< Ufunuo 1 >

1 Huu ni ufunuo wa Yesu Kristo ambao Mungu alimpa ili kuwaonesha watumishi wake mambo ambayo lazima yatokee karibuni. Aliyafanya yajulikane kwa kumtuma malaika wake kwa mtumishi wake Yohana.
Owuu wigule wa Yesu Kilisiti lwashele Ongolobhe apiye abhalanje abhembombo bhakwe ezyaje lazima zifumile nanalieshi. Agabhombile aje gabhoneshe owasontezyo ontumwa wakwe wasontezyo wakwe oYohana.
2 Yohana alitoa ushuhuda wa kila kitu alichoona kuhusiana na neno la Mungu na kwa ushuhuda uliotolewa kuhusu Yesu Kristo.
O Yohana ayanjile wahala hahalolile hahahusina nizu elwa Ngolobhe gayanjili gafumiziwe ahusu oYesu Kilisti.
3 Amebarikiwa yeye asomaye kwa sauti na wale wote wanaoyasikia maneno ya unabii huu na kutii kilichoandikwa humo, kwa sababu muda umekaribia.
Asaiwe oyo yamanyila yauje sana nabhala bhoti bhabahgovwa amazu gakuuha ega nahwogope gagasimbilwe omwo, afwatanaje omuda gupalamie.
4 Yohana, kwa makanisa saba yaliyoko Asia: neema iwe kwenu na amani kutoka kwake aliyepo, aliyekuwepo, na atakayekuja, na kutoka kwa roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi,
O Yohana, huu makanisa saba gagali hu Asia: owene gubhe hulimwi ne lweteshelo afume hulimwe, yahweli, yahali, nowayenza, nafume humpepo saba bhabholi witagalila witengo lyakwe elya pamwanya,
5 na kutoka kwa Yesu Kristo ambaye ni shahidi mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mtawala wa wafalme wa dunia hii. Kwake yeye atupendaye na ametuweka huru kutoka katika dhambi zetu kwa damu yake,
nafume hwa Yesu Kilisti yashele keti owelyoli, opapwa owahwande wabhala bhabha fwiye, nayakhete amwene ebhensi ene. Hwamwene oyo yatigene atibheshele shinza afume mmbibhi zyetu widanda lyakwe,
6 ametufanya kuwa ufalme, makuhani wa Mungu na Baba yake - kwake kuwa utukufu na nguvu milele daima. Amina. (aiōn g165)
atibheshele aje umwene ougosi wa Ngolobhe no Baba wakwe - hwamwene zuvyo neguvu wilawila hani lyoli. Amina. (aiōn g165)
7 Tazama, anakuja na mawingu; kila jicho litamwona, pamoja na wote waliomchoma. Na kabila zote za dunia wataomboleza kwake. Ndiyo, Amina.
Enya, ehwenza namabhengo; kila liso libhahulole, pandwemo na bhala bhonti bhabhalese. Na makabela gonti ege nsi. Bailila hwa mwene. Lyoli, Amina.
8 “Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu, “Yeye aliyepo, na aliyekuwepo, na ambaye anakuja, Mwenye nguvu.”
“Omwene yohwawande no wamalezye, ayanga Ogosi Ongolobhe, “Umwene yahweli, na yahali, nayabhe ahwenza owenguvu.”
9 Mimi, Yohana - ndugu yenu na mmoja anayeshiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na uvumilivu thabiti ulio katika Yesu; nilikuwa katika kisiwa kiitwacho Patimo kwa sababu ya neno la Mungu na ushuhuda kuhusu Yesu.
Ane, ne Yohana - neholo wenyu nembapandemo namwe humateso na humwene navumilile hasa wauli hwa Yesu; ehali hukisiwa shashiliwetwa patimo husabu hwizu elya Ngolobhe noshuhuda owa Yesu.
10 Nilikuwa katika Roho siku ya Bwana. Nilisikia nyuma yangu sauti ya juu kama ya tarumbeta,
Ehali hu Mpepo isiku elya Gosi. ehonvweze hunyumayane esauti yapamwanya eye itarumbeta,
11 ikisema, “andika katika kitabu unayo yaona, na uyatume kwa makanisa saba, kwenda Efeso, kwenda Smirna, kwenda Pergamo, kwenda Thiatira, kwenda Sardi, kwenda Philadelphia, na kwenda Laodikia.”
eyiga, “simba huikalata gogalola ogatume humakanisa saba, abhale wa Efeso, abhale Smirna, abhale Pergamo, abhale Thiatira, abhale Sardi, abhale Philadelphia, na abhale Laodikia.”
12 Nikageuka kuona ni sauti ya nani aliyekuwa akiongea nami, na nilipogeuka niliona kinara cha dhahabu cha taa saba.
Nagaluhana ahwenje aje sauti yananu yayangaga nane, nanagaluha nahalola ishinala eshedhahabu eshetaa saba.
13 Katikati ya kinara cha taa alikuwemo mmoja kama Mwana wa Adamu, amevaa kanzu ndefu iliyofika chini ya miguu yake, na mkanda wa dhababu kuzunguka kifua chake.
Pahati pashinala eshetaa aliomo nashi Omwana wa Adamu, akwete inkanzu itali lyalifishile pansi pamanama gakwe, nilampa lyedhahabu azyongole hushifubha shakwe.
14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe kama theluji, na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto.
Itwe lyakwe nisisi lyakwe zyalinyini nashi ahantu ahazelu nashi ebalafu, na maso gakwe gali nashi omelegwe mwoto.
15 Nyayo zake zilikuwa kama shaba iliyosuguliwa sana, kama shaba ambayo imekwisha pitishwa katika moto, na sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji mengi yanayotiririka kwa kasi.
Entondwe zyakwe nashi eshaba yesuguliwe tee, nashi eshaba yeshizenywe hu mwoto, ne sauti yakwe ehali nanshi esauti eyamenze aminji gagafuma nanali.
16 Alikuwa ameshikilia nyota saba katika mkono wake wa kuume, na kutoka kinywani mwake kulikuwa na upanga mkali wenye makali kuwili. Uso wake ulikuwa uking'aa kama mwanga mkali wa jua.
Ali khatizizye entondi saba mkhono gwakwe ogwelelo, nafume mwilomu mwakwe hwali ni panga ilyoji lyalili lyoji hwoti hubhele. Humaso gakwe hwali hulwaha nasho mwanga okhali owisanya.
17 Nilipomwona, nikaanguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kulia juu yangu na kusema, “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa Mwisho,
Nenalola, nagwa mmanama gakwe nashi umntu yafwiye. Wabheha okhono gwakwe ogwelelo pamwanya pane na yanje, “Osahogope! Ane newa Hwande na wa Malishile,
18 na ambaye ninaishi. Nalikuwa nimekufa, lakini tazama, ninaishi milele! Na ninazo funguo za mauti na kuzimu. (aiōn g165, Hadēs g86)
nanewendi ekhala. Ehali efwiye, lelo enya, ekhala wilawila! Endine nfukulo ezye nfwa na wilongo. (aiōn g165, Hadēs g86)
19 Kwa hiyo, yaandike uliyoyaona, yaliyopo sasa, na yale yatakayotokea baada ya haya.
Esho yasimbe gogalolile gagali eshi na galagagabhafumile pega.
20 Kwa maana iliyojificha kuhusu nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume, na kile kinara cha dhahabu cha taa saba: nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba, na kinara cha taa saba ni yale makanisa saba.”
Kwana gagawifisile ahusu entondwe saba zyehazilolile hukhono wane olelo, shila eshinala eshe dhahabu eshetala saba: ntondwe saba bhantumi bhagala amakanisa saba, neshinara shetala saba gagala amakanisa saba.”

< Ufunuo 1 >