< Ufunuo 10 >
1 Kisha nikaona malaika mwingine mkuu akishuka chini kutoka mbinguni. Alikuwa amefungwa katika wingu, na kulikuwa na upinde wa mvua juu ya kichwa chake. Uso wake ulikuwa kama jua na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto.
And I saw another mighty angel coming down out of heaven, clad with a cloud; and a rainbow was upon his head, and his face was like the sun, and his feet like pillars of fire.
2 Alishikilia gombo dogo katika mkono wake lililokuwa limefunuliwa, naye aliweka mguu wake wa kulia juu ya bahari na mguu wake wa kushoto juu ya nchi kavu.
In his hand he had a little book, open; and he set his right foot upon the sea, and his left upon the land.
3 Kisha alipaza sauti ya juu kama simba aungurumapo, na wakati alipopaza sauti radi saba ziliunguruma.
With a great voice he shouted as a lion roars; and when he shouted, the seven thunders uttered their voices.
4 Wakati radi saba zilipounguruma, nilikuwa nakaribia kuandika, lakini nilisikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Tunza iwe siri kile ambacho radi saba zimesema. Usiiandike.”
When the seven thunders uttered their voices, I was about to write; but I heard a voice from the sky, saying, "Seal up the words which the seven thunders uttered, and write them not."
5 Kisha malaika niliyemwona amesimama juu ya bahari na nchi kavu, aliinua mkono wake juu mbinguni
And the angel whom I had seen standing upon the sea and upon the land lifted up his right hand to heaven,
6 na kuapa kwa yule aishiye milele na milele —aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, dunia na vyote vilivyomo, na bahari na vyote vilivyomo: “Hakutakuwepo kuchelewa tena. (aiōn )
and swore by him who lives forever and ever, who created the heaven and all that is in it, and the earth and all that is in it, and the sea and all that is in it, "Delay there shall be no more, (aiōn )
7 Lakini katika siku ile, wakati malaika wa saba atakapokaribia kupiga tarumbeta yake, ndipo siri ya Mungu itakuwa imetimizwa, kama alivyotangaza kwa watumishi wake manabii.”
but in the days of the voice of the seventh angel, when he is about to blow his trumpet, then shall there be finished the mystery of God, according to the Good News which he told unto his slaves, the prophets."
8 Sauti niliyosikia kutoka mbinguni iliniambia tena: “Nenda, chukua gombo dogo lililofunuliwa ambalo kiko katika mkono wa malaika aliyesimama juu ya bahari na juu ya nchi kavu.”
And the voice which I had heard from heaven, I heard again, speaking to me, and saying, "Go, take the little book that is open in the hand of the angel who stands upon the sea and upon the land."
9 Kisha nilikwenda kwa malaika na kumwambia anipe gombo dogo. Aliniambia, “Chukua gombo na ule. Litalifanya tumbo lako liwe na uchungu, lakini katika mdomo wako litakuwa tamu kama asali.”
And I went to the angel and told him to give me the little book. And he said to me. "Take it, and eat it up; it will make your belly bitter, but in your mouth it will be as sweet as honey."
10 Nilichukua gombo dogo kutoka mkononi mwa malaika na kulila. Lilikuwa kitamu kama asali katika mdomo wangu, lakini baada ya kula, tumbo langu lilikuwa na uchungu.
I took the little book out of the hand of the angel, and ate it up, and it was in my mouth sweet like honey; but when I had eaten it, my belly was made bitter.
11 Kisha baadhi ya sauti ziliniambia, “Unapaswa kutabiri tena kuhusu watu wengi, mataifa, lugha, na wafalme.”
Then I was told, "You must prophesy again over many peoples and nations and tongues and kings."