< Zaburi 95 >

1 Oh njoni, tumwimbie Yahwe; na tumwimbie kwa shangwe mwamba wa wokovu wetu.
לכו נרננה ליהוה נריעה לצור ישענו
2 Tuingie uweponi mwake kwa shukrani; tumwimbie yeye kwa zaburi ya sifa.
נקדמה פניו בתודה בזמרות נריע לו
3 Kwa maana Yahwe ni Mungu mkuu na Mfalme mkuu juu ya miungu yote.
כי אל גדול יהוה ומלך גדול על-כל-אלהים
4 Mkononi mwake zimo bonde za dunia; navyo vilele vya milima ni vyake.
אשר בידו מחקרי-ארץ ותועפת הרים לו
5 Bahari ni yake, maana aliiumba, na mikono yake ilitengeneza nchi kavu.
אשר-לו הים והוא עשהו ויבשת ידיו יצרו
6 Oh njoni, tumwabudu na tupige magoti; tupige magoti mbele za Yahwe, muumbaji wetu:
באו נשתחוה ונכרעה נברכה לפני-יהוה עשנו
7 Kwa maana yeye ni Mungu wetu, na sisi tu watu wa malisho yake na kondoo wa mkono wake. Ni heri leo mngesikia sauti yake!
כי הוא אלהינו-- ואנחנו עם מרעיתו וצאן ידו היום אם-בקלו תשמעו
8 Msiifanye migumu mioyo yenu, kama vile huko Meriba, au kama ile siku ya Masa jangwani,
אל-תקשו לבבכם כמריבה כיום מסה במדבר
9 ambako baba zenu walinijaribu na kunipima, japo walikuwa wameyaona matendo yangu.
אשר נסוני אבותיכם בחנוני גם-ראו פעלי
10 Kwa miaka arobaini nilikasirishwa na kizazi hicho na kusema, 'Hawa ni watu ambao mioyo yao imepotoka; hawazijui njia zangu.'
ארבעים שנה אקוט בדור-- ואמר עם תעי לבב הם והם לא-ידעו דרכי
11 Hivyo katika hasira yangu niliapa kwamba wasingeingia kamwe mahali pa pumziko.”
אשר-נשבעתי באפי אם-יבאון אל-מנוחתי

< Zaburi 95 >