< Zaburi 98 >
1 Oh, mwimbieni Yahwe wimbo mpya, kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu; mkono wake wa kuume na mkono wake mtakatifu vimempa ushindi.
Un salmo. Cantad a Yahvé un cántico nuevo, porque ha hecho cosas maravillosas. Su mano derecha y su brazo santo han obrado la salvación para él.
2 Yahwe ameufanya wokovu wake ujulikane; ameidhihirisha haki yake kwa mataifa yote.
Yahvé ha dado a conocer su salvación. Ha mostrado abiertamente su justicia a la vista de las naciones.
3 Hukumbuka uaminifu wa agano lake na uaminifu kwa ajili ya nyumba ya Israeli; miisho yote ya dunia itauona ushindi wa Mungu wetu.
Se ha acordado de su amorosa bondad y de su fidelidad hacia la casa de Israel. Todos los confines de la tierra han visto la salvación de nuestro Dios.
4 Mshangilieni Yahwe, nchi yote; pazeni sauti kwa wimbo, imbeni kwa furaha, na imbeni sifa.
¡Aclamad a Yahvé, toda la tierra! Estalla y canta de alegría, sí, ¡canta alabanzas!
5 Mwimbieni Yahwe sifa kwa kinubi, kwa kinubi na wimbo wenye muiki wa kupendeza.
Canten alabanzas a Yahvé con el arpa, con el arpa y la voz de la melodía.
6 Kwa panda na sauti ya baragumu, fanyeni kelele za shangwe mbele ya Mfalme, Yahwe.
Con trompetas y sonido de cuerno de carnero, hagan un ruido alegre ante el Rey, Yahvé.
7 Bahari na ipige kelele na vyote vilivyomo, ulimwengu na wale wakaao ndani yake!
Que el mar ruja con su plenitud; el mundo y los que lo habitan.
8 Mito na ipige makofi, na milima ipige kelele kwa furaha.
Que los ríos aplaudan. Que las montañas canten juntas de alegría.
9 Yahwe anakuja kuihukumu nchi; naye ataihukumu dunia kwa haki na mataifa kwa adili.
Quecanten ante Yahvé, porque viene a juzgar la tierra. Él juzgará al mundo con justicia, y los pueblos con equidad.