< Zaburi 96 >
1 Oh, mwimbieni Yahwe wimbo mpya; mwimbieni Yahwe, nchi yote.
O sing to the LORD a new song: sing to the LORD, all the earth.
2 Mwimbieni Yahwe, tukuzeni jina lake; tangazeni wokovu wake siku hadi siku.
Sing to the LORD, bless his name; show forth his salvation from day to day.
3 Tangazeni utukufu wake kati ya mataifa, matendo yake ya ajabu kati ya mataifa.
Declare his glory among the heathen, his wonders among all people.
4 Maana Yahwe ni mkuu na wakusifiwa sana. Ni wakuhofiwa kuliko miungu mingine.
For the LORD [is] great, and greatly to be praised: he [is] to be feared above all gods.
5 Maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, bali ni Yahwe aliye zifanya mbingu.
For all the gods of the nations [are] idols: but the LORD made the heavens.
6 Heshima na adhama ziko mbele zake. Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake.
Honor and majesty [are] before him: strength and beauty [are] in his sanctuary.
7 Mpeni Yahwe sifa, enyi ukoo wa watu, mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
Give to the LORD, O ye kindreds of the people, give to the LORD glory and strength.
8 Mpeni Yahwe utukufu ambao unastahili jina lake. Leteni matoleo na muingie nyuani mwake.
Give to the LORD the glory [due to] his name: bring an offering, and come into his courts.
9 Mpigieni magoti Yahwe mkiwa mmevaa mavazi ambayo yanaheshimu utakatifu wake. Nchi yote tetemekeni mbele zake.
O worship the LORD in the beauty of holiness: fear before him, all the earth.
10 Semeni kati ya mataifa, Yahwe anatawala.” Ulimwengu pia umeimarishwa; hauwezi kutikiswa. Yeye huwahukumu watu kwa haki.
Say among the heathen [that] the LORD reigneth: the world also shall be established that it shall not be moved: he will judge the people righteously.
11 Mbingu na zifurahi, na nchi ishangilie; bahari na ivume na vyote viijazavyo vipige kelele kwa shangwe.
Let the heavens rejoice, and let the earth be glad; let the sea roar, and the fullness of it.
12 Mashamba yashangilie na vyote vilivyomo. Kisha miti ya mstuni ipige kelele kwa furaha
Let the field be joyful, and all that [is] in it: then shall all the trees of the wood rejoice before the LORD:
13 mbele za Yahwe, maana yeye anakuja. Anakuja kuihukumu nchi. Naye atauhukumu ulumwengu kwa haki na mataifa kwa uaminifu wake.
For he cometh, for he cometh to judge the earth: he will judge the world with righteousness, and the people with his truth.