< Zaburi 97 >

1 Yahwe anatawala; nchi ishangilie; visiwa vingi na vifurahi.
主は王となられた。地は楽しみ、海に沿った多くの国々は喜べ。
2 Mawingu na giza vyamzunguka. Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chake.
雲と暗やみとはそのまわりにあり、義と正とはそのみくらの基である。
3 Moto huenda mbele zake nao huwateketeza adui zake pande zote.
火はそのみ前に行き、そのまわりのあだを焼きつくす。
4 Taa yake huangaza ulimwengu; nchi huona na kutetemeka.
主のいなずまは世界を照し、地は見ておののく。
5 Milima huyeyuka kama nta mbele za Yahwe, Bwana wa dunia yote.
もろもろの山は主のみ前に、全地の主のみ前に、ろうのように溶けた。
6 Mbingu hutangaza haki yake, na mataifa yote huuona utukufu wake.
もろもろの天はその義をあらわし、よろずの民はその栄光を見た。
7 Wale wote waabuduo sanamu za kuchonga wataaibishwa, wale wanao jivuna katika sanamu zisizo na maana mpigieni yeye magoti, enyi miungu wote!
すべて刻んだ像を拝む者、むなしい偶像をもってみずから誇る者ははずかしめをうける。もろもろの神は主のみ前にひれ伏す。
8 Sayuni ilisikia na kufurahi, na miji ya Yuda ilishangilia kwa sababu ya amri zako za haki, Yahwe.
主よ、あなたのさばきのゆえに、シオンは聞いて喜び、ユダの娘たちは楽しむ。
9 Kwa kuwa wewe, Yahwe, ndiye uliye juu sana, juu ya nchi yote. Umetukuka sana juu ya miungu yote.
主よ、あなたは全地の上にいまして、いと高く、もろもろの神にまさって大いにあがめられます。
10 Ninyi ambao mnampenda Yahwe, chukieni uovu! Yeye hulinda uhai wa watakatifu wake, naye huwatoa mikononi mwa waovu.
主は悪を憎む者を愛し、その聖徒のいのちを守り、これを悪しき者の手から助け出される。
11 Nuru imepandwa kwa ajili ya wenye haki na furaha kwa ajili ya wanyoofu wa moyo.
光は正しい人のために現れ、喜びは心の正しい者のためにあらわれる。
12 Furahini katika Yahwe, enyi wenye haki; na mpeni shukurani mkumbukapo utakatifu wake.
正しき人よ、主によって喜べ、その聖なるみ名に感謝せよ。

< Zaburi 97 >