< Zaburi 94 >
1 Yahwe, Ee Mungu ulipaye kisasi, Mungu ulipaye kisasi, utuangazie sisi.
JEHOVÁ, Dios de las venganzas, Dios de las venganzas, muéstrate.
2 Inuka, muhukumu wa nchi, uwape wenye majivuno kile wanachosahili.
Ensálzate, oh Juez de la tierra: da el pago á los soberbios.
3 Mpaka lini waovu, Yahwe, mpaka lini waovu watafurahia?
¿Hasta cuándo los impíos, hasta cuándo, oh Jehová, se gozarán los impíos?
4 Wanamwaga maneno yao ya kiburi; wote watendao uovu wanajivuna.
¿Hasta cuándo pronunciarán, hablarán cosas duras, y se vanagloriarán todos los que obran iniquidad?
5 Wanawaangamiza watu wako, Yahwe; wanalitesa taifa ambao ni milki yako.
A tu pueblo, oh Jehová, quebrantan, y á tu heredad afligen.
6 Wanamuua mjane na mgeni aishiye nchini mwao, na wanamuua yatima.
A la viuda y al extanjero matan, y á los huérfanos quitan la vida.
7 Nao husema, “Yahwe hawezi kuona, Mungu wa Yakobo hayagundui haya.”
Y dijeron: No verá JAH, ni entenderá el Dios de Jacob.
8 Tambueni, ninyi watu wajinga! Enyi wapumbavu, mtajifunza lini?
Entended, necios del pueblo; y vosotros fatuos, ¿cuándo seréis sabios?
9 Yeye aliye liumba sikio, hasikii? Yeye aliye litengeneza jicho, haoni?
El que plantó el oído, ¿no oirá? el que formó el ojo, ¿no verá?
10 Yeye awaadhibuye mataifa, hayuko sahihi? Yeye ndiye ampaye maarifa mwanadamu.
El que castiga las gentes, ¿no reprenderá? ¿no sabrá el que enseña al hombre la ciencia?
11 Yahwe anayajua mawazo ya wanadamu, kuwa ni mvuke.
Jehová conoce los pensamientos de los hombres, que son vanidad.
12 Amebarikiwa yule ambaye umuongozaye, Yahwe, yule ambaye wewe humfundisha kutoka katika sheria yako.
Bienaventurado el hombre á quien tú, JAH, castigares, y en tu ley lo instruyeres;
13 Wewe humpa pumziko wakati wa shida mpaka shimo litakapokuwa limechimbwa kwa ajili ya waovu.
Para tranquilizarle en los días de aflicción, en tanto que para el impío se cava el hoyo.
14 Maana Yahwe hatawaacha watu wake wala kutelekeza warithi wake.
Porque no dejará Jehová su pueblo, ni desamparará su heredad;
15 Kwa kuwa tena hukumu itakuwa ya haki; na wote walio wanyoofu wa moyo wataifuata.
Sino que el juicio será vuelto á justicia, y en pos de ella irán todos los rectos de corazón.
16 Ni nani atainuka kunitetea dhidi ya watendao uovu? Ni nani atasimama dhidi ya waovu kwa ajili yangu?
¿Quién se levantará por mí contra los malignos? ¿quién estará por mí contra los que obran iniquidad?
17 Kama Yahwe asingelikuwa msaada wangu, haraka ningekuwa nimelala mahali pa ukimya.
Si no me ayudara Jehová, presto morara mi alma en el silencio.
18 Niliposema, mguu wangu unateleza,” Uaminifu wa agano lako, Yahwe, uliniinua.
Cuando yo decía: Mi pie resbala: tu misericordia, oh Jehová, me sustentaba.
19 Wasiwasi uwapo mwingi ndani yangu, faraja yako hunifurahisha.
En la multitud de mis pensamientos dentro de mí, tus consolaciones alegraban mi alma.
20 Kiti cha uharibifu chaweza kushirikiana nawe, kitungacho madhara kwa njia ya sheria?
¿Juntaráse contigo el trono de iniquidades, que forma agravio en el mandamiento?
21 Wao kwa pamoja hupanga njama kuwaua wenye haki na kuwahukumu adhabu ya kifo wenye haki.
Pónense en corros contra la vida del justo, y condenan la sangre inocente.
22 Lakini Yahwe amekuwa mnara wangu mrefu, na Mungu wangu amekuwa mwamba wa kimbilio langu.
Mas Jehová me ha sido por refugio; y mi Dios por roca de mi confianza.
23 Yeye atawarudishia uovu wao wenyewe na atawaangamiza katika uovu wao wenyewe. Yahwe Mungu wetu atawaangamiza.
Y él hará tornar sobre ellos su iniquidad, y los destruirá por su propia maldad; los talará Jehová nuestro Dios.