< Zaburi 96 >
1 Oh, mwimbieni Yahwe wimbo mpya; mwimbieni Yahwe, nchi yote.
Oh sing unto the Lord a new song: sing unto the Lord, all the lands.
2 Mwimbieni Yahwe, tukuzeni jina lake; tangazeni wokovu wake siku hadi siku.
Sing unto the Lord, bless his name: announce from day to day his salvation.
3 Tangazeni utukufu wake kati ya mataifa, matendo yake ya ajabu kati ya mataifa.
Relate among the nations his honor, among all the people his wonders.
4 Maana Yahwe ni mkuu na wakusifiwa sana. Ni wakuhofiwa kuliko miungu mingine.
For the Lord is great, and greatly praised: he is to be feared above all gods.
5 Maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, bali ni Yahwe aliye zifanya mbingu.
For all the gods of the nations are idols; but the Lord hath made the heavens.
6 Heshima na adhama ziko mbele zake. Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake.
Glory and majesty are before him: strength and beauty are in his sanctuary.
7 Mpeni Yahwe sifa, enyi ukoo wa watu, mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
Ascribe unto the Lord, O ye families of the people, ascribe unto the Lord honor and strength.
8 Mpeni Yahwe utukufu ambao unastahili jina lake. Leteni matoleo na muingie nyuani mwake.
Ascribe unto the Lord the honor [due unto] his name: bear hither a present, and come unto his courts.
9 Mpigieni magoti Yahwe mkiwa mmevaa mavazi ambayo yanaheshimu utakatifu wake. Nchi yote tetemekeni mbele zake.
Bow down unto the Lord in the beauty of holiness: tremble before him, all ye lands.
10 Semeni kati ya mataifa, Yahwe anatawala.” Ulimwengu pia umeimarishwa; hauwezi kutikiswa. Yeye huwahukumu watu kwa haki.
Say among the nations, “The Lord reigneth;” [therefore] also the world is ever firmly established that it shall hot be moved: he will judge the people in equity.
11 Mbingu na zifurahi, na nchi ishangilie; bahari na ivume na vyote viijazavyo vipige kelele kwa shangwe.
Let the heavens rejoice, and let the earth be glad: let the sea roar, with all that filleth it.
12 Mashamba yashangilie na vyote vilivyomo. Kisha miti ya mstuni ipige kelele kwa furaha
Let the field exult, and all that is therein: then shall all the trees of the forest sing for joy,
13 mbele za Yahwe, maana yeye anakuja. Anakuja kuihukumu nchi. Naye atauhukumu ulumwengu kwa haki na mataifa kwa uaminifu wake.
Before the Lord; for he cometh, for he cometh to judge the earth: he will judge the world with righteousness, and people in his truth.