< Zaburi 92 >

1 Ni jambo jema kumshukuru Yahwe na kuliimbia sifa jina lako, Uliye Juu,
psalmus cantici in die sabbati bonum est confiteri Domino et psallere nomini tuo Altissime
2 kutangaza uaminifu wa agano lako wakati wa asubuhi na uaminifu wako kila usiku,
ad adnuntiandum mane misericordiam tuam et veritatem tuam per noctem
3 kwa kinubi cha nyuzi kumi na kwa tuni ya kinubi.
in decacordo psalterio cum cantico in cithara
4 Kwa kuwa wewe, Yahwe, matendo yako yamenifurahisha. Nitaimba kwa furaha kwa sababu ya matendo ya mikono yako.
quia delectasti me Domine in factura tua et in operibus manuum tuarum exultabo
5 Ni jinsi gani matendo yako ni makuu, Yahwe! mawazo yako ni ya kina.
quam magnificata sunt opera tua Domine nimis profundae factae sunt cogitationes tuae
6 Mtu mpumbavu hawezi kuyajua, wala mjinga kuyaelewa haya:
vir insipiens non cognoscet et stultus non intelleget haec
7 Wasio haki watakapochipuka kama nyasi, na hata watendao uovu watakapo stawi, bado wataangamizwa kwenye uharibifu wa milele.
cum exorti fuerint peccatores sicut faenum et apparuerint omnes qui operantur iniquitatem ut intereant in saeculum saeculi
8 Lakini wewe, Yahwe, utatawala milele.
tu autem Altissimus in aeternum Domine
9 Hakika, watazame adui zako, Yahwe! Hakika, watazame adui zako. Wataangamia! Wale wote watendao maovu watatawanywa.
quoniam ecce inimici tui Domine; quoniam ecce inimici tui peribunt et dispergentur omnes qui operantur iniquitatem
10 Wewe umeyainua mapembe yangu kama mapembe ya Nyati wa porini; nimepakwa mafuta safi.
et exaltabitur sicut unicornis cornu meum et senectus mea in misericordia uberi
11 Macho yangu yameona kuanguka kwa adui zangu; masikio yangu yamesikia maangamizi ya maadui zangu waovu.
et despexit oculus meus inimicis meis et insurgentibus in me malignantibus audiet auris mea
12 Wenye haki watastawi kama mtende; watakua kama mwerezi wa Lebanoni.
iustus ut palma florebit ut cedrus Libani multiplicabitur
13 Wamepandwa katika nyumba ya Yahwe; wakistawi katika nyua za Mungu wetu.
plantati in domo Domini in atriis Dei nostri florebunt
14 Wao huzaa matunda hata uzeeni; hukaa safi na wenye afya,
adhuc multiplicabuntur in senecta uberi et bene patientes erunt
15 kutangaza kuwa Yahwe ni wa haki. Yeye ni mwamba wangu, na hakuna udhalimu ndani yake.
ut adnuntient quoniam rectus Dominus Deus noster et non est iniquitas in eo

< Zaburi 92 >