< Ufunuo 10 >

1 Kisha nikaona malaika mwingine mkuu akishuka chini kutoka mbinguni. Alikuwa amefungwa katika wingu, na kulikuwa na upinde wa mvua juu ya kichwa chake. Uso wake ulikuwa kama jua na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto.
Pak jsem spatřil jiného mocného anděla, jak sestupuje z nebe zahalen oblakem. Nad hlavou se mu klenula duha, tvář mu zářila jako slunce a jeho nohy se podobaly ohnivým sloupům.
2 Alishikilia gombo dogo katika mkono wake lililokuwa limefunuliwa, naye aliweka mguu wake wa kulia juu ya bahari na mguu wake wa kushoto juu ya nchi kavu.
V ruce držel právě otevřenou knihu. Pravou nohou se postavil na moře, levou na pevninu.
3 Kisha alipaza sauti ya juu kama simba aungurumapo, na wakati alipopaza sauti radi saba ziliunguruma.
Zařval a odpovědělo mu sedminásobné hřmění hromů.
4 Wakati radi saba zilipounguruma, nilikuwa nakaribia kuandika, lakini nilisikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Tunza iwe siri kile ambacho radi saba zimesema. Usiiandike.”
Rozuměl jsem tomu a chtěl jsem to zaznamenat, ale hlas z nebe mi to zakázal: „Co jsi teď slyšel, nezapisuj, nech si to zatím pro sebe!“
5 Kisha malaika niliyemwona amesimama juu ya bahari na nchi kavu, aliinua mkono wake juu mbinguni
Pak ten anděl stojící na moři i na zemi pozdvihl pravici k nebi
6 na kuapa kwa yule aishiye milele na milele —aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, dunia na vyote vilivyomo, na bahari na vyote vilivyomo: “Hakutakuwepo kuchelewa tena. (aiōn g165)
a přísahal při tom, který žije věčně a stvořil nebe i zemi se vším, co je na ní, i moře a všechny jeho obyvatele. Přísahal: „Čas je dovršen. Bůh už nebude odkládat svůj konečný soud; (aiōn g165)
7 Lakini katika siku ile, wakati malaika wa saba atakapokaribia kupiga tarumbeta yake, ndipo siri ya Mungu itakuwa imetimizwa, kama alivyotangaza kwa watumishi wake manabii.”
až zatroubí sedmý anděl, cele se naplní Boží tajemný plán, který však už dávno vyhlašoval Bůh ústy svých proroků.“
8 Sauti niliyosikia kutoka mbinguni iliniambia tena: “Nenda, chukua gombo dogo lililofunuliwa ambalo kiko katika mkono wa malaika aliyesimama juu ya bahari na juu ya nchi kavu.”
Hlas, který už před tím ke mně mluvil z nebe, se ozval znovu: „Jdi a vezmi tu otevřenou knihu z ruky anděla stojícího na moři i na zemi!“
9 Kisha nilikwenda kwa malaika na kumwambia anipe gombo dogo. Aliniambia, “Chukua gombo na ule. Litalifanya tumbo lako liwe na uchungu, lakini katika mdomo wako litakuwa tamu kama asali.”
Šel jsem tedy k tomu andělovi a požádal jsem ho, aby mi tu knihu dal. „Vezmi si ji, “řekl anděl, „a sněz ji. V ústech bude sladká jako med, v žaludku ti však zhořkne.“
10 Nilichukua gombo dogo kutoka mkononi mwa malaika na kulila. Lilikuwa kitamu kama asali katika mdomo wangu, lakini baada ya kula, tumbo langu lilikuwa na uchungu.
Vzal jsem tedy tu knihu a poslušně jsem ji snědl; skutečně chutnala sladce, ale když jsem ji spolkl, byla opravdu hořká.
11 Kisha baadhi ya sauti ziliniambia, “Unapaswa kutabiri tena kuhusu watu wengi, mataifa, lugha, na wafalme.”
Pak mi bylo řečeno: „Pokračuj ve svém těžkém úkolu a prorokuj proti mnoha národům, kmenům, jazykům a vládcům.“

< Ufunuo 10 >