, na wafalme.”
And a voice said to me, "You must prophesy yet further concerning peoples, nations, languages, and many kings."

< Ufunuo 10 >