< Zaburi 96 >
1 Oh, mwimbieni Yahwe wimbo mpya; mwimbieni Yahwe, nchi yote.
Sing to Adonai a new song! Sing to Adonai, all the earth.
2 Mwimbieni Yahwe, tukuzeni jina lake; tangazeni wokovu wake siku hadi siku.
Sing to Adonai! Bless his name! Proclaim his yishu'ah ·salvation· from day to day!
3 Tangazeni utukufu wake kati ya mataifa, matendo yake ya ajabu kati ya mataifa.
Declare his kavod ·weighty glory· among the nations, his marvelous works among all the peoples.
4 Maana Yahwe ni mkuu na wakusifiwa sana. Ni wakuhofiwa kuliko miungu mingine.
For great is Adonai, and greatly to be praised! He is to be feared above all deities.
5 Maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, bali ni Yahwe aliye zifanya mbingu.
For all the deities of the peoples are idols, but Adonai made the heavens.
6 Heshima na adhama ziko mbele zake. Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake.
Honor and majesty are before him. Strength and beauty are in his sanctuary.
7 Mpeni Yahwe sifa, enyi ukoo wa watu, mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
Ascribe to Adonai, you families of nations, ascribe to Adonai kavod ·weighty glory· and strength.
8 Mpeni Yahwe utukufu ambao unastahili jina lake. Leteni matoleo na muingie nyuani mwake.
Ascribe to Adonai the kavod ·weighty glory· due to his name. Bring an offering, and come into his courts.
9 Mpigieni magoti Yahwe mkiwa mmevaa mavazi ambayo yanaheshimu utakatifu wake. Nchi yote tetemekeni mbele zake.
Hawa ·Bow low, prostrate· to worship Adonai in holy array. Tremble before him, all the earth.
10 Semeni kati ya mataifa, Yahwe anatawala.” Ulimwengu pia umeimarishwa; hauwezi kutikiswa. Yeye huwahukumu watu kwa haki.
Say among the nations, “Adonai reigns.” The world is also established. It can’t be moved. He will judge the peoples with equity.
11 Mbingu na zifurahi, na nchi ishangilie; bahari na ivume na vyote viijazavyo vipige kelele kwa shangwe.
Let the heavens be glad, and let the earth rejoice. Let the sea roar, and its fullness!
12 Mashamba yashangilie na vyote vilivyomo. Kisha miti ya mstuni ipige kelele kwa furaha
Let the field and all that is in it exult! Then all the trees of the woods shall sing for joy
13 mbele za Yahwe, maana yeye anakuja. Anakuja kuihukumu nchi. Naye atauhukumu ulumwengu kwa haki na mataifa kwa uaminifu wake.
before Adonai; for he comes, for he comes to judge the earth. He will judge the world with righteousness, the peoples with his truth.