< Zaburi 1 >

1 Amebarikiwa mtu yule asiye enenda katika ushauri wa waovu, au kusimama katika njia ya wenye dhambi, au kukaa katika kusanyiko la wenye mizaha.
Blessed is the man who has not walked in the counsel of the ungodly, and has not stood in the way of sinners, and has not sat in the seat of evil men.
2 Bali yeye huifurahia sheria ya Yahwe, na huitafakari sheria yake mchana na usiku.
But his pleasure is in the law of the Lord; and in his law will he meditate day and night.
3 Atakuwa kama mti uliopandwa karibu na mkondo wa maji ambao huzaa matunda yake kwa majira yake, ambao majani yake hayakauki; lolote afanyalo litafanikiwa.
And he shall be as a tree planted by the brooks of waters, which shall yield its fruit in its season, and its leaf shall not fall off; and whatsoever he shall do shall be prospered.
4 Waovu hawako hivyo, wao badala yake ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
Not so the ungodly; —not so: but rather as the chaff which the wind scatters away from the face of the earth.
5 Kwa hivyo waovu hawatasimama katika hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
Therefore the ungodly shall not rise in judgment, nor sinners in the counsel of the just.
6 Kwa kuwa Yahweh huikubali njia ya wenye haki, njia ya waovu itaangamizwa.
For the Lord knows the way of the righteous; but the way of the ungodly shall perish.

< Zaburi 1 >