< Zaburi 93 >

1 Yahwe anatawala; amevikwa adhama; Yahwe amejivika na kujifunga nguvu. Ulimwengu umeimalishwa; hauwezi kusogezwa.
יהוה מלך גאות לבש לבש יהוה עז התאזר אף-תכון תבל בל-תמוט
2 Kiti chako cha enzi kimeimarishwa nyakati za kale; umekuwepo siku zote.
נכון כסאך מאז מעולם אתה
3 Bahari zimeinuka, Yahwe; zimemepaza sauti zao; mawimbi ya bahari yapiga ghasia na ngurumo.
נשאו נהרות יהוה--נשאו נהרות קולם ישאו נהרות דכים
4 Zaidi ya ghasia ya mawimbi mengi, mawimbi ya bahari yenye nguvu, Yahwe aliye juu ni mwenye nguvu.
מקלות מים רבים--אדירים משברי-ים אדיר במרום יהוה
5 Amri zako makini ni za kuaminika sana; utakatifu huipamba nyumba yako, Yahwe, milele.
עדתיך נאמנו מאד--לביתך נאוה-קדש יהוה לארך ימים

< Zaburi 93 >