< Zaburi 96 >

1 Oh, mwimbieni Yahwe wimbo mpya; mwimbieni Yahwe, nchi yote.
Sing vnto the Lord a newe song: sing vnto the Lord, all the earth.
2 Mwimbieni Yahwe, tukuzeni jina lake; tangazeni wokovu wake siku hadi siku.
Sing vnto the Lord, and prayse his Name: declare his saluation from day to day.
3 Tangazeni utukufu wake kati ya mataifa, matendo yake ya ajabu kati ya mataifa.
Declare his glory among all nations, and his wonders among all people.
4 Maana Yahwe ni mkuu na wakusifiwa sana. Ni wakuhofiwa kuliko miungu mingine.
For the Lord is great and much to be praysed: he is to be feared aboue all gods.
5 Maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, bali ni Yahwe aliye zifanya mbingu.
For all the gods of the people are idoles: but the Lord made the heauens.
6 Heshima na adhama ziko mbele zake. Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake.
Strength and glory are before him: power and beautie are in his Sanctuarie.
7 Mpeni Yahwe sifa, enyi ukoo wa watu, mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
Giue vnto the Lord, ye families of the people: giue vnto the Lord glory and power.
8 Mpeni Yahwe utukufu ambao unastahili jina lake. Leteni matoleo na muingie nyuani mwake.
Giue vnto the Lord the glory of his Name: bring an offering, and enter into his courtes.
9 Mpigieni magoti Yahwe mkiwa mmevaa mavazi ambayo yanaheshimu utakatifu wake. Nchi yote tetemekeni mbele zake.
Worship the Lord in the glorious Sanctuarie: tremble before him all the earth.
10 Semeni kati ya mataifa, Yahwe anatawala.” Ulimwengu pia umeimarishwa; hauwezi kutikiswa. Yeye huwahukumu watu kwa haki.
Say among the nations, The Lord reigneth: surely the world shalbe stable, and not moue, and he shall iudge the people in righteousnesse.
11 Mbingu na zifurahi, na nchi ishangilie; bahari na ivume na vyote viijazavyo vipige kelele kwa shangwe.
Let the heauens reioyce, and let the earth be glad: let the sea roare, and all that therein is.
12 Mashamba yashangilie na vyote vilivyomo. Kisha miti ya mstuni ipige kelele kwa furaha
Let the field be ioyfull, and all that is in it: let all the trees of the wood then reioyce
13 mbele za Yahwe, maana yeye anakuja. Anakuja kuihukumu nchi. Naye atauhukumu ulumwengu kwa haki na mataifa kwa uaminifu wake.
Before the Lord: for he commeth, for he cometh to iudge the earth: he wil iudge the world with righteousnes, and the people in his trueth.

< Zaburi 96 >