< Zaburi 95 >
1 Oh njoni, tumwimbie Yahwe; na tumwimbie kwa shangwe mwamba wa wokovu wetu.
請大家前來向上主歡呼,齊向救助我們的磐石歌舞。
2 Tuingie uweponi mwake kwa shukrani; tumwimbie yeye kwa zaburi ya sifa.
一齊到祂面前感恩讚頌,向祂歌唱聖詩,歡呼吟詠。
3 Kwa maana Yahwe ni Mungu mkuu na Mfalme mkuu juu ya miungu yote.
因為上主是尊高的天主,是超越諸神的偉大聖主;
4 Mkononi mwake zimo bonde za dunia; navyo vilele vya milima ni vyake.
大地深淵都在祂的手中,高山崚嶺都是祂的化工。
5 Bahari ni yake, maana aliiumba, na mikono yake ilitengeneza nchi kavu.
海洋屬於祂,因為是祂所創造;陸地屬於祂,因為是祂所形成。
6 Oh njoni, tumwabudu na tupige magoti; tupige magoti mbele za Yahwe, muumbaji wetu:
請大家前來叩首致敬,向造我們的上主跪拜。
7 Kwa maana yeye ni Mungu wetu, na sisi tu watu wa malisho yake na kondoo wa mkono wake. Ni heri leo mngesikia sauti yake!
因為祂是我們的真神,我們是祂牧養的人民,是祂親手引導的羊群。您們今天該聽從祂的聲音:
8 Msiifanye migumu mioyo yenu, kama vile huko Meriba, au kama ile siku ya Masa jangwani,
不要再像在默黎巴那樣心頑,也不要像在曠野中瑪撒那天!
9 ambako baba zenu walinijaribu na kunipima, japo walikuwa wameyaona matendo yangu.
您們的祖先雖然見過我的工作,在那裏他們還是試探我,考驗我。
10 Kwa miaka arobaini nilikasirishwa na kizazi hicho na kusema, 'Hawa ni watu ambao mioyo yao imepotoka; hawazijui njia zangu.'
四十年之久,我厭惡了那一世代,曾說:這百姓心中迷惑,不肯承認我的真道,
11 Hivyo katika hasira yangu niliapa kwamba wasingeingia kamwe mahali pa pumziko.”
因此我懷著憤怒而起說:他們決不得進入我的的安所。