< Zaburi 1 >

1 Amebarikiwa mtu yule asiye enenda katika ushauri wa waovu, au kusimama katika njia ya wenye dhambi, au kukaa katika kusanyiko la wenye mizaha.
Selig der Mann, der in der Ungerechten Rat nicht wandelt, und auf der Sünder Weg nicht steht, noch sitzet auf der Spötter Sitz.
2 Bali yeye huifurahia sheria ya Yahwe, na huitafakari sheria yake mchana na usiku.
Sondern hat seine Lust am Gesetze Jehovahs, und sinnet in Seinem Gesetze Tag und Nacht.
3 Atakuwa kama mti uliopandwa karibu na mkondo wa maji ambao huzaa matunda yake kwa majira yake, ambao majani yake hayakauki; lolote afanyalo litafanikiwa.
Und er ist wie ein Baum gepflanzet an Bächlein der Wasser, der seine Frucht gibt zu seiner Zeit und seine Blätter welken nicht, und alles, was er tut, gelingt.
4 Waovu hawako hivyo, wao badala yake ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
Nicht so die Ungerechten, sondern wie die Spreu sind sie, welche der Wind vertreibt.
5 Kwa hivyo waovu hawatasimama katika hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
Darum bestehen die Ungerechten nicht im Gericht, noch die Sünder in der Gemeinde der Gerechten.
6 Kwa kuwa Yahweh huikubali njia ya wenye haki, njia ya waovu itaangamizwa.
Denn Jehovah kennt den Weg der Gerechten, aber der Ungerechten Weg vergeht.

< Zaburi 1 >