< Ufunuo 10 >

1 Kisha nikaona malaika mwingine mkuu akishuka chini kutoka mbinguni. Alikuwa amefungwa katika wingu, na kulikuwa na upinde wa mvua juu ya kichwa chake. Uso wake ulikuwa kama jua na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto.
And I saw another mighty angel come down from heaven, clothed with a cloud, and a rainbow was on his head, and his face was as the sun, and his feet as pillars of fire.
2 Alishikilia gombo dogo katika mkono wake lililokuwa limefunuliwa, naye aliweka mguu wake wa kulia juu ya bahari na mguu wake wa kushoto juu ya nchi kavu.
And he had in his hand a little book open: and he set his right foot upon the sea, and his left foot upon the earth.
3 Kisha alipaza sauti ya juu kama simba aungurumapo, na wakati alipopaza sauti radi saba ziliunguruma.
And he cried with a loud voice as when a lion roareth. And when he had cried, seven thunders uttered their voices.
4 Wakati radi saba zilipounguruma, nilikuwa nakaribia kuandika, lakini nilisikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Tunza iwe siri kile ambacho radi saba zimesema. Usiiandike.”
And when the seven thunders had uttered their voices, I was about to write: and I heard a voice from heaven saying to me: Seal up the things which the seven thunders have spoken; and write them not.
5 Kisha malaika niliyemwona amesimama juu ya bahari na nchi kavu, aliinua mkono wake juu mbinguni
And the angel, whom I saw standing upon the sea and upon the earth, lifted up his hand to heaven,
6 na kuapa kwa yule aishiye milele na milele —aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, dunia na vyote vilivyomo, na bahari na vyote vilivyomo: “Hakutakuwepo kuchelewa tena. (aiōn g165)
And he swore by him that liveth for ever and ever, who created heaven, and the things which are therein; and the earth, and the things which are in it; and the sea, and the things which are therein: That time shall be no longer. (aiōn g165)
7 Lakini katika siku ile, wakati malaika wa saba atakapokaribia kupiga tarumbeta yake, ndipo siri ya Mungu itakuwa imetimizwa, kama alivyotangaza kwa watumishi wake manabii.”
But in the days of the voice of the seventh angel, when he shall begin to sound the trumpet, the mystery of God shall be finished, as he hath declared by his servants the prophets.
8 Sauti niliyosikia kutoka mbinguni iliniambia tena: “Nenda, chukua gombo dogo lililofunuliwa ambalo kiko katika mkono wa malaika aliyesimama juu ya bahari na juu ya nchi kavu.”
And I heard a voice from heaven again speaking to me, and saying: Go, and take the book that is open, from the hand of the angel who standeth upon the sea, and upon the earth.
9 Kisha nilikwenda kwa malaika na kumwambia anipe gombo dogo. Aliniambia, “Chukua gombo na ule. Litalifanya tumbo lako liwe na uchungu, lakini katika mdomo wako litakuwa tamu kama asali.”
And I went to the angel, saying unto him, that he should give me the book. And he said to me: Take the book, and eat it up: and it shall make thy belly bitter, but in thy mouth it shall be sweet as honey.
10 Nilichukua gombo dogo kutoka mkononi mwa malaika na kulila. Lilikuwa kitamu kama asali katika mdomo wangu, lakini baada ya kula, tumbo langu lilikuwa na uchungu.
And I took the book from the hand of the angel, and ate it up: and it was in my mouth, sweet as honey: and when I had eaten it, my belly was bitter.
11 Kisha baadhi ya sauti ziliniambia, “Unapaswa kutabiri tena kuhusu watu wengi, mataifa, lugha, na wafalme.”
And he said to me: Thou must prophesy again to many nations, and peoples, and tongues, and kings.

< Ufunuo 10 >