< Zaburi 96 >

1 Oh, mwimbieni Yahwe wimbo mpya; mwimbieni Yahwe, nchi yote.
Cantae ao Senhor um cantico novo, cantae ao Senhor toda a terra.
2 Mwimbieni Yahwe, tukuzeni jina lake; tangazeni wokovu wake siku hadi siku.
Cantae ao Senhor, bemdizei o seu nome; annunciae a sua salvação de dia em dia.
3 Tangazeni utukufu wake kati ya mataifa, matendo yake ya ajabu kati ya mataifa.
Annunciae entre as nações a sua gloria; entre todos os povos as suas maravilhas.
4 Maana Yahwe ni mkuu na wakusifiwa sana. Ni wakuhofiwa kuliko miungu mingine.
Porque grande é o Senhor, e digno de louvor, mais tremendo do que todos os deuses.
5 Maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, bali ni Yahwe aliye zifanya mbingu.
Porque todos os deuses dos povos são idolos, mas o Senhor fez os céus.
6 Heshima na adhama ziko mbele zake. Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake.
Gloria e magestade estão ante a sua face, força e formosura no seu sanctuario.
7 Mpeni Yahwe sifa, enyi ukoo wa watu, mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
Dae ao Senhor, ó familias dos povos, dae ao Senhor gloria e força.
8 Mpeni Yahwe utukufu ambao unastahili jina lake. Leteni matoleo na muingie nyuani mwake.
Dae ao Senhor a gloria devida ao seu nome: trazei offerenda, e entrae nos seus atrios.
9 Mpigieni magoti Yahwe mkiwa mmevaa mavazi ambayo yanaheshimu utakatifu wake. Nchi yote tetemekeni mbele zake.
Adorae ao Senhor na belleza da sanctidade: tremei diante d'elle toda a terra.
10 Semeni kati ya mataifa, Yahwe anatawala.” Ulimwengu pia umeimarishwa; hauwezi kutikiswa. Yeye huwahukumu watu kwa haki.
Dizei entre as nações que o Senhor reina: o mundo tambem se firmará para que se não abale: julgará os povos com rectidão.
11 Mbingu na zifurahi, na nchi ishangilie; bahari na ivume na vyote viijazavyo vipige kelele kwa shangwe.
Alegrem-se os céus, e regozije-se a terra: brama o mar e a sua plenitude.
12 Mashamba yashangilie na vyote vilivyomo. Kisha miti ya mstuni ipige kelele kwa furaha
Alegre-se o campo com tudo o que ha n'elle: então se regozijarão todas as arvores do bosque,
13 mbele za Yahwe, maana yeye anakuja. Anakuja kuihukumu nchi. Naye atauhukumu ulumwengu kwa haki na mataifa kwa uaminifu wake.
Ante a face do Senhor, porque vem, porque vem a julgar a terra: julgará o mundo com justiça e os povos com a sua verdade.

< Zaburi 96 >