< Zaburi 96 >

1 Oh, mwimbieni Yahwe wimbo mpya; mwimbieni Yahwe, nchi yote.
¡Canten a Yavé un canto nuevo! ¡Cante a Yavé toda la tierra!
2 Mwimbieni Yahwe, tukuzeni jina lake; tangazeni wokovu wake siku hadi siku.
¡Canten a Yavé, bendigan su Nombre! Anuncien de día en día su salvación.
3 Tangazeni utukufu wake kati ya mataifa, matendo yake ya ajabu kati ya mataifa.
Proclamen su gloria entre las naciones, Entre todos los pueblos, sus maravillosas obras.
4 Maana Yahwe ni mkuu na wakusifiwa sana. Ni wakuhofiwa kuliko miungu mingine.
Porque grande es Yavé Y digno de suprema alabanza. Él debe ser temido por encima de todos los ʼelohim.
5 Maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, bali ni Yahwe aliye zifanya mbingu.
Porque todos los ʼelohim de los pueblos son ídolos. Pero Yavé hizo los cielos.
6 Heshima na adhama ziko mbele zake. Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake.
Esplendor y majestad hay ante Él. Fortaleza y hermosura hay en su Santuario.
7 Mpeni Yahwe sifa, enyi ukoo wa watu, mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
Tributen a Yavé, oh familias de los pueblos. Tributen a Yavé gloria y fortaleza.
8 Mpeni Yahwe utukufu ambao unastahili jina lake. Leteni matoleo na muingie nyuani mwake.
Tributen a Yavé la gloria debida a su Nombre. Lleven ofrenda y entren en sus patios.
9 Mpigieni magoti Yahwe mkiwa mmevaa mavazi ambayo yanaheshimu utakatifu wake. Nchi yote tetemekeni mbele zake.
Adoren a Yavé en la hermosura de la santidad. Tiemble ante Él toda la tierra.
10 Semeni kati ya mataifa, Yahwe anatawala.” Ulimwengu pia umeimarishwa; hauwezi kutikiswa. Yeye huwahukumu watu kwa haki.
Digan entre las naciones: ¡Yavé reina! Ciertamente el mundo está firmemente establecido. No será conmovido. Él juzgará a los pueblos con equidad.
11 Mbingu na zifurahi, na nchi ishangilie; bahari na ivume na vyote viijazavyo vipige kelele kwa shangwe.
¡Alégrense los cielos Y regocíjese la tierra! Brame el mar y todo lo que contiene.
12 Mashamba yashangilie na vyote vilivyomo. Kisha miti ya mstuni ipige kelele kwa furaha
Exáltese el campo y todo lo que hay en él. Entonces todos los árboles del bosque cantarán con gozo
13 mbele za Yahwe, maana yeye anakuja. Anakuja kuihukumu nchi. Naye atauhukumu ulumwengu kwa haki na mataifa kwa uaminifu wake.
Delante de Yavé Quien viene, Porque viene a juzgar la tierra. Él juzgará al mundo con justicia Y a los pueblos con su fidelidad.

< Zaburi 96 >