< Ufunuo 1 >

1 Huu ni ufunuo wa Yesu Kristo ambao Mungu alimpa ili kuwaonesha watumishi wake mambo ambayo lazima yatokee karibuni. Aliyafanya yajulikane kwa kumtuma malaika wake kwa mtumishi wake Yohana.
Wa yi hinhran u Yesu Kristi wa Irji nnowu ndu tsro ba granma ikpye waa a tie weiwiere a. A tru meleka ma ye ni Yohanna ye nhra wa.
2 Yohana alitoa ushuhuda wa kila kitu alichoona kuhusiana na neno la Mungu na kwa ushuhuda uliotolewa kuhusu Yesu Kristo.
Yohanna ahla lantre Rji nda hla u Yseu Kristi u kyi wa atoh wawumbambawu.
3 Amebarikiwa yeye asomaye kwa sauti na wale wote wanaoyasikia maneno ya unabii huu na kutii kilichoandikwa humo, kwa sababu muda umekaribia.
Indi uluw ahi wa akra totsuma ma ngbangban me'a ma kii biwa mba tsi wo tre waatre nda kpa nyemen ni kpe wa mba ha nimi into a he whewhir.
4 Yohana, kwa makanisa saba yaliyoko Asia: neema iwe kwenu na amani kutoka kwake aliyepo, aliyekuwepo, na atakayekuja, na kutoka kwa roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi,
Ime, Yohanna, hi ni Ikilisiyoyi tagban wa mba he nigbu mba asiya; tsitsi hi niyi ni sikpa ni wa ahe tsizan, wa he ni tsenmu, wawu ni ye ni shi-shi ruhohin tagban wa mba he ni kgbu kursiyin ma.
5 na kutoka kwa Yesu Kristo ambaye ni shahidi mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mtawala wa wafalme wa dunia hii. Kwake yeye atupendaye na ametuweka huru kutoka katika dhambi zetu kwa damu yake,
Arji ni Yesu Kristi wa mba kpanyemen ni wu, iver mumla wa alude nimi mben; wa atu chu bi gbugbu ni wa ni sonta. nda situ ihuwo ni la bi latre gbu ni iyinman.
6 ametufanya kuwa ufalme, makuhani wa Mungu na Baba yake - kwake kuwa utukufu na nguvu milele daima. Amina. (aiōn g165)
Aleta te bi chu firistoci bi Rji ma ni teman. ndidin, ukpele wi he ai wu tun nitse ahemen (amin) (aiōn g165)
7 Tazama, anakuja na mawingu; kila jicho litamwona, pamoja na wote waliomchoma. Na kabila zote za dunia wataomboleza kwake. Ndiyo, Amina.
Nya atsiye nimi kpan, shishi nde mbato ni nde biwa tugbu ni njigba ndi bi gbugbu pepemen mbayin niwu, ahemen (amin).
8 “Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu, “Yeye aliyepo, na aliyekuwepo, na ambaye anakuja, Mwenye nguvu.”
Ameyin mumudin ni klekle Irji treme wawu zizan; wa ahe tu nitsemu, wawu niyen, wawu ni kpekple wawu.
9 Mimi, Yohana - ndugu yenu na mmoja anayeshiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na uvumilivu thabiti ulio katika Yesu; nilikuwa katika kisiwa kiitwacho Patimo kwa sababu ya neno la Mungu na ushuhuda kuhusu Yesu.
Eme, Yohanna, rayinbin, wa ahe niyin ni mi iyabin, ni son ndidi ni fusroun waube ni Yesu. Igbulu mba wambayo Badmusa, ni tre Rji wa ala ni tu Yesu.
10 Nilikuwa katika Roho siku ya Bwana. Nilisikia nyuma yangu sauti ya juu kama ya tarumbeta,
Mi he nimi Ruhu nifi u Rji, ndi wo lanri ni kwugon nu na ijun.
11 ikisema, “andika katika kitabu unayo yaona, na uyatume kwa makanisa saba, kwenda Efeso, kwenda Smirna, kwenda Pergamo, kwenda Thiatira, kwenda Sardi, kwenda Philadelphia, na kwenda Laodikia.”
Ala ha ikpe wawu to rinu vuvu; nde tru hi ni Ikilisiyoyin tagban mba; wa ahe Afisus; ni Simirna, waahe ni Tayatira, wa ahe ni Sardisu, waahe ni Filadalfiya, ni waahe ni Laudikiya.
12 Nikageuka kuona ni sauti ya nani aliyekuwa akiongea nami, na nilipogeuka niliona kinara cha dhahabu cha taa saba.
Mi ya ndi atsi tre nimen, wa mi ya miton ilu fitila tagban ni ngbugbu klomba.
13 Katikati ya kinara cha taa alikuwemo mmoja kama Mwana wa Adamu, amevaa kanzu ndefu iliyofika chini ya miguu yake, na mkanda wa dhababu kuzunguka kifua chake.
Nimi ilu nde ri hena ker nde a kri ni gla gagloma hi ni zanma, alakpa ni zinariya nitsan ma.
14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe kama theluji, na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto.
Ituma ni fukpa kye na fu fu rjurju na men atsi gji ni kpama; shishi ahe na wau.
15 Nyayo zake zilikuwa kama shaba iliyosuguliwa sana, kama shaba ambayo imekwisha pitishwa katika moto, na sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji mengi yanayotiririka kwa kasi.
Izama mba kpa, mbahe na klalu wa mba la niwu, atsi glo na man ni nei.
16 Alikuwa ameshikilia nyota saba katika mkono wake wa kuume, na kutoka kinywani mwake kulikuwa na upanga mkali wenye makali kuwili. Uso wake ulikuwa uking'aa kama mwanga mkali wa jua.
Nuwo kota ma agji tsitse tangba ni nyuma agji gjin e. nyu ha shishi ma tsi kpa na rji.
17 Nilipomwona, nikaanguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kulia juu yangu na kusema, “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa Mwisho,
Wa mi tori mi jeku nza ma na kgbu nde. akawo ma ikita san ni tu mu nda la, na ti tsitsirena, imee mi mumle ni nklekle.
18 na ambaye ninaishi. Nalikuwa nimekufa, lakini tazama, ninaishi milele! Na ninazo funguo za mauti na kuzimu. (aiōn g165, Hadēs g86)
Niwa ahe, mi kwu nya mi he nitse mi he ni mukuli re mba u kwu ni iko lu. (aiōn g165, Hadēs g86)
19 Kwa hiyo, yaandike uliyoyaona, yaliyopo sasa, na yale yatakayotokea baada ya haya.
A he nawa, ha kpe wawu to igpi waahe zizan, waani he ni kwogon waujin.
20 Kwa maana iliyojificha kuhusu nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume, na kile kinara cha dhahabu cha taa saba: nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba, na kinara cha taa saba ni yale makanisa saba.”
Mi tu ma'ana, ni tsitse tagban wa mba to niwo kotama, ni whirji wa mbalo. Fitila tagban u Zinariya. tsitse tagban mba malaiku (pastoci) bi Ikilisiya tagban, whi rji mba lo fitilu tagban mba Ikilisiyoyi tagban mba.

< Ufunuo 1 >