< Ufunuo 10 >

1 Kisha nikaona malaika mwingine mkuu akishuka chini kutoka mbinguni. Alikuwa amefungwa katika wingu, na kulikuwa na upinde wa mvua juu ya kichwa chake. Uso wake ulikuwa kama jua na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto.
And I saw another angel mighty coming down out of heaven having clothed himself with a cloud, and the rainbow upon (the head *NK(o)*) of him, and the face of him [was] like the sun, and the feet of him like pillars of fire,
2 Alishikilia gombo dogo katika mkono wake lililokuwa limefunuliwa, naye aliweka mguu wake wa kulia juu ya bahari na mguu wake wa kushoto juu ya nchi kavu.
and (having *N(k)O*) in the hand of him (a little scroll *NK(o)*) opened And he placed the foot of him right upon (the sea, *N(k)O*) the and left upon (the earth, *N(k)O*)
3 Kisha alipaza sauti ya juu kama simba aungurumapo, na wakati alipopaza sauti radi saba ziliunguruma.
And he cried out in a voice loud as a lion roars. And when he cried out, sounded the seven thunders the their own voice.
4 Wakati radi saba zilipounguruma, nilikuwa nakaribia kuandika, lakini nilisikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Tunza iwe siri kile ambacho radi saba zimesema. Usiiandike.”
And when spoke the seven thunders, (the voices of themselves *K*) I was about to write. But I heard a voice out of heaven saying (to me *K*) do seal what spoke the seven thunders, and not (them *N(k)O*) may write.
5 Kisha malaika niliyemwona amesimama juu ya bahari na nchi kavu, aliinua mkono wake juu mbinguni
And the angel whom I saw standing on the sea and on the land lifted up the hand of him (the right *NO*) to heaven
6 na kuapa kwa yule aishiye milele na milele —aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, dunia na vyote vilivyomo, na bahari na vyote vilivyomo: “Hakutakuwepo kuchelewa tena. (aiōn g165)
and he swore by the [One] living to the ages of the ages, who created heaven and the [things] in it and the earth and the [things] in it and the sea and the [things] in it that Delay no longer no longer will there be! (aiōn g165)
7 Lakini katika siku ile, wakati malaika wa saba atakapokaribia kupiga tarumbeta yake, ndipo siri ya Mungu itakuwa imetimizwa, kama alivyotangaza kwa watumishi wake manabii.”
But in the days of the voice of the seventh angel, when he may soon to sound [the] trumpet, then (would be completed *N(k)O*) the mystery of God, as evangelised ([to] those *N(k)O*) (His own *NK(o)*) (servants [to] the prophets. *N(k)O*)
8 Sauti niliyosikia kutoka mbinguni iliniambia tena: “Nenda, chukua gombo dogo lililofunuliwa ambalo kiko katika mkono wa malaika aliyesimama juu ya bahari na juu ya nchi kavu.”
And the voice that I heard out of heaven again (was speaking *N(k)O*) with me and (saying; *N(k)O*) do go do take the (little scroll *N(k)O*) which opened in the hand of the angel who standing upon the sea and upon the land.
9 Kisha nilikwenda kwa malaika na kumwambia anipe gombo dogo. Aliniambia, “Chukua gombo na ule. Litalifanya tumbo lako liwe na uchungu, lakini katika mdomo wako litakuwa tamu kama asali.”
And I went to the angel saying to him (to give *N(k)O*) me the little scroll. And he says to me; do take and do eat it. and it will make bitter your stomach, but in the mouth of you it will be sweet as honey.
10 Nilichukua gombo dogo kutoka mkononi mwa malaika na kulila. Lilikuwa kitamu kama asali katika mdomo wangu, lakini baada ya kula, tumbo langu lilikuwa na uchungu.
And I took the (little scroll *NK(o)*) out of the hand of the angel and I ate it, and it was in the mouth of mine as honey sweet; and when I had eaten it, was made bitter the stomach of mine.
11 Kisha baadhi ya sauti ziliniambia, “Unapaswa kutabiri tena kuhusu watu wengi, mataifa, lugha, na wafalme.”
And (they say *N(k)O*) to me; It is necessary for you again to prophesy concerning peoples and (concerning *o*) nations and [concerning] tongues and [concerning] kings many.

< Ufunuo 10 >